'Mzigo mzito mpe mnyamwezi'. Tumshauri mbinu gani za kulibeba hili zigo zito la nishati ya Taifa letu

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Nishati ndiyo roho ya taifa lo lote. Uchumi na ustawi wa nchi hutegemea upatikanaji wa kutosha na wa bei nafuu wa nishati. Uharibifu wa tabia nchi unatokana kwa kiasi kikubwa na ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa kwa sababu ya ukosefu wa nishati mbadala ya bei nafuu.

Suala la nishati na hasa umeme, na sasa hivi pia mafuta ya petroleum, limekuwa zigo kubwa kuanzia enzi za Lowasa na Kikwete. Mmasai huyo na mswahili huyo wa pwani ya Msoga walishindwa kabisa kulibeba zigo hilo la nishati. Alipopewa zigo hilo mnyamwezi wa Chato aliweza kulibeba vizuri zigo hilo na kuashiria kutimia kwa ndoto ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo 2025 (industrial country by 2025).

Awamu ya sita ilimbebesha zigo hili la nishati mswahili mmoja wa pwani ya Tanga. Kwa miaka takribani miwili mswahili huyu wa Tanga aligara gara na zigo hili hadi kutia huruma. Nchi ikakosa umeme kwa asilimia 60%, viwanda vikasimama kwa asilimia 40% na bidhaa kutoka viwandani vikapanda bei maradufu, ikawa haiwezekani kuanzisha viwanda vipya. Mbaya zaidi ikafikia hadi mafuta ya petroleum kuadimia kwa asilimia 90% na bei zake kupanda kwa asilimia 300%. Hali ikawa mbaya sana, uswahili ukawa mwingi ku justify hali hiyo.

Wahenga walishatuasa kwamba mzigo mzito mpe mnyamwezi abebe. Siku zote wahenga hawasei. Sasa zigo hili kabebeshwa mnyamwezi wa Bukombe. Tena kaongezewa nguvu ya unaibu waziri mkuu kulibeba hilo zigo ambalo kwa sasa limekuwa kubwa zaidi. Anahitaji mbinu za namna ya kulibeba. Jf kama jukwaa la Great Thinkers tumshauri mbinu anazoweza kuzitumia kulibeba zigo hili bila kuumia. Nitaanza na hizi chache:

1. Bwawa la NHPP lilishakamilika tayari kuanza kwa uzalishaji wa umeme. Sababu walizotoa hao waswahili ni kwamba kituo cha Chalinze cha kupitishia huo umeme hakijakamilika na wanatarajia kitakamilika mwezi July 2024. Ushauri: ziwashwe genereta mbili au tatu kati ya genereta 9 zilizopo pale bwawa la Nyerere. Hizi zitatupa MW takribani 600. Hizi ziingizwe kwenye grid ya taifa kupitia njia iliyo karibu na bwawa hilo. Waharakishe kujenga hiko kituo cha Chalinze, kikamilike ifikapo Desemba mwaka huu. Kijengwe mchana na usiku.

2. Umeme kutoka bwawa hilo usiuzwe zaidi ya TSh. 50 kwa kila unit moja ili hata mwananchi wa kawaida aweze kutumia umeme kupikia chakula badala ya kuni na mkaa.

Hao waswahili walishapanga kuongeza bei ya unit mradi huo wa JNHPP utakapokamilika. Walishasema kamwe hawatateremsha bei hiyo ya unit. Walishapanga kwamba kiasi kikubwa kama siyo chote cha umeme huo watauuza nje ya nchi hususani Zambia na Kenya kupata USD dollars, sisi tutaendelea kubangaiza huo umeme wa gesi kutoka Kinyerezi. Sababu waliyotoa eti ni kurudisha pesa iliyotumika kwenye ujenzi wa huo mradi.

Fedha zilizotumika kwenye ujenzi huo siyo zao bali ni kodi za wananchi zilizotumika ili wapate umeme wa bei nafuu na wa uhakika. Huwezi ukajenga hospitali au barabara kwa pesa itokanayo na kodi za wananchi, halafu ukataka kuwatoza tena wananchi hao wakitumia hiyo hospitali au hiyo barabara ili kurudisha pesa iliyotumika kuijenga. Vivyo hivyo kwa miundombinu zingine zinazojengwa na serikali au kwa vifaa na vitendea kazi vinavyonunuliwa na serikali hususani CT scan, MRI na kadhalika. Anayefanya hivyo ni mtu binafsi au kampuni binafsi aliyetumia hela yake binafsi kununua vifaa hivyo au kujenga miundombinu hizo. Pesa ya serikali inatoka kwenye kodi na tozo za wananchi. Hata kama pesa hiyo serikali ilizikopa, marejesho yake yanatoka kwenye kodi za wananchi.

3. Utaalamu (profession) unabidi uheshimiwe. Kwenye tasisi za kitaalamu, mtendaji mkuu anapaswa kuwa ni mtu aliyebobea kwenye hiyo taaluma. Huyo ndiye atakayeweza kuwasimamia, kuwaongoza na kuwaelekeza watendaji wenzake kwenye hiyo taasisi na kamwe haitakuwa rahisi kumdanganya.

Haingii kichwani mtendaji mkuu wa hospitali ya taifa kama Muhimbili akawa ni mwanahabari (journalist) halafu ukategemea ufanisi kwenye hiyo hospitali. Mhasibu akawa mtendaji mkuu wa TANROADS, Medical Doctor akawa mtendaji mkuu wa jeshi la wananchi au la polisi na kadhalika. Watu wapewe kuongoza maeneo ambayo wana utaalamu nayo. Wakurugenzi wa utawala wawe ambao wana taaluma ya utawala wa watu (public administration), wakurugenzi wa fedha lazima wawe wenye taaluma ya fedha na kadhalika.

Shirika la umeme, mtendaji mkuu wake anapaswa kuwa mbobezi kwenye taaluma ya umeme (senior electrical engineer). Vivyo hivyo kwa mameneja wa kanda, mikoa na wilaya. Vinginevyo shirika litaendelea kuchezewa na kudanganywa na wahandisi wake wa umeme.

4. Serikali inunue mafuta ya petroleum yenyewe moja kwa moja kutoka nchi zinzozalisha hayo mafuta. BoT na TPDC zitumike kutekeleza hili. Tutimize ndoto ya nchi yetu ya kuwa hub ya mafuta haya kwa nchi zinazotuzunguka na ambazo ni landlocked.

Tuachane kabisa kutumia hawa middle men ambao wametuchezea sana. Bei ya mafuta haya duniani yalifikia peak ya USD 135 kwa pipa mwezi March 2022. Baada ya hapo yalianza kushuka taratibu hadi kufikia USD 60 kwa pipa. Ni hivi juzi tu nchi za OPEC+ ikiwamo Russia zilipoamua kupunguza kidogo uzalishaji na kuwezesha kuyapandisha bei hadi kufikia USD 90 kwa pipa. Hii ndiyo trend ya bei ya mafuta haya duniani. Serikali kupitia wizara ya nishati na EWURA yao, imekuwa ikijifanya haioni trend hii na hivyo kuruhusu middle men hawa trend za bei zao ni ya kupaa tu kila mwezi kuanzia hiyo March 2022. Yaani leo sisi bei yetu kwa sasa ni maradufu ya bei ya mwezi March 2023 pipa lilipokuwa linauzwa dollar 135 wakati sasa linauzwa dollar 90 tu.

5. Great thinkers wa JF endeleeni kumpa mbinu za kulibeba hili zigo kubwa la nishati huyu mnyamwezi. Hapa mambo ya itikadiza kisiasa hazitakiwi. Na kama wewe siyo Great thinker hautakiwi.
 
Hizo ndizo bei za crude oil tangia Feb 2020 hadi Jun 2023. Bei za Tanzania ni za mwendo wa kupanda tu, hazina mwendo wa kushuka. Hazina reverse gear, zina gear za kwenda mbele tu tena kwa mwendo kasi na hakuna brake ya kusimama!
NWM Dotto Biteko aweke hiyo revers gear na brake zote.
 
Kuwashauri ccm inabidi ujitoe fahamu. Pamoja na hilo bwawa Bado ume utapanda Bei.
Niko hapa!
 
Nishati ndiyo roho ya taifa lo lote. Uchumi na ustawi wa nchi hutegemea upatikanaji wa kutosha na wa bei nafuu wa nishati. Uharibifu wa tabia nchi unatokana kwa kiasi kikubwa na ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa kwa sababu ya ukosefu wa nishati mbadala ya bei nafuu.

Suala la nishati na hasa umeme, na sasa hivi pia mafuta ya petroleum, limekuwa zigo kubwa kuanzia enzi za Lowasa na Kikwete. Mmasai huyo na mswahili huyo wa pwani ya Msoga walishindwa kabisa kulibeba zigo hilo la nishati. Alipopewa zigo hilo mnyamwezi wa Chato aliweza kulibeba vizuri zigo hilo na kuashiria kutimia kwa ndoto ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo 2025 (industrial country by 2025).

Awamu ya sita ilimbebesha zigo hili la nishati mswahili mmoja wa pwani ya Tanga. Kwa miaka takribani miwili mswahili huyu wa Tanga aligara gara na zigo hili hadi kutia huruma. Nchi ikakosa umeme kwa asilimia 60%, viwanda vikasimama kwa asilimia 40% na bidhaa kutoka viwandani vikapanda bei maradufu, ikawa haiwezekani kuanzisha viwanda vipya. Mbaya zaidi ikafikia hadi mafuta ya petroleum kuadimia kwa asilimia 90% na bei zake kupanda kwa asilimia 300%. Hali ikawa mbaya sana, uswahili ukawa mwingi ku justify hali hiyo.

Wahenga walishatuasa kwamba mzigo mzito mpe mnyamwezi abebe. Siku zote wahenga hawasei. Sasa zigo hili kabebeshwa mnyamwezi wa Bukombe. Tena kaongezewa nguvu ya unaibu waziri mkuu kulibeba hilo zigo ambalo kwa sasa limekuwa kubwa zaidi. Anahitaji mbinu za namna ya kulibeba. Jf kama jukwaa la Great Thinkers tumshauri mbinu anazoweza kuzitumia kulibeba zigo hili bila kuumia. Nitaanza na hizi chache:

1. Bwawa la NHPP lilishakamilika tayari kuanza kwa uzalishaji wa umeme. Sababu walizotoa hao waswahili ni kwamba kituo cha Chalinze cha kupitishia huo umeme hakijakamilika na wanatarajia kitakamilika mwezi July 2024. Ushauri: ziwashwe genereta mbili au tatu kati ya genereta 9 zilizopo pale bwawa la Nyerere. Hizi zitatupa MW takribani 600. Hizi ziingizwe kwenye grid ya taifa kupitia njia iliyo karibu na bwawa hilo. Waharakishe kujenga hiko kituo cha Chalinze, kikamilike ifikapo Desemba mwaka huu. Kijengwe mchana na usiku.

2. Umeme kutoka bwawa hilo usiuzwe zaidi ya TSh. 50 kwa kila unit moja ili hata mwananchi wa kawaida aweze kutumia umeme kupikia chakula badala ya kuni na mkaa.

Hao waswahili walishapanga kuongeza bei ya unit mradi huo wa JNHPP utakapokamilika. Walishasema kamwe hawatateremsha bei hiyo ya unit. Walishapanga kwamba kiasi kikubwa kama siyo chote cha umeme huo watauuza nje ya nchi hususani Zambia na Kenya kupata USD dollars, sisi tutaendelea kubangaiza huo umeme wa gesi kutoka Kinyerezi. Sababu waliyotoa eti ni kurudisha pesa iliyotumika kwenye ujenzi wa huo mradi.

Fedha zilizotumika kwenye ujenzi huo siyo zao bali ni kodi za wananchi zilizotumika ili wapate umeme wa bei nafuu na wa uhakika. Huwezi ukajenga hospitali au barabara kwa pesa itokanayo na kodi za wananchi, halafu ukataka kuwatoza tena wananchi hao wakitumia hiyo hospitali au hiyo barabara ili kurudisha pesa iliyotumika kuijenga. Vivyo hivyo kwa miundombinu zingine zinazojengwa na serikali au kwa vifaa na vitendea kazi vinavyonunuliwa na serikali hususani CT scan, MRI na kadhalika. Anayefanya hivyo ni mtu binafsi au kampuni binafsi aliyetumia hela yake binafsi kununua vifaa hivyo au kujenga miundombinu hizo. Pesa ya serikali inatoka kwenye kodi na tozo za wananchi. Hata kama pesa hiyo serikali ilizikopa, marejesho yake yanatoka kwenye kodi za wananchi.

3. Utaalamu (profession) unabidi uheshimiwe. Kwenye tasisi za kitaalamu, mtendaji mkuu anapaswa kuwa ni mtu aliyebobea kwenye hiyo taaluma. Huyo ndiye atakayeweza kuwasimamia, kuwaongoza na kuwaelekeza watendaji wenzake kwenye hiyo taasisi na kamwe haitakuwa rahisi kumdanganya.

Haingii kichwani mtendaji mkuu wa hospitali ya taifa kama Muhimbili akawa ni mwanahabari (journalist) halafu ukategemea ufanisi kwenye hiyo hospitali. Mhasibu akawa mtendaji mkuu wa TANROADS, Medical Doctor akawa mtendaji mkuu wa jeshi la wananchi au la polisi na kadhalika. Watu wapewe kuongoza maeneo ambayo wana utaalamu nayo. Wakurugenzi wa utawala wawe ambao wana taaluma ya utawala wa watu (public administration), wakurugenzi wa fedha lazima wawe wenye taaluma ya fedha na kadhalika.

Shirika la umeme, mtendaji mkuu wake anapaswa kuwa mbobezi kwenye taaluma ya umeme (senior electrical engineer). Vivyo hivyo kwa mameneja wa kanda, mikoa na wilaya. Vinginevyo shirika litaendelea kuchezewa na kudanganywa na wahandisi wake wa umeme.

4. Serikali inunue mafuta ya petroleum yenyewe moja kwa moja kutoka nchi zinzozalisha hayo mafuta. BoT na TPDC zitumike kutekeleza hili. Tutimize ndoto ya nchi yetu ya kuwa hub ya mafuta haya kwa nchi zinazotuzunguka na ambazo ni landlocked.

Tuachane kabisa kutumia hawa middle men ambao wametuchezea sana. Bei ya mafuta haya duniani yalifikia peak ya USD 135 kwa pipa mwezi March 2022. Baada ya hapo yalianza kushuka taratibu hadi kufikia USD 60 kwa pipa. Ni hivi juzi tu nchi za OPEC+ ikiwamo Russia zilipoamua kupunguza kidogo uzalishaji na kuwezesha kuyapandisha bei hadi kufikia USD 90 kwa pipa. Hii ndiyo trend ya bei ya mafuta haya duniani. Serikali kupitia wizara ya nishati na EWURA yao, imekuwa ikijifanya haioni trend hii na hivyo kuruhusu middle men hawa trend za bei zao ni ya kupaa tu kila mwezi kuanzia hiyo March 2022. Yaani leo sisi bei yetu kwa sasa ni maradufu ya bei ya mwezi March 2023 pipa lilipokuwa linauzwa dollar 135 wakati sasa linauzwa dollar 90 tu.

5. Great thinkers wa JF endeleeni kumpa mbinu za kulibeba hili zigo kubwa la nishati huyu mnyamwezi. Hapa mambo ya itikadiza kisiasa hazitakiwi. Na kama wewe siyo Great thinker hautakiwi.
Huo ni mtegp asijisahau
 
Huo ni mtegp asijisahau
Kwa nini Dotto Biteko ategwe? Kama ni kumchomoa mbona rahisi tu kama walivyochomolewa wengine kama wakina Kabudi, Lukuvi, Kalemani nk.
Huyu kijana ana uwezo wa kipekee ambao Rais ameuona unaweza kumsaidia kutatua hili tatizo kubwa la nishati lililolikumba taifa letu. Tayari cheche zake zimeanza kuonekana kwa wale wenye macho na masikio. Matokeo yataanza kuonekana bila shaka baada ya mwezi mmoja wa kazi yake. Ni kijana wa hapa kazi tu. Watanzania wanataka umeme na si bla bla.
 
Nishati ndiyo roho ya taifa lo lote. Uchumi na ustawi wa nchi hutegemea upatikanaji wa kutosha na wa bei nafuu wa nishati. Uharibifu wa tabia nchi unatokana kwa kiasi kikubwa na ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa kwa sababu ya ukosefu wa nishati mbadala ya bei nafuu.

Suala la nishati na hasa umeme, na sasa hivi pia mafuta ya petroleum, limekuwa zigo kubwa kuanzia enzi za Lowasa na Kikwete. Mmasai huyo na mswahili huyo wa pwani ya Msoga walishindwa kabisa kulibeba zigo hilo la nishati. Alipopewa zigo hilo mnyamwezi wa Chato aliweza kulibeba vizuri zigo hilo na kuashiria kutimia kwa ndoto ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo 2025 (industrial country by 2025).

Awamu ya sita ilimbebesha zigo hili la nishati mswahili mmoja wa pwani ya Tanga. Kwa miaka takribani miwili mswahili huyu wa Tanga aligara gara na zigo hili hadi kutia huruma. Nchi ikakosa umeme kwa asilimia 60%, viwanda vikasimama kwa asilimia 40% na bidhaa kutoka viwandani vikapanda bei maradufu, ikawa haiwezekani kuanzisha viwanda vipya. Mbaya zaidi ikafikia hadi mafuta ya petroleum kuadimia kwa asilimia 90% na bei zake kupanda kwa asilimia 300%. Hali ikawa mbaya sana, uswahili ukawa mwingi ku justify hali hiyo.

Wahenga walishatuasa kwamba mzigo mzito mpe mnyamwezi abebe. Siku zote wahenga hawasei. Sasa zigo hili kabebeshwa mnyamwezi wa Bukombe. Tena kaongezewa nguvu ya unaibu waziri mkuu kulibeba hilo zigo ambalo kwa sasa limekuwa kubwa zaidi. Anahitaji mbinu za namna ya kulibeba. Jf kama jukwaa la Great Thinkers tumshauri mbinu anazoweza kuzitumia kulibeba zigo hili bila kuumia. Nitaanza na hizi chache:

1. Bwawa la NHPP lilishakamilika tayari kuanza kwa uzalishaji wa umeme. Sababu walizotoa hao waswahili ni kwamba kituo cha Chalinze cha kupitishia huo umeme hakijakamilika na wanatarajia kitakamilika mwezi July 2024. Ushauri: ziwashwe genereta mbili au tatu kati ya genereta 9 zilizopo pale bwawa la Nyerere. Hizi zitatupa MW takribani 600. Hizi ziingizwe kwenye grid ya taifa kupitia njia iliyo karibu na bwawa hilo. Waharakishe kujenga hiko kituo cha Chalinze, kikamilike ifikapo Desemba mwaka huu. Kijengwe mchana na usiku.

2. Umeme kutoka bwawa hilo usiuzwe zaidi ya TSh. 50 kwa kila unit moja ili hata mwananchi wa kawaida aweze kutumia umeme kupikia chakula badala ya kuni na mkaa.

Hao waswahili walishapanga kuongeza bei ya unit mradi huo wa JNHPP utakapokamilika. Walishasema kamwe hawatateremsha bei hiyo ya unit. Walishapanga kwamba kiasi kikubwa kama siyo chote cha umeme huo watauuza nje ya nchi hususani Zambia na Kenya kupata USD dollars, sisi tutaendelea kubangaiza huo umeme wa gesi kutoka Kinyerezi. Sababu waliyotoa eti ni kurudisha pesa iliyotumika kwenye ujenzi wa huo mradi.

Fedha zilizotumika kwenye ujenzi huo siyo zao bali ni kodi za wananchi zilizotumika ili wapate umeme wa bei nafuu na wa uhakika. Huwezi ukajenga hospitali au barabara kwa pesa itokanayo na kodi za wananchi, halafu ukataka kuwatoza tena wananchi hao wakitumia hiyo hospitali au hiyo barabara ili kurudisha pesa iliyotumika kuijenga. Vivyo hivyo kwa miundombinu zingine zinazojengwa na serikali au kwa vifaa na vitendea kazi vinavyonunuliwa na serikali hususani CT scan, MRI na kadhalika. Anayefanya hivyo ni mtu binafsi au kampuni binafsi aliyetumia hela yake binafsi kununua vifaa hivyo au kujenga miundombinu hizo. Pesa ya serikali inatoka kwenye kodi na tozo za wananchi. Hata kama pesa hiyo serikali ilizikopa, marejesho yake yanatoka kwenye kodi za wananchi.

3. Utaalamu (profession) unabidi uheshimiwe. Kwenye tasisi za kitaalamu, mtendaji mkuu anapaswa kuwa ni mtu aliyebobea kwenye hiyo taaluma. Huyo ndiye atakayeweza kuwasimamia, kuwaongoza na kuwaelekeza watendaji wenzake kwenye hiyo taasisi na kamwe haitakuwa rahisi kumdanganya.

Haingii kichwani mtendaji mkuu wa hospitali ya taifa kama Muhimbili akawa ni mwanahabari (journalist) halafu ukategemea ufanisi kwenye hiyo hospitali. Mhasibu akawa mtendaji mkuu wa TANROADS, Medical Doctor akawa mtendaji mkuu wa jeshi la wananchi au la polisi na kadhalika. Watu wapewe kuongoza maeneo ambayo wana utaalamu nayo. Wakurugenzi wa utawala wawe ambao wana taaluma ya utawala wa watu (public administration), wakurugenzi wa fedha lazima wawe wenye taaluma ya fedha na kadhalika.

Shirika la umeme, mtendaji mkuu wake anapaswa kuwa mbobezi kwenye taaluma ya umeme (senior electrical engineer). Vivyo hivyo kwa mameneja wa kanda, mikoa na wilaya. Vinginevyo shirika litaendelea kuchezewa na kudanganywa na wahandisi wake wa umeme.

4. Serikali inunue mafuta ya petroleum yenyewe moja kwa moja kutoka nchi zinzozalisha hayo mafuta. BoT na TPDC zitumike kutekeleza hili. Tutimize ndoto ya nchi yetu ya kuwa hub ya mafuta haya kwa nchi zinazotuzunguka na ambazo ni landlocked.

Tuachane kabisa kutumia hawa middle men ambao wametuchezea sana. Bei ya mafuta haya duniani yalifikia peak ya USD 135 kwa pipa mwezi March 2022. Baada ya hapo yalianza kushuka taratibu hadi kufikia USD 60 kwa pipa. Ni hivi juzi tu nchi za OPEC+ ikiwamo Russia zilipoamua kupunguza kidogo uzalishaji na kuwezesha kuyapandisha bei hadi kufikia USD 90 kwa pipa. Hii ndiyo trend ya bei ya mafuta haya duniani. Serikali kupitia wizara ya nishati na EWURA yao, imekuwa ikijifanya haioni trend hii na hivyo kuruhusu middle men hawa trend za bei zao ni ya kupaa tu kila mwezi kuanzia hiyo March 2022. Yaani leo sisi bei yetu kwa sasa ni maradufu ya bei ya mwezi March 2023 pipa lilipokuwa linauzwa dollar 135 wakati sasa linauzwa dollar 90 tu.

5. Great thinkers wa JF endeleeni kumpa mbinu za kulibeba hili zigo kubwa la nishati huyu mnyamwezi. Hapa mambo ya itikadiza kisiasa hazitakiwi. Na kama wewe siyo Great thinker hautakiwi.
Pamoja na kua ushauri wako kamwe hawawez tekeleza ingawa una manufaa!! NB: Nakuhakikishia hata bwawa likianza uzalishaj umeme utakua ghali na mkatiko kama kawaida, tupo hapa!! Watanzania waliambiwa gas ya ntwara itamsaidia mtanzania kupata nishat hiyo kwa gharama nafuu pia itasaidia kuzalisha umeme na kua na umeme wa kutosha mpaka kuuza nje ya Nchi!! Nothing 'll be changed under this system!!
 
Kuwashauri ccm inabidi ujitoe fahamu. Pamoja na hilo bwawa Bado ume utapanda Bei.
Niko hapa!
Hautapanda bali utashuka sana kama Biteko atakuwa pale. Kuwa na amani ndugu yangu. Kama yule mswahili mwenye upara angaliendelea pale, ndipo ungalipanda tena maradufu.
 
Hautapanda bali utashuka sana kama Biteko atakuwa pale. Kuwa na amani ndugu yangu. Kama yule mswahili mwenye upara angaliendelea pale, ndipo ungalipanda tena maradufu.
Who and what is biteko? Jina lenyewe tu linakupa half of the story
 
Pamoja na kua ushauri wako kamwe hawawez tekeleza ingawa una manufaa!! NB: Nakuhakikishia hata bwawa likianza uzalishaj umeme utakua ghali na mkatiko kama kawaida, tupo hapa!! Watanzania waliambiwa gas ya ntwara itamsaidia mtanzania kupata nishat hiyo kwa gharama nafuu pia itasaidia kuzalisha umeme na kua na umeme wa kutosha mpaka kuuza nje ya Nchi!! Nothing 'll be changed under this system!!
Hiyo gesi ya Mtwara pamoja na hilo bomba la kutoka Mtwara hadi Kinyerezi tuliporwa na mwekezaji wa kutoka nchi fulani ya huko ulaya. Tuliingia naye mkaba mbovu sana, gas na bomba likawa ni mali yake na siyo yetu tena kwa miaka mingi ijayo kama si milele basi hadi gas hiyo iishe huko Mtwara. Tanzania huuziwa hiyo gas na huyo mwekezaji kwa bei anayotaka huyo mwekezaji aka mmiliki. Sasa hivi mwekezaji amepanga kuwauzia Kenya hiyo gas ila gharama ya ujenzi wa hilo bomba la gas nchi yetu itaghalimia.

Yaani huo mkataba ni mbovu kuliko hata huu wa DP World tunaokaribia kujitosa. Jiwe ulimshinda kuuvunja kwani hauna namna ya kuuvunja, vinginevyo nchi itakuwa inalipa matrilioni kila mwezi hadi kiama.

Dotto Biteko akiwa pale hilo bwawa la umeme la Nyerere kamwe hatapewa mwekezaji wa uendeshaji yo yote. Sana sana vijana wetu wa JKT wanaweza kusaidia shughuli fulani fulani za uendeshaji na watapewa mafunzo na uwezo. Hivyo bwawa litakuwa letu na bei ya umee itakuwa ni ile tunayotaka sisi wenyewe na kwa kuanzia haitazidi TSh 50 kwa kila unit. Yule mswahili wa Tanga angaliendelea kukaa pale bwawa lile angalipewa bure mwekezaji wa kutoka nje ambaye ndiye angalikuwa anatuuzia umeme kwa bei aitakayo na kiasi kikubwa cha umeme huo angaliuuza nje ya nchi. Hili alikuwa tayari ameshalitamka na kusisitizwa na mtendaji mkuu wake wa tanesco, Bw. Maharage wa DSTV.
 
Hiyo gesi ya Mtwara pamoja na hilo bomba la kutoka Mtwara hadi Kinyerezi tuliporwa na mwekezaji wa kutoka nchi fulani ya huko ulaya. Tuliingia naye mkaba mbovu sana, gas na bomba likawa ni mali yake na siyo yetu tena kwa miaka mingi ijayo kama si milele basi hadi gas hiyo iishe huko Mtwara. Tanzania huuziwa hiyo gas na huyo mwekezaji kwa bei anayotaka huyo mwekezaji aka mmiliki. Sasa hivi mwekezaji amepanga kuwauzia Kenya hiyo gas ila gharama ya ujenzi wa hilo bomba la gas nchi yetu itaghalimia.

Yaani huo mkataba ni mbovu kuliko hata huu wa DP World tunaokaribia kujitosa. Jiwe ulimshinda kuuvunja kwani hauna namna ya kuuvunja, vinginevyo nchi itakuwa inalipa matrilioni kila mwezi hadi kiama.

Dotto Biteko akiwa pale hilo bwawa la umeme la Nyerere kamwe hatapewa mwekezaji wa uendeshaji yo yote. Sana sana vijana wetu wa JKT wanaweza kusaidia shughuli fulani fulani za uendeshaji na watapewa mafunzo na uwezo. Hivyo bwawa litakuwa letu na bei ya umee itakuwa ni ile tunayotaka sisi wenyewe na kwa kuanzia haitazidi TSh 50 kwa kila unit. Yule mswahili wa Tanga angaliendelea kukaa pale bwawa lile angalipewa bure mwekezaji wa kutoka nje ambaye ndiye angalikuwa anatuuzia umeme kwa bei aitakayo na kiasi kikubwa cha umeme huo angaliuuza nje ya nchi. Hili alikuwa tayari ameshalitamka na kusisitizwa na mtendaji mkuu wake wa tanesco, Bw. Maharage wa DSTV.
Walaaniwe walioingia mikataba mibovu na wanaotaka kuingia!! NB Narudia tena... Hata bwawa likianza uzalishaj umeme utakua ghali na sio hiyo sh50. Kwa upendo gan walionao kwa watanzania mpaka wauziwe sh 50? Never ever!!
 
Dotto ni mnyarwanda yaani mtutsi na familia yake yote ni watutsi wazazi mke n.k
Kihistoria ukifuatilia (tracing) origin ya kila mtanzania utakuta hakuna mtanzania hata mmoja anayeishi Tanzania. Utakuta kumbe akina Mkapa kwao ni Msumbiji. Utakuta kwamba kumbe watu wa Msoga ni wasomali na kadhalika. Soma historia ya north to south migration ya makabila ya Afrika. Watanzania original wengi wao wako nchi za kusini hususani South Afrika. Hata wewe babu wa babu wa babu yako hakuwa mkazi wa Douche Ostoafrika aka tanganyika aka tanzania.
 
Sasa mwalimu wa upe unampa wizara ya nishati aiongoze?🤣🤣
Si ungempa wizara ya elimu ambayo ana ujuzi nayo aiboreshe? Hamna kitu pale
 
Walaaniwe walioingia mikataba mibovu na wanaotaka kuingia!! NB Narudia tena... Hata bwawa likianza uzalishaj umeme utakua ghali na sio hiyo sh50. Kwa upendo gan walionao kwa watanzania mpaka wauziwe sh 50? Never ever!!
Hatutauziwa bali tutajiuzia wenyewe kwani utakuwa ni wa kwetu, tena ni mwingi wa kumwaga na running cost ni negligible kwani unaendeshwa na maji ambayo ni ya bure.

Ukitoza Sh 50 kila unit na watanzania wote wakaweza kutumia umeme, serikali itakusanya pesa nyingi kuliko zile zinazokusanywa na TRA. Wewe kokotoa uone. Hivyo serikali itaachana na tozo za kipuuzi za kutafuta hela ya uendeshaji. Itapunguza hata hizo kodi lukuki kwenye kila lita ya mafuta ya petroli. Viwanda vitaongezeka na kuzalisha bidhaa zenye bei nafuu na kadhalika.
 
Sijamuelewa kwanini anataka magari ya serikali yaweke mfumo WA gesi...the best ingekuwa kuomba Toyota waweke kabisa huo mfumo kabla hayajafika Tz...but anyway labda sijui sana
 
Sasa mwalimu wa upe unampa wizara ya nishati aiongoze?🤣🤣
Si ungempa wizara ya elimu ambayo ana ujuzi nayo aiboreshe? Hamna kitu pale
Biteko ana PhD degree. Nyerere alikuwa mwalimu na alikuwa na MA degree tu, hafika PhD. Mwinyi alikuwa na Bachelor degree in education. Magufuli alikuwa pia mwalimu mwenye PhD kama Biteko. Mkapa alikuwa na Bachelor degree ya habari. Kikwete alikuwa na Bachelor degree ya sanaa.
Sasa wewe unaongea kitu gani? Walimu ndio best organizers and administrators wa kufanya mambo mazuri yatendeke. They are the best thinkers in the broad range. Huo ndiyo ukweli.
 
Huwezi fananisha Nyerere na huo uchafu
Nyerere hakuwa na vyeti vya upe🤣🤣
Na elimu ya supagluu
Biteko ana PhD degree. Nyerere alikuwa mwalimu na alikuwa na MA degree tu, hafika PhD. Mwinyi alikuwa na Bachelor degree in education. Magufuli alikuwa pia mwalimu mwenye PhD kama Biteko. Mkapa alikuwa na Bachelor degree ya habari. Kikwete alikuwa na Bachelor degree ya sanaa.
Sasa wewe unaongea kitu gani? Walimu ndio best organizers and administrators wa kufanya mambo mazuri yatendeke. They are the best thinkers in the broad range. Huo ndiyo ukweli.
 
Huyu Mheshimiwa hakuwa kabisa akilini mwangu. Si kuwahi kufikiri hata kumfuatilia hadi na andika hapa sijui alikuwa waziri wa nini.

Lakini, lakini, lakini,......!!!!! Nimemsikia kwenye kideo clip kwa ufupi akiongea na wafanyakazi wa Tanesco. Anacho kitu cha maana sana ndani yake. Kubwa zaidi anayo hofu ya Mungu. Anajua umuhimu wa kumuweka Mungu mbele ndio mengine ya fuate. Akipewa ushirikiano anaweza akawa kiongozi mzuri sana. Wasiwasi wangu ni fitina za kwenye siasa na kati ya wanasiasa. Wanasiasa wanaogopa sana kutokea mwengine akamfunika/akakubalika zaidi yake. Hawana ile ya kumtumia mwenye uwezo zaidi yako kufanikisha malengo yako.
 
Sijamuelewa kwanini anataka magari ya serikali yaweke mfumo WA gesi...the best ingekuwa kuomba Toyota waweke kabisa huo mfumo kabla hayajafika Tz...but anyway labda sijui sana
Serikali ingesitisha manunuzi ya magari yake yanotumia mafuta na yale yote yalotumika yangeuzwa.

Kisha dealers waagizwa kuleta magari mapya yenye kutumia hiyo gesi.

Yaani serikali yatakiwa kufanya mambo haya kwa awamu phase1, phase2 na kuendelea. Si kukurupuka tu usubuhi jogoo awika na waja na kauli tatanishi hata wale wauza mafuta waweza kupatwa na mstuko wa moyo.
 
Back
Top Bottom