Naacha rasmi kusaidia wenye uhitaji

Naacha rasmi kusaidia wenye uhitaji

Ubinadamu kazi wakuu,

Vitendo ninavyopata toka kwa ninaowasaidia kutoka ni vya kukatisha tamaa kwa kweli.

Huyu ni mtu wa nne sasa; anahitaji ajira unampa shavu anakua na life lake lakini akishatoa matongotongo tu anaanza visa vyake.Unaonekana mjinga na mshamba tu.

Yeye ndio anajua kila kitu anajifanya kama hakujui vile kumbe wewe ndio umempa hiyo nafasi.Sasa hata nikiona nafasi mahali bora nikae kimya tu maana napata dharau toka wema wangu.

Wakuu binadamu watu hatari mno,nimekuja jua maana kama ingekua ni huyu tu nisingekua na wazo tofauti ila huyu ni wa nne kwahiyo hii ndio tabia halisi ta binadamu kwamba akishatoka anasahau kua kuna jamaa walihenyeka kumpa support mpaka kufikia hapo alipo.

Watu wabaya

hilo sawa kabisa japo sio wote, nakumbuka kuna mtu hivyohivyo japo uwezo nimemzidi sana kuna siku after 1 year nikampigia as a friend hakupokea hata simu, siku nyingine nikakutana naye akawa na haraka ila psycholocally nikamsoma nkamwambia napenda tu tukapate kinywaji wengine ndo hivyo nshawasahau kabisa.

all in all lengo nikupata company tu ya kupiga story weekend but ndo hivo na wapo wanaoshukuru ila huwa nawaambia hicho kidogo wasaidie wasiojiweza mtaani kwako au peleka kanisani!!!!
 
Kuna mdau kakuuliza swali zuri sana, wewe ulitaka wakulipe nini??!! Usidhani hawataki kukulipa, lakini wanakulipaje ndiyo ishu. Inawezekana washafanya/wanafanya kitu ambacho wao wanatafsiri ni kukulipa wewe hung'amui kwa kuwa una tafsiri yako. Kama vipi wakati wa kuwapigia hayo unayoyaita mapande muwekane sawa kabisa nini unategemea kutoka kwao; kama kweli unahitaji kulipwa!
 
Hao unaowasaidia ni jinsia gani? Na pia kama unasaidia wewe saidia tu, kurudisha fadhila ni moyo na roho ya mtu mwenyewe.
 
Kuna jamaa mwingine humu alikuja na stori kama hii hii na mbwembwe kibao lakini baada ya kuusikiliza upande wa pili ikaonekana kumbe jamaa ndiye kimeo.

Mkuu,Too much expectations huishia kwenye disappointments tu siku zote.
 
hua napiga mapande ya ajira mkuu; wakishapata sasa huwaoni mkuu na wanageuka wajuaji. inauma sana kuona mtu umempa pande then anakugeuka baada ya kua mambo safi. kama binadamu you expect walau hata kuona ukikumbukwa kidogo inaleta faraja ila hakuna. wabongo si watu.

Kama unaweza kuwasaidia kwa njia hiyo ni vizuri zaidi ila sio kuwa nao kila siku.
 
Post yako ya mwanzo nilielewa vizuri kwamba baada yakumsaidia amekutenga labda hata salam hakuna
Ila hii ya pili ndio nimepata picha kwamba Kumbe unataka kauli iwe Tenda wema usubiri chochote.

Hii inanipa picha kwa wewe ndio mtata,na hao watu karibia wanne unaosema unawasaidia na hakuna anaekukumba sio kweli.

Kwa maelezo yako tu ni kwamba jamaa wewe mtata saaana,yaani unampa mtu mchongo kisha yeye ndio aendeshe maisha yako?

Watu wa namna hii mpo wengi sana,na unapompa mtu mchongo sio kwamba ndio umeunda ajira mpya,au msaada wa kukusaidia majukum yako,mtu kukusaidia ni hiari yake.

Na ndio maana hao woote wanne umesema umewasaidia na kila mmoja hakukumbuki,mi nawaunga mkono kabisaaaa.
Huwezi kuchuniwa na wote wanne lazima utakuwa na mapungufu makubwa sana na kitengo chako cha MIZINGA kipo Acvtive sana,ila wewe ni MTATA

shutuma zako hazina ukweli wowote mkuu; sasa inakuwaje tena niombe fedha kwa mtu niliyemsaidia kupata nafasi ya kutengeneza kipato. kama inatokoea nakutana na hizo nafasi badala ya kuomba ningekamata fursa na kupiga mwenyewe. roho mbaya tu na kujisahau. i wish ningeweka wazi kila detail ila ni ngumu.

binadamu tuna hulka ya kujisahau. hilo tu. sihitaji fedha wala lolote ila nachogusia hapa ni behaviour za wahusika baada ya kufanikiwa.

mfano kabla hajapata nafasi mawasiliano hua mazuri na approach pia ila akishatoka all of a sudden hutamsikia tena.
 
hua napiga mapande ya ajira mkuu; wakishapata sasa huwaoni mkuu na wanageuka wajuaji. inauma sana kuona mtu umempa pande then anakugeuka baada ya kua mambo safi. kama binadamu you expect walau hata kuona ukikumbukwa kidogo inaleta faraja ila hakuna. wabongo si watu.

Kama unaweza kuwasaidia kwa njia hiyo ni vizuri zaidi ila sio kuwa nao kila siku.
 
Ubinadamu kazi wakuu,

Vitendo ninavyopata toka kwa ninaowasaidia kutoka ni vya kukatisha tamaa kwa kweli.

Huyu ni mtu wa nne sasa; anahitaji ajira unampa shavu anakua na life lake lakini akishatoa matongotongo tu anaanza visa vyake.Unaonekana mjinga na mshamba tu.

Yeye ndio anajua kila kitu anajifanya kama hakujui vile kumbe wewe ndio umempa hiyo nafasi.Sasa hata nikiona nafasi mahali bora nikae kimya tu maana napata dharau toka wema wangu.

Wakuu binadamu watu hatari mno,nimekuja jua maana kama ingekua ni huyu tu nisingekua na wazo tofauti ila huyu ni wa nne kwahiyo hii ndio tabia halisi ta binadamu kwamba akishatoka anasahau kua kuna jamaa walihenyeka kumpa support mpaka kufikia hapo alipo.

Watu wabaya

Tulivyomaliza chuo nilibahatika kupata kazi mapema sasa pale ofisini wakawa wanahitaji mtu mie nikaona ngoja nimvute mshkaji lakini huwezi amini huyo mshkaji wangu ndio ilikuwa sababu ya mimi kufukuzwa kazi sababu ya majungu yake! kuna watu na viatu!
 
Kuna mmoja nilimtoa humu jf,tulibadilishana contacts nika muekekeza sehemu ya kazi akakutana na boss wake.sijawai kumuona na wala hajawai kuniona.alivyopata hiyo kazi hata asante tu ilimshinda huwa napata habari zake tu kutoka kwa boss wake...!!
 
Kama wewe ni muamini wa hizi dini zetu...ni wapi umeahidiwa kuwa ukimsaidia mtu basi utalipwa na mtu/watu?
Mimi nadhani utarajie kulipwa na MUNGU kupitia watu ambao si lazima wawe hao uliowasaidia.

Maana hao uliowasaidia wakikulipa sasa wewe utakuwa umewafanyia wema au imewauzia wema?

Wema haulipwi na biandamu aliyefanyiwa bana

Umenena vyema...
 
Mkuu shukurani inakuja wakati ukiwa hutegemei. Ukishaidai hiyo sio shukurani tena bali malipo kwa ulichofanya.
 
shutuma zako hazina ukweli wowote mkuu; sasa inakuwaje tena niombe fedha kwa mtu niliyemsaidia kupata nafasi ya kutengeneza kipato. kama inatokoea nakutana na hizo nafasi badala ya kuomba ningekamata fursa na kupiga mwenyewe. roho mbaya tu na kujisahau. i wish ningeweka wazi kila detail ila ni ngumu.

binadamu tuna hulka ya kujisahau. hilo tu. sihitaji fedha wala lolote ila nachogusia hapa ni behaviour za wahusika baada ya kufanikiwa.

mfano kabla hajapata nafasi mawasiliano hua mazuri na approach pia ila akishatoka all of a sudden hutamsikia tena.

Zekidon,nakushauri tuliza mori kwanza.
Hao hata kama hawatakukumbuka basi Kizazi chake kitakukumbuka.
Maisha ni dynamic kama Lowasa,kuna siku yanaweza kuwageukia then wakaona hakuna pa kwenda zaidi ya kuja kwako.
We vuta subira tu,ila endelea tu kuwaombe maisha mema na kazi njema.
Mungu humbariki sana anaewaombea mema wenzio hata kama kuna tofauti za kimaisha.
 
Mi huwa naona misaada bora nipeleke kanisani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom