Nabii Tito sharti achunguzwe

Nabii Tito sharti achunguzwe

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
27,427
Reaction score
28,473
Kuna haja ya serikali kumchunguza nabii Titto kama inavyomchunguza Askofu Kakobe ili kubaini kama pombe anazokunywa hadharani kila kukicha anazinunua kwa fedha za sadaka au ana chanzo kingine cha kipato. Pia nitoe wito kwa TRA kuchunguza vyanzo vyote vya mapato vya nabii huyu ijiridhishe kama analipa kodi stahiki serikalini.

Pamoja na hayo, naishauri serikali imdhibiti Titto asiharibu kizazi cha watanzania kwa mahaubiri yake tata na yasiyozingatia biblia. Mungu hadhihakiwi. Siku zote serikali imekuwa mstari wa mbele kukemea udhalilishaji wa kijinsia, kuzuia maambukizi ya VVU na kuzuia mimba za utotoni. Lakini, ama kwa makusudi au kwa kutokujua, huyu nabii amekuwa mstari wa mbele kuhamasisha uvunjaji wa sheria, huku akijua fika anaenda kinyume na sheria za nchi na mafundisho ya dini.

Katika siku za hivi karibuni Nabii Titto ameonekana akihamasisha watu kunywa pombe. Unywaji wa pombe ni kinyume na azma ya serikali ya kupunguza ajali za barabarani kwani ajali nyingi husababishwa na madereva walevi pale wanaposhindwa kufanya maamuzi sahihi wanapokuwa barabarani. Juzi tumeshuhudia ajali iliyoua ndugu zetu 11 papo kwa papo na huenda dereva alikuwa amelewa. Mtu yeyote anayewahamasisha watu kunywa pombe ni wa kumuogopa kama ukoma.



Aidha, nabii huyu amekuwa akiwahamasisha akina baba kutembea na kuzaa na wajakazi (house maids) wao. Ili kusisitiza azma yake hiyo, amekuwa siku zote akitangaza kutembea na mjakazi wake na amekuwa akitamba hadharani. Kitendo cha kutembea na mjakazi sio tu kinaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa ya ngono na VVU, bali kinadhalilisha wanawake – kwamba wao ni viburudisho vya mabosi wao sehemu za kazi. Hapa haki za binadamu zimevunjwa. Mjakazi anayo haki ya kufanya kazi kwa uhuru pasipokuwa na wasiwasi wa kuingiliwa kimwili na “baba”. Kwa kweli, hili suala halijakaa sawa mbele za watetezi wa haki za wanawake.

Kana kwamba hilo halitoshi, nabii Titto amekuwa akivaa hereni masikioni mwake na kucheza nyimbo za taarabu, jambo linalohusishwa na ushoga. Kwa maana nyingine ni kwamba anatangaza vitendo vya kishoga hapa nchini. Vitendo, vya ushoga sio tu ni chukizo kwa serikali ila ni dhambi kubwa kwa Mungu.



Kufuatia matukio haya na mengine mengi ambayo nabii Titto amekuwa akijihusisha nayo, serikali haijakaa kimya. Juzi nimeongea na mtaalamu mmoja wa masuala ya kijamii akanitonya kwamba serikali inamsaka nabii Titto ili imfikisha katika vyombo vya sheria kwani vitendo vya uvunjivu wa maadili anavyofanya ni zaidi ya ugaidi.

Naungana na watanzania wazalendo kwa kukemea vitendo hivi na ninaipongeza serikali kwa hatua zake za kumuwajibisha nabii Titto ili liwe fundisho kwa wachochezi wengine wanaovunja sheria za nchi kwa makusudi. Najua kuna wafuasi wa nabii Titto wapo humu na wasingependa kuona nabii wao akitiwa msukosuko na serikali kwa namna yoyote ile. Tulizeni munkari. Sheria za nchi hazina dini. Ndio maana hadi sasa hivi polisi wanamhoji Askofu Kakobe kwa kuvunja sheria za nchi. Sheria ni msumeno.

Habari zaidi soma=>Polisi Dodoma: Daktari toka hospitali ya Milembe athibitisha kuwa nabii Tito ana tatizo la akili
 
Namshangaa sana anapohamasisha baba kulala na wajakazi wao. Hebu mtazame jinsi anavyokula denda kwa dada wa kazi kwenye video hapo juu. Hivi huyu hana ndugu? Kwanini hawamkanyi?
Kuna muda nahisigi in shetani kaja mzimamzima ,,kwa hali ya kawaisa kuna maswali mengi sana ya kujiuliza juu take hayana majibu,,ana wazazi? Jamii gani anaishi? Watoto je
 
Mkuu kwani huyo Nabii anakupunguzia au anakuongezea nini hasa katika maisha yako binafsi? Akikamatwa na Serikali ndiyo Muamala wako wa Kibenki au wa katika Simu yako utaongezeka? Tatizo ni kwamba hao Waumini unaohangaika hapa kuwapigania wengi wao ni ' Wapuuzi ' mno Kiimani na sidhani hata kama watakuelewa. Suala hapa siyo tu huyo Nabii bali ni kuwatahadharisha Watu juu ya hawa Viongozi wengi wa Makanisa haya ya Kiroho jinsi walivyo wa ' hovyo hovyo ' ili waachane nao mara moja. Tena kwa taarifa yako tu sasa bora hata ya huyo Nabii ambaye Yeye bila aibu kaamua ' Kujilipua ' hadharani hadi leo hii Wewe unamuona ' kapotoka ' Kimaadili ila Mimi kuna Viongozi wawili wa Kidini tena ni wakubwa hapa nchini ' matukio ' wanayoyafanya nadhani hata ya huyo Nabii yana afadhali na najua wale ' Watafiti ' wenzangu hapa tayari wameshawajua hao Viongozi wa Kiroho ninaowalenga hapa. Kuna mmoja wapo anavuta Bangi / Bange nadhani hata Hayati Bob Marley akifufuka leo na kumuoana anaweza kumpa Kombe la Ushindi huku mwingine akiwa ni hodari sana kwa ' Kuwabandua / Kuwabaioloji ' Wake za Watu tena katika Kanisa lake ambapo kuna Chumba chake ' maalum ' na mwaka jana alikoswakoswa ' Kiduchu ' tu katika ' mtego ' ili aliwe ' ndogo ' ila Malaika wake walimwokoa.

Kwa leo naomba niishie hapa tafadhali.
 
Mkuu kwani huyo Nabii anakupunguzia au anakuongezea nini hasa katika maisha yako binafsi? Akikamatwa na Serikali ndiyo Muamala wako wa Kibenki au wa katika Simu yako utaongezeka? Tatizo ni kwamba hao Waumini unaohangaika hapa kuwapigania wengi wao ni ' Wapuuzi ' mno Kiimani na sidhani hata kama watakuelewa. Suala hapa siyo tu huyo Nabii bali ni kuwatahadharisha Watu juu ya hawa Viongozi wengi wa Makanisa haya ya Kiroho jinsi walivyo wa ' hovyo hovyo ' ili waachane nao mara moja. Tena kwa taarifa yako tu sasa bora hata ya huyo Nabii ambaye Yeye bila aibu kaamua ' Kujilipua ' hadharani hadi leo hii Wewe unamuona ' kapotoka ' Kimaadili ila Mimi kuna Viongozi wawili wa Kidini tena ni wakubwa hapa nchini ' matukio ' wanayoyafanya nadhani hata ya huyo Nabii yana afadhali na najua wale ' Watafiti ' wenzangu hapa tayari wameshawajua hao Viongozi wa Kiroho ninaowalenga hapa. Kuna mmoja wapo anavuta Bangi / Bange nadhani hata Hayati Bob Marley akifufuka leo na kumuoana anaweza kumpa Kombe la Ushindi huku mwingine akiwa ni hodari sana kwa ' Kuwabandua / Kuwabaioloji ' Wake za Watu tena katika Kanisa lake ambapo kuna Chumba chake ' maalum ' na mwaka jana alikoswakoswa ' Kiduchu ' tu katika ' mtego ' ili aliwe ' ndogo ' ila Malaika wake walimwokoa.

Kwa leo naomba niishie hapa tafadhali.
Usikute wewe ndyo Huyo nabii
 
Nasema hivi, kati ya manabii wote wa kikristo huyu ndiye nabii asiye mnafiki peke yake manabii wengine wote waliobaki wa kikristo ni wanafiki tu.

Nampa sana hongera kwa kuuweka unafiki pembeni na aendelee hivyo hivyo aseee.

Safi Sana.
 
Itakuwa kakunyima nanii ...maana sio kwa kumuandama uko.
Wewe unaona mafundisho yake yana maadili au kwa kuwa tu wewe ni mfuasi wake unafuata tu kama nyumbu?
 
Mkuu kwani huyo Nabii anakupunguzia au anakuongezea nini hasa katika maisha yako binafsi? Akikamatwa na Serikali ndiyo Muamala wako wa Kibenki au wa katika Simu yako utaongezeka? Tatizo ni kwamba hao Waumini unaohangaika hapa kuwapigania wengi wao ni ' Wapuuzi ' mno Kiimani na sidhani hata kama watakuelewa. Suala hapa siyo tu huyo Nabii bali ni kuwatahadharisha Watu juu ya hawa Viongozi wengi wa Makanisa haya ya Kiroho jinsi walivyo wa ' hovyo hovyo ' ili waachane nao mara moja. Tena kwa taarifa yako tu sasa bora hata ya huyo Nabii ambaye Yeye bila aibu kaamua ' Kujilipua ' hadharani hadi leo hii Wewe unamuona ' kapotoka ' Kimaadili ila Mimi kuna Viongozi wawili wa Kidini tena ni wakubwa hapa nchini ' matukio ' wanayoyafanya nadhani hata ya huyo Nabii yana afadhali na najua wale ' Watafiti ' wenzangu hapa tayari wameshawajua hao Viongozi wa Kiroho ninaowalenga hapa. Kuna mmoja wapo anavuta Bangi / Bange nadhani hata Hayati Bob Marley akifufuka leo na kumuoana anaweza kumpa Kombe la Ushindi huku mwingine akiwa ni hodari sana kwa ' Kuwabandua / Kuwabaioloji ' Wake za Watu tena katika Kanisa lake ambapo kuna Chumba chake ' maalum ' na mwaka jana alikoswakoswa ' Kiduchu ' tu katika ' mtego ' ili aliwe ' ndogo ' ila Malaika wake walimwokoa.

Kwa leo naomba niishie hapa tafadhali.
Mfundisho yake wewe unayonaje? Yana chembe ya ukweli?
 
Ni aibu sana kwa serikali kudeal na wanasiasa peke yao huku wakiacha jamii ikipotoshwa na hawa manabii wa uongo. Inauma sana.
 
Nasema hivi, kati ya manabii wote wa kikristo huyu ndiye nabii asiye mnafiki peke yake manabii wengine wote waliobaki wa kikristo ni wanafiki tu.

Nampa sana hongera kwa kuuweka unafiki pembeni na aendelee hivyo hivyo aseee.

Safi Sana.
Mkuu unakumbuka wale maimamu waliokuwa wanawapiga mashine watoto wa madrasa?[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kama kuhamasisha unywaji pombe ni kosa, kwanini serikali inakata kodi kwenye vileo?
 
Back
Top Bottom