Upinzani unapokuwa ni wa kutetea wauza madawa ya kulevya ni bora kuminywa tu.Na ukitoa nchi zenye utajiri wa asili wa kupindukia usiolingana na idadi ya watu wake, utagundua ni nchi moja tu ndiyo iliweza kufanikiwa pamoja na kuminya demokrasia... na nchi hiyo ni Cuba!
Kinyume chake, Afrika ingawaje tuna utajiri mkubwa wa asili lakini bado tumebaki maskini kwa sababu, ukosefu wa demokrasia na uhuru wa watu kuji-express, kunafanya walio madarakani maovu yao kutoonekana!
Tanzania ni linchi likubwa sana lililo na changamoto lukuki kuweza kuifikia kila mahali! Huko kwenye halmashauri hadi kesho watu wanapiga pesa! JPM na chuki zake zote dhidi ya ufisadi, asiporuhusu demokrasia ataweza kuzifikia taasisi kubwa kubwa tu zilizo Dar es salaam manake huko kwingine kunahitaji msaada wa watu wasio na hofu ya kueleza what's going on!
Demokrasia ni nzuri kama kuna wapinzani wa kweli na principled. Sio hawa wanaounganishwa na CCM kwenye MADAWA YA KULEVYA.
Udikteta unaweza kufaa sana unapokuwa na wapinzani wa hovyo kama hawa ambao badala ya kuunga mkono juhudi zilizoanzishwa na kushauri njia mbadala itakayofaa ili kurekebisha makosa ya Makonda, wao wanaungana na miCCM kudai Makonda asulubiwe kwa kujaribu kupambana na wauza madawa ya kulevya.
Tuna MAPINZANI ya HOVYO sana Tanzania kwa hivi sasa. Mapinzani ambayo ukisema Lowasa ni FISADI eti leo ndo yamejua kuwa kabla hujatuhumu unatakiwa uwe na USHAHIDI. Mapinzani ambayo yapo tayari kuungana na MiCCM kupinga juhudi za kupambana na madawa ya kulevya yanhitaji kudhibitiwa kwa nguvu zote. Yakiachiwa Taifa litaangamia.