Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,408
- 31,392
Nape,
Unapozungunguka huko mikoani, wilayani na vijijini hivi kweli huoni umasikini uliotamalaki! Hivi hujawahi kukaa na kujiuliza bajeti ya mwaka jana, juzi, na kurudi nyuma zimemsaidiaje yule masikini aliyekaa katika majani bila malapa kwa uchovu akikusikiliza.
Majuzi umesema chama tawala kimeagiza serikali iangalie mfumuko wa bei.
Sasa kwa bajeti hii unadhani mfumo utashuka au utapanda?
Hujiulizi kwanini serikali katika nchi tajiri kwa rasilimali kama Tanzania bado inategemea kodi za vocha za wapiga simu?
Nape, wewe na serikali yako mumefanya nini kuzuia misamaha kwa mafisadi, makontena kuingia bila kodi, wawekezaji kukwepa kodi kwa kubadili majina na wawekezaji kupewa muda wa kupora kabla ya kuondoka!
Nape, Hivi hujaona ni jinsi gani nchi hii ni tajiri na kudai kodi ya soda na bia ni ujinga uliokubuhu.
Unaweza kusimama kweli na kusema gharama za kuendesha serikali ni sahihi kwa kutumia akili tu.
Hivi hujiulizi kama baba mwenye familia kuwa unawezaje kuwa na mshahara wa sh 100 halafu matumizi yako yakawa sh 150! simple logic isiyohitaji degree.
Ninachotaka kusema hapa ni kuwa Nape Nnauye Jr you preach what you don't practice
Waache Watanzania waigombee na waigomboe nchi yao, wewe endelea kula mafao ndani ya VX ukipita kuwalaghai watoto wanaofia njiani, ukiwakejeli wakulima waliogonga na mijoka, ukiwadhihaki wanafunzi wasioweza kulipa ada kwa maneno matamu ya bajeti nzuri.
Unapozungunguka huko mikoani, wilayani na vijijini hivi kweli huoni umasikini uliotamalaki! Hivi hujawahi kukaa na kujiuliza bajeti ya mwaka jana, juzi, na kurudi nyuma zimemsaidiaje yule masikini aliyekaa katika majani bila malapa kwa uchovu akikusikiliza.
Majuzi umesema chama tawala kimeagiza serikali iangalie mfumuko wa bei.
Sasa kwa bajeti hii unadhani mfumo utashuka au utapanda?
Hujiulizi kwanini serikali katika nchi tajiri kwa rasilimali kama Tanzania bado inategemea kodi za vocha za wapiga simu?
Nape, wewe na serikali yako mumefanya nini kuzuia misamaha kwa mafisadi, makontena kuingia bila kodi, wawekezaji kukwepa kodi kwa kubadili majina na wawekezaji kupewa muda wa kupora kabla ya kuondoka!
Nape, Hivi hujaona ni jinsi gani nchi hii ni tajiri na kudai kodi ya soda na bia ni ujinga uliokubuhu.
Unaweza kusimama kweli na kusema gharama za kuendesha serikali ni sahihi kwa kutumia akili tu.
Hivi hujiulizi kama baba mwenye familia kuwa unawezaje kuwa na mshahara wa sh 100 halafu matumizi yako yakawa sh 150! simple logic isiyohitaji degree.
Ninachotaka kusema hapa ni kuwa Nape Nnauye Jr you preach what you don't practice
Waache Watanzania waigombee na waigomboe nchi yao, wewe endelea kula mafao ndani ya VX ukipita kuwalaghai watoto wanaofia njiani, ukiwakejeli wakulima waliogonga na mijoka, ukiwadhihaki wanafunzi wasioweza kulipa ada kwa maneno matamu ya bajeti nzuri.