Mzungu angeongoza Tanzania!

Mzungu angeongoza Tanzania!

That's one but two, hakuna anayemkejeli Makonda bali inayokejeliwa ni approach yake! Na si kwamba hafahamu kwamba approach yake ni mbovu, anajua na kama alikuwa hajui sina shaka watu walio chini yake walimwambia this's wrong approach! Siamini mtu kama Simon Sirro anaamini kutoa tip hadharani kwamba XYZ ni drug dealers kabla hujaenda kumpekua na kupata ushahidi wa kuanzia hiyo ndiyo best approach!!!
Nilikuuliza approach ipi ni nzuri na je tangu mapambano yaanze imetoa matunda gani? au hizo approach nzuri ndo mmezigundua sasa na hamjawahi kuzitumia ila mnataka aanze nazo Makonda?
 
Lakini kama Makonda aliingia kwenye game na ile tabia yake ya kuanza kuonesha watu hawajui kazi ; inawezekana kabisa kabisa akina Sirro walikata shauri la kumuitikilia kila analosema...!! Huyo Sirro mwenyewe keshawahi kutuhumiwa na Makonda kwamba inawezekana amechukua 50 million za shisha... sasa ya nini mtu ati mdomo wake halafu aambiwe anajengwa ghorofa na wauza dawa za kulevya!!!!
Makonda ameeleza ukweli kuwa Shisha ipo na akina Sirro wapo. Au sio kweli?
 
Mkuu wa mkoa anahusika pia kwani yeye ndiye rais katika mkoa anao tawala. Tanzania hatuhitaji demokrasi kwa sasa, tunahitaji Magufuli aendeshe nchi hii kimabavu kama afanyavyo sasa. Mbona wananchi wa nchi nyingine za Afrika zinamlilia Magufuli? Watu wamechoka na tawala za kijinga na magumashi. Angalieni Kikwete, alijifanya kaleta demokrasia....mtoto wake mwenyewe anauza unga, akapewa majina ya wauza unga awachukulie hatua, kaacha kwani alijuwa angewafichua basi na yeye angetajwa. Hii ni haki kweli kwa akili yako? It's too early for demokrasi hapa nchini. Hapa kazi tu.
Too early for democracy in africa. Bado tunao ujinga mwingi sana maishani mwetu kuweza kuishi kwa matakwa ya demokrasia.
 
Hata kwenye huo uzi hukusema zinatakiwa gram ngapi ili iwe significant evidence. acha kukwepa swali kinapenape.
Inawezekana hutaki kuelewa!! Hoja pale ni kwamba unapiga kelele dunia mzima ukiaminisha watu kwamba hawa ni drug dealers na kwamba kabla hamjaita mtu mna ushahidi wa kutosha kwamba wanahusika na dawa za kulevya!!!

Sasa kama kelele zote hizo unaishia kupeleka mtu mahakamani kwa msokoto mmoja wa bhangi basi unaonesha wazi kwamba hujui unachofanya!! Hiyo misokoto ya bhangi imejaa kila kona kwahiyo ni kiroja kuutangazia umma kwamba ni vita dhidi ya dawa za kulevya halafu unaishia kuwa na ushahidi wa 1.83 g of marijuana! Yule hata akipelekwa mahakamani, haiwezi kuwa kesi kuhusu uuzaji wa dawa za kulevya bali dhidi ya matumizi ya bhangi na ndio maana alipelekwa kwa Mkemia Mkuu pawe na evidence kwamba anatumia bhangi!!!

Sasa kama ndo vita mnayoisifia ndo hiyo au mnayotaka watu waunge mkono ndo hiyo; basi mna kazii manake sie wengine tunaona drama zaidi!!!

Now look, wale ambao wana dalili kwamba kweli wanaweza kuwa drug dealers, unaanza kuwapa alert! Hivi unapotangaza hadharani kwamba fulani anauza dawa za kulevya ni nini maana yake kama sio unamwambia afiche ushahidi?!!! Nimetoa mfano hapo wa mmiliki wa Slipway! Kama kweli anatumia bandari yake kupakulisha dawa za kulevya, kulikuwa na sababu gani za kupiga kelele kwamba yule nae anatumia bandari yake kupakua shehena za dawa za kulevya halafu unamtaka aje kuripoti?

Akija kuripoti ndo unaondoka nae kwenda kufanya upekuzi... is he really serious?! Hivi hata kama kulikuwa na mzigo unakuja si alishaupiga stop?! Sasa Kamanda Sirro na wenzake wakienda kumpekua na kukuta msokoto mmoja wa bhangi ndo tushangilie kwamba ni vita dhidi ya dawa za kulevya wakati tunajua kabisa, kama asingefanya mambo kwa kutaka atteention basi walikuwa na uwezo hata wa kukamata kilo kadhaa za drugs!!!
 
Leo hii Mzungu, Mjapani, au hata Mchina na Mkorea ukimpa nafasi ya kuongoza Tanzania hataruhusu demokrasia!
Jambo la kwanza kabisa atakalo lifanya ni kusitisha kila kitu na kuongoza nchi kwa decree kwa miaka kama 50 au zaidi, ndiyo aje kuruhusu, kuna sababu kwa nini apartheid AK Wazungu walikataa Waafrika wasipige kura kuwachagulia Viongozi!

USA ilianzishwa miaka ya 1700 lkn Wanawake walianza kupiga kura mwaka 1920, Native Americans waliruhusiwa kwenye mwaka 1924 wakati Wamarekani wenye asili ya Afrika waliruhusiwa kuanza kupiga kura mwaka 1965, izingatiwe kwamba USA ili uweze kupiga kura ilikuwa ni lazima uonyeshe uwezo wakujua kusoma na kuandika lugha ya Kiingereza na reasonig jambo ambalo makundi hayo niliyoyataja hapo juu yalishindwa kuthibitisha kutokana na sababu mbali mbali! Kuna sababu kubwa sana kwa nini ilikuwa hivyo, nayo ni kwamba demokrasia inahitaji binadamu kufikia ngazi fulani ya uelewa kuweza kuimudu!

Angalia leo hii Afrika yetu ni chaos tu, misunderstanding ya demokrasia inazidi kulibomoa na kulirudisha nyuma bara la Afrika, watu wanatetea Wauza unga tena Bungeni na kujaribu kuwaadhibu na wale wanaojitokeza kupambana nao ili kuokoa jamii, wakati huo huo hawatoi njia mbadala na bora zaidi ya iliyotajwa lkn wanaikataa iliyopo ingawaje watu wetu wanaendelea kuathirika na Madawa huu ni mmoja tu wa mifano mingi ambayo inaonyesha kwamba Afrika tumeanza na demokrasia mapema sana, ilipaswa tuwe na One ruler for all!

Nchini AK Wabunge wa Chama cha Economic Freedom Fighters (EFF) wakichapana Bungeni!

eff-vs-zuma.jpg
fikra na mawazo mgando

yani mtanzania mwenzangu umekaa umetafakari ukaone uje na hiki kitu and then you later call yourself a great thinker. more like an enslaved thinker!

geez
 
Makonda ameeleza ukweli kuwa Shisha ipo na akina Sirro wapo. Au sio kweli?
Hoja si kuwepo shisha... don't exaggerate! Issue ni Kamanda Sirro kushukiwa ikiwa alizidaka million za wauza shisha!

Labda umesahau, jikumbushe:

Sirro.png


Kuonesha tuhuma za Makonda dhidi ya Kamanda Sirro hazikuwa tuhuma za mchezo mchezo; kumbe jeshi la polisi likatia nia ya kumfanyia uchunguzi Sirro!!

Swali: Matokeo ya uchunguzi huu yameshatoka au uchunguzi bado haujafanyika?! Kama matokeo yameshatoka na Kamanda Sirro kusafishwa, unaweza kuweka hapa ili tuhuma dhidi ya Sirro zifutike rasmi?!

Na ikiwa uchunguzi haujafanyika wakati jeshi la polisi liliona hili ni suala linalohitaji kufanyiwa uchunguzi; inakuwaje tena kamanda yule yule aliyetiliwa shaka huenda amekula rushwa za wauza shisha leo hii anafanya kazi na yule yule aliyemtuhumu dhidi ya wale wale wanaohusika na mihadarati?! Upi usahihi katika hili: Ni kwamba Makonda aliamua tu kumchafua Kamanda Sirro na ndio maana bado anafanya nae kazi kwa kuwa anafahamu kwamba alimsingizia au Makonda ameamua kufanya kazi na mtu mwenye tuhuma za kula rushwa za wauza mihadarati?

Ikiwa jibu hapo juu ni kwamba Makonda anafahamu Kamanda Sirro hakula rushwa kama alivyopata kumtuhumu hadharani; kuna tofauti gani basi na anachofanya sasa kutuhumu watu hadharani bila kuwa na ushahidi?!

Na kama jibu ni kwamba bado Makonda anaamini Siiro huenda alishachukua chake kutoka kwa wauza mihadarati; kwanini leo hii tusiamini hizi zote ni drama kwa sababu yule yule aliyetuhumiwa kupiga pesa za wauza mihadarati ndo huyo huyo leo hii tunaambiwa anatekeleza maagizo ya Makonda dhidi ya wauza mihadarati wengine ambao ni matajiri maradufu ukilinganisha na wale wa awali?!
 
Leo hii Mzungu, Mjapani, au hata Mchina na Mkorea ukimpa nafasi ya kuongoza Tanzania hataruhusu demokrasia!

Si nchi zote za wazungu wana demokrasia wengine wana utawala wa Kimila. China hakuna demokrasia kama ya Nchi za Magharibi.

USA ilianzishwa miaka ya 1700 lkn Wanawake walianza kupiga kura mwaka 1920, Native Americans waliruhusiwa kwenye mwaka 1924 wakati Wamarekani wenye asili ya Afrika waliruhusiwa kuanza kupiga kura mwaka 1965,

Unafananishaje wanawake na waafrika wote?

Angalia leo hii Afrika yetu ni chaos tu, misunderstanding ya demokrasia inazidi kulibomoa na kulirudisha nyuma bara la Afrika,

Utawala wa kimla ulishindwa kuleta maendeleo ndio maana tumeamia kwenye demokrasia ya Magharibi. Misunderstanding hata ulaya na USA zipo.
 
USA ili uweze kupiga kura ilikuwa ni lazima uonyeshe uwezo wakujua kusoma na kuandika lugha ya Kiingereza na reasonig jambo ambalo makundi hayo niliyoyataja hapo juu yalishindwa kuthibitisha kutokana na sababu mbali mbali!

Nakubaliana na 'reasoning' factor na nafikiri ndio maana wana electoral college.
 
Sihamii kokote nimezaliwa, kukulia na nitafia hapa wewe ndiyo uhame!
basi kaa uelewe nchi hii utawala wa kiimla hakuna. too late. ila wewe unaruhusiwa kuwa na mawazo ya kiimla na unaweza kujaribu utawala wa dizaini hiyo nyumbani kwako.
 
Yaani kama Tanzania ikipita hii, " ili upige kura lazima uthibitishe unajua kusoma na kuandika na pia uwe na reasoning capacity ya kiwango fulani" hapo sidhani kama chama chetu kile cha CCM kitapata hata 35%..


Hata chadema pia haitapita hata 5% kama utaratibu huu ukija na kitaibuka Chama kipya ambacho kitafiti na hali itakayo kuwepo, lkn kumbuka pia ukipitisha hilo kutakuwa na voter aparthy kubwa sana au watu ambao hawatapiga kura wengi sana, na hivyo kuwa na apartheid Tanzania, hiyo ndiyo changamoto yake, hivyo suluhisho ni kusimamisha zoezi zima mpaka sehemu kubwa ya jamii yetu iweze kukidhi hivyo vigezo!!
 
Hata chadema pia haitapita hata 5% kama utaratibu huu ukija na kitaibuka Chama kipya ambacho kitafiti na hali itakayo kuwepo, lkn kumbuka pia ukipitisha hilo kutakuwa na voter aparthy kubwa sana au watu ambao hawatapiga kura wengi sana, na hivyo kuwa na apartheid Tanzania, hiyo ndiyo changamoto yake, hivyo suluhisho ni kusimamisha zoezi zima mpaka sehemu kubwa ya jamii yetu iweze kukidhi hivyo vigezo!!

Jamii inakidhi vipi vigezo hivyo kama kuna kundi fulani linanufaika na vigezo vilivyopo.. Huoni kama kundi nufaika na hivyo vigezo litaendelea kudumaza watu kiakili ili liendelee kunufaika?
 
Barbarosa hiki kichaa cha kuutamani udicteta unatokana na 2015, wananchi walivyowanyima kura mpaka mkalazimika kutumia vyombo vya dola kubaki madarakani, na hivyo kuingia na mfumo wa kidicteta mkidhani mtawalazimisha watu kukipenda CCM . You are very wrong.

Nchi zote hizo mnazoenda kutembeza bakuli na zenye kupigiwa mfano zina mifumo ya kidemocrasi na mihimili iliyojitegemea isiyoingiliwa na mtu aliye hai bali katiba sheria za nchi.

Udicteta poote duniani hakuwahi kurithisha maendeleo endelevu ya kupigia mfano.


Siyo kweli! Nchi zote Duniani ambazo zimeendelea leo hii zilianza na Udikteta (benovalent dictatorship) wa namna moja au nyingine na ndiyo maana nikatoa mfano wa USA kwamba mwanzoni hawakuruhusu makundi fulani ya watu kupiga kura, hata Ulaya mwanzoni ilikuwa ni hivyo hivyo Monarchy walikuwa na absolute powers au absolute rulers na ndiyo waliojenga Ulaya, Korea Kusini ilijengwa na Udikteta wa Park, Singapore mpaka leo hii kuna udikteta, Taiwani yenyewe imeanza kufunguka juzi juzi tu na kuruhusu demokrasia baada ya kufikia kiwango fulani cha maendeleo hasa ya kijamii na ndiyo maana Uchina wamekataa demokrasia ya Ulaya na USA wamesema itakuja baadaye sasa angalia tofauti kati ya Uchina India, nani amepiga hatua kubwa ya kimaendeleo? India ambayo inaitwa the largest democracy in World mpaka aleo hii kuna masikini zaidi ya Tanzania, matatizo yote ya kijamii ambayo Uchina alishayondoa yapo India kama utapiamlo, umaskini uliokithiri yaani ufukara, usalama mdogo wa raia n.k. hivyo hata wao India pia wamefanya makosa kama ya Afrika, kwamba wameanza na demokrasia mapema sana!
 
Siyo kweli! Nchi zote Duniani ambazo zimeendelea leo hii zilianza na Udikteta (benovalent dictatorship) wa namna moja au nyingine na ndiyo maana nikatoa mfano wa USA kwamba mwanzoni hawakuruhusu makundi fulani ya watu kupiga kura, hata Ulaya mwanzoni ilikuwa ni hivyo hivyo Monarchy walikuwa na absolute powers au absolute rulers na ndiyo waliojenga Ulaya, Korea Kusini ilijengwa na Udikteta wa Park, Singapore mpaka leo hii kuna udikteta, Taiwani yenyewe imeanza kufunguka juzi juzi tu na kuruhusu demokrasia baada ya kufikia kiwango fulani cha maendeleo hasa ya kijamii na ndiyo maana Uchina wamekataa demokrasia ya Ulaya na USA wamesema itakuja baadaye sasa angalia tofauti kati ya Uchina India, nani amepiga hatua kubwa ya kimaendeleo? India ambayo inaitwa the largest democracy in World mpaka aleo hii kuna masikini zaidi ya Tanzania, mamtatizo yote ya kijamaa ambayo Uchina alishayondo yapo India kama utapiamlo, umaskini uliokithiri yaani ufukara, usalama mdogo wa raia n.k. hivyo hata wao India pia wamefanya makosa kama ya Afrika, kwamba wameanza na demomkrasia mapema sana!
Barbarosa unaushabikia u dictator kwa vile tu una maslahi na walio madarakani otherwise ni kitu hatari na inaambatana na yafuatayo:_
1. Kufunga watu hovyo hasa wenye mawazo tofauti na watawala
2. Kupotezana (mauaji) kwa wasioamini falsafa yao
3. Kuongoza kwa kufuata amri na matakwa ya boss hata kama ni nonsense
4. Mihimili ile miwili kuwekwa ktk mfuko mpana wa executive

Hili jambo huwezi kujua ni nani ataiongoza nchi kwa sababu udicteta hauna kanuni
 
Barbarosa unaushabikia u dictator kwa vile tu una maslahi na walio madarakani otherwise ni kitu hatari na inaambatana na yafuatayo:_
1. Kufunga watu hovyo hasa wenye mawazo tofauti na watawala
2. Kupotezana (mauaji) kwa wasioamini falsafa yao
3. Kuongoza kwa kufuata amri na matakwa ya boss hata kama ni nonsense
4. Mihimili ile miwili kuwekwa ktk mfuko mpana wa executive

Hili jambo huwezi kujua ni nani ataiongoza nchi kwa sababu udicteta hauna kanuni


Hakuna mahali niliposhabikia udikteta kama ulivyosema bali nimeongelea hali halisi ambapo Binadamu ni lazima apitie kufika mahali fulani, hakuna jamii ambayo leo hii imejenga Civilazation ya maana ambayo haijapitia hiyo hatua ya udikteta, hakuna kama ipo, nitajie!"
 
Kwanini mnaamini ni ccm tu ndiyo wanatumia ujinga wa wananchi?

Kwa sababu ndivyo ilivyo. Ni impossible kwenye any knowledgeable society kuendelea kutawala kwa miaka zaidi ya 50 bila kuonyesha ulichofanya kwa manufaa ya society hiyo na resources ulizonazo.
 
By the way, ikiwa ameshindwa kumsilikiza Waziri wa serikali anayeitumikia, ndo atakuja kusikiliza ya Wapinzani?! Nini alichoambulia Nape baada ya kusema this's wrong zaidi ya kashifa toka kwa wafuasi uchwara kwamba Nape anatetea wauza dawa za kulevya?! Ndo maana hata mawaziri wanaohusika na hili jambo wameamua kupiga kimya!!!!

Hivi ni lini hawakuwa kimya? una maana makonda kawakuta wakiwashughulikia wauza madawa ya kulevya yeye akawapiga kumbo na sasa ndo "wakaamua kukaa kimya"?
 
Mkuu wa mkoa anahusika pia kwani yeye ndiye rais katika mkoa anao tawala. Tanzania hatuhitaji demokrasi kwa sasa, tunahitaji Magufuli aendeshe nchi hii kimabavu kama afanyavyo sasa. Mbona wananchi wa nchi nyingine za Afrika zinamlilia Magufuli? Watu wamechoka na tawala za kijinga na magumashi. Angalieni Kikwete, alijifanya kaleta demokrasia....mtoto wake mwenyewe anauza unga, akapewa majina ya wauza unga awachukulie hatua, kaacha kwani alijuwa angewafichua basi na yeye angetajwa. Hii ni haki kweli kwa akili yako? It's too early for demokrasi hapa nchini. Hapa kazi tu.

Wakati Hitler anaingia madarakani watu walishangilia sana. Alipozoea madaraka walijuta. Kujuta ni process haiji kama mwanga unapowasha bulb kwenye chumba chenye giza. Tusubiri.
 
Hivi ni lini hawakuwa kimya? una maana makonda kawakuta wakiwashughulikia wauza madawa ya kulevya yeye akawapiga kumbo na sasa ndo "wakaamua kukaa kimya"?
Kuna maswali kadhaa pale nimekuuliza lakini hujajibu hata moja!

Utamu wa mjadala ni kwamba, ukiulizwa swali unatakiwa kwanza ujibu nddipo nawe uulize swali au maswali!
 
Back
Top Bottom