Nabii Flora Peter wa Mbezi Beach...

Nabii Flora Peter wa Mbezi Beach...

Ndugu zangu kuweni macho. Kama ni miujuza mbona mazingaombwe yalikuwepo tangu enzi na enzi? Tusivutwe na miujiza tutapotea. Someni biblia vizuri mtagundua kuwa mwanamke kusimama madhabauni ni chukizo kwa Mungu. Ibada za sanamu ni nyingi sana siku hizi. Hizo stika na sabuni anazowauzia ni sawa na sanamu. Ukiwa na imani kwa mungu wa kweli maombi yanatosha huhitaji vitu vya kuonekana ili uamini.
 
Aisee huyu mama sio mtu wa kawaida kabisa em mwangalie macho yake yalivyo mekundu na huo uso sijui kapaka kitu gani Yesu wangu turehemu na masheitwan watu.
 
picha yake imenitisha, najipongeza kutohudhuria makanisani japo naamini ktk imani ya kikristo

Mungu wangu..! Ndio huyu nabii mwenyewe?

Huyu sio nabii wa Mungu huyu ni nabii wa kuzimu, malkia wa kuzimu mwenye sura ya binadamu... Hili Nalisema wazi na kwa uhakika, angalia 👑 yake ni satanic crown angalia imenakshiwa na 🎀 ribbon ya pink, tafuta asili ya rangi ya pink, gauni lake ni rangi nyeusi ya kumetameta ina maana kubwa sana kuzimu, nyusi kazitinda na kuziongezea urefu ni Mulemule....... Nitakuja na picha





Aiseee nimeshangazwa sana na muonekano wa huyu nabii



Lkn kama nikwel abarikiwe kwakwel
 
Paulo ni nani?

..........humjui !? .... any way ni tapeli fulani hivi ana jina lingine anaitwa Sauli. Ana Kitabu kinaitwa 'Agano Jipya' !
Sijui aliagana na nani ! Kyenju
 
Last edited by a moderator:
Nabii Frola Peter anatenda asee!...kuna siku nakumbuka tuko kanisani kwake aliombea maji ya uhai yakawa asali tamuu...

Katika siku za mwisho yatatokea makristo ya uongo. Siku hizi kuna wimbi kubwa la manabii wa uongo wanaofanya miujiza ambayo kama watu wasipokuwa makini wanaweza kuiacha imani ya kweli waliyonayo.
 
..........humjui !? .... any way ni tapeli fulani hivi ana jina lingine anaitwa Sauli. Ana Kitabu kinaitwa 'Agano Jipya' !
Sijui aliagana na nani ! Kyenju
Kumbe alikuwa ni tapeli?
 
Last edited by a moderator:
Acha kumuhukumu mtu, kila mtu anayake kabeba moyoni, nivema mtu kujisafisha nafsi yako kuliko kumwona mwingine mdhambi.

Hajahukumu mtu bali amesema kweli ili watu wapone. Inashangaza kuona watu wengi wanapoambiwa ukweli wakilalamika na kuona wanahukumiwa. Ndugu, usiposimama katika neno la kweli hakika utakwenda motoni. Hiyo siyi hukumu bali ni onyo na tahadharu kwa faida yako.
 
Ndio maana watu wengi wanakata tamaa na dini. Sasa wewe na uchafu wote unaoandika hapa forum eti unasali kwa nabii halafu tena amekusaidia? Basi atakuwa ni Lusifa mwenyewe na wewe ni ibilisi

Biblia inasema mtawajua kwa matunda yao. Roho iliyo kwa nabii wakr ndiye aliye ndani yake. Ni roho za.siku za mwisho za kupenda fedha kuliko kumpenda Mungu wa kweli.
 
Ziada.
Usimdiscuss mtumishi wa Mungu. Hata kama anakosea kumbuka Miriam na nduguze walifanywa nini kwa kumsema mtumishi wa Mungu. Mungu ana makusudi kuacha magugu na mbegu njema kuota pamoja.

Huyo siyo mtumishi wa Mungu bali ni wakala wa Shetani. Roho ya uwezo wa mfalme wa anga ndiyo.inayotenda kazi ndani yake.
 
Watu mbalimbali wanapokea kila leo miujiza
1. Stika zipo na watu wanapokea miujiza
2. Mafuta yapo na watu wanapokea miujiza
3. Sabuni anatoa na watu wanapokea miujiza
4. Damu ya YESU anatoa kila siku saa10 kasoro Jumamosi na Jumapili
5. Anatabiri njoo ujionee mwenyewe na anavyotabiri na unajua wa kweli au uongo
0657442699 au 0753335673

Huu ni uthibitisho siyo nabii wa Mungu.
 
Mungu nisaidie. Hivi hao waumini kwake wanafanya kazi yoyote? Juma3 mpaka jumapili wanasali asub mp jioni. wanaishi kwa mana au miujiza.?
 
Kumbe alikuwa ni tapeli?

................tehee tehee..tihii hii ! Aliwatokea Wagalatia na Wakorintho, akawashuhudia kuwa Yesu kamtokea na kamwagiza aje awahubirie kuwa ni mungu !
Wakati Yesu mwenyewe anasema: Baba ni Mkuu kuliko mimi (Yohana: 14:28) ..... au kwa Kiarabu ni 'Allahu Akbar'
Au soma Zaburi ya Daudi: (Zaburi: 83:18)

Na Yesu akawafundisha wafuasi wake kusali, na akawaambia mkitaka kusali basi salini hivi:

'Baba yetu uliye Mbinguni,

'Jina lako litukuzwe,

'Ufalme wako uje, na

'Mapenzi yako yatimizwe,

'Utupe leo riziki yetu,

'Utusamehe madhambi yetu, na

'Utuepushe na Shetani yule muovu,

'Kwakuwa Ufalme ni wako hata milele,

Ameeen......Ameeen !
 
Jamani mumgu hayupo.

Hayo munayoyaona anayafanya kutokana na kufungua jicho la tatu.

Ndio jicho latatu, na kilamtu anaweza kulifungua na akatenda miujiza.

Hawa walioweza kulifungua ndio hawa tuliowaita manabii na mpaka leo ndio hao akina Gwajima sijui Th joshua na huyo mama hapo.

Hujiita watu wamungu ili kuwaficha wengine wasistukie kilicho nyuma ya pazia, sababu wanajua watuwengi wakistukia watakua hawana wa mkutapeli.

Mtaani kwetu kunamzee alishawahi kuibadili Gongo (pombe) kua siki (ndim) pale mahakama ya mwanzo Temeke (Chang'ombe) mpele ya wazee wa baraza. Napata picha tukio hili lingefanywa na hao manabii lingeitwa ni utukufu kutoka kwa mumgu.

Jamani tuamke, sikuhizi neno mungu (lisilo na maana moja) limekua linatumika kutapelia watu.
 
Back
Top Bottom