Mzee Mtei hajafilisika mawazo - kasema ukweli

Mzee Mtei hajafilisika mawazo - kasema ukweli

mwanzoni nilikuwa najua ni CHAGA DEVELOPMENT MANIFESTO kumbe CRISTIAN DEMOCRATIC MOVEMENT? na hii ndo sababu ya kuanzisha jina la CDM badala ya chadema?

mungu wangu wee! kumbe ndo maana yake?
 
Wabongo mnanishangaza sana kuhusu suala la udini.
Yaani nyinyi mtu kuitwa Abdallah au John tayari mmesham-categorize kwenye dini fulani.

Mnasahau kua dini sio Jina, bali vitendo. Hivi mnawajua vizuri kimatendo hao mnaowaita waislam/wakristo???

Ok, tume ina wajumbe wengi wenye majina ya kiislam so wakristo wanalalamika, but waislam nao walalamike kwa kua Mwenyekiti wake Warioba ana jina la Kikristo????

Unataka ku-balance members between Zanzibar na Bara kwa kuweka idadi sawa. Zanzibar 99.99% ni waislamu so nusu ya wajumbe wote, yaani wale wa Zanzibar wote inakua waislam.
Unakuja bara atleast ni nusu kwa nusu so Bara unapata nusu waislam, nusu wakristo,
Mwisho wa Siku unategemea nini hapo?? Kosa liko wapi hapo??
hata wachache wana haki! Mbona bara ni wengi kuliko Zanz lakini idadi sawa?
 
Wakristo, wapagan, wabudha, wahindu na waislam, wote kwa midhani moja ninawaheshimu na kuwaamin katika hili la katiba mpya as long as tunaunganishwa na utanzania wetu.
Ndugu zangu hatuendi kuandika katiba ya taasisi ya kidini au kikundi fulan bali katiba ya nchi yetu. Na tulishakubaliana kuwa nchi yetu haina dini, sasa hizi porojo ni za nini? Hata hivyo ninaheshimu maoni ya mtu yeyote katika hili
 
Tutafutie wewe Wazanzibari unaoona wanaweza kuwa kwenye tume.

Ukishutumu kitu unatakiwa uje na mbadala, sio unalalama tu, na Serikali ya sasa ina Waislaam wangapi na Wakristo wangapi? chadema ina waislaam wangapi na wakristo wangapi?

Fikiri!

mawazo mgando, ina maana hakuna wakristo wenye uwezo Zenj? Cant blv this
 
Mzee wetu wa kichaga Mtei yupo sahihi kabisa. Hakukuwa na sababu za msingi kuwa na idadi sawa na wazanzibar. Nimetazama ramani ya nchi ya kusadikika tanzania, nikatazama Tanganyika then nikavaa miwani niweze kuiona zenj, nikatambua kuwa walioko magogoni akili zao hazifanyi kazi.
Sitaki mabishano, jaribu kufanya zoezi hili, chukua picha yenye ramani ya Tanzania, itazame sehemu ya Tanganyika then tafuta iliko zanzibaa utaelewa naongea nini.
Lazima akili zao pale hazifanyia kazi, zinawaza ufisdai muda wote. Mtu mwenye akili kichwani wawikilishi watatu tuu wangetosha kabisa kuiwakilisha zanzibaa, isitoshe huu muungano ni mzigo wa Tanganyika ifike mahali tuutueee.
Mimi naapa leo nitakuwa wa kwanza kuuvunja huu muungano wa kifisadi.
 
Wakristo, wapagan, wabudha, wahindu na waislam, wote kwa midhani moja ninawaheshimu na kuwaamin katika hili la katiba mpya as long as tunaunganishwa na utanzania wetu.
Ndugu zangu hatuendi kuandika katiba ya taasisi ya kidini au kikundi fulan bali katiba ya nchi yetu. Na tulishakubaliana kuwa nchi yetu haina dini, sasa hizi porojo ni za nini? Hata hivyo ninaheshimu maoni ya mtu yeyote katika hili
 
Mimi ninajua na kuamini Ukristo ni dini ya Kiyahudi kwa mapokeo ya mila za Wazungu, yaani Anglo Saxon.
Wakati Uislamu ni dini ya Kiyahudi kwa mapokeo ya Mila za Kiarabu. Hivi ni lazima tuishi Kizungu ama Kiarabu? Why is Ukristo ama Uislamu an Issue ya kutuumiza vichwa! Hivi hatuwezi kutoka out of the dini box? Mbona Kuna mataifa yanafanya vizuri bila Ukristo ama Uislamu.

A secular state is the answer.

Iran na Saudia kwenye Waislam wengi ama Uingereza na Marekani kwenye Wakristo
wengi kunamzidi nini Mchina na Mrusi kusikojali hizi dini mbili?

To h...with religion!
 
Duu! Thread kama hizi huwa zinakua na memba wageni wengi kwann?
 
Mwingira naimani upo JF mbona huleti jeshi lako la EFFATA hapa iliupambane na wana JF?
 
Kwanini mtu alaumiwe kwa mawazo yake ambayo watu hawataki kujibu kwa hoja bali in general tu bila kueleza sababu? Pamoja na kuwa nchi yetu haina dini watu wake wana dini zao nazo zinachangia sana katika maamuzi na chaguzi zao. Kama hivyo ndivyo kwanini basi ili kuleta mlingano sahihi katika nchi hii na kuepuka biases kusiwe na defined latent factors ambazo zina influence decision za watu? Moja ya hizo ni dini ambapo kwa hiyo tumeona watu wako tayari kufa wakizitetea.

Hili swala si dogo kama watu wanavyotaka kulifanya na Mzee Mtei na mpongeza kwa ujasiri wake wa kutamka hadharani bila kuangalia kama chama chake kita loose ama kita gain. Ameepuka kuwa mnafiki na mkimbia matatizo. Ame kubali kuface reality ili hatimaye suluhu ipatikane mapema kabla madhara hayajatokea mbele ya safari. Amekuwa kama yule mtoto aliye piga kelele za 'Mfalme yuko uchi' kwenye hadith ya Mfalme yule aliyependa kusikia yale tu yalikuwa yana mfurahisha. Kwa hili mimi nina simama pamoja naye hata kama tutaonekana vibaya. Na hata hivyo ameainisha swala zima la watu wasiofika milioni 2 kupewa nafasi kubwa ya uwakilishi kwa matamanio yao kulinganisha na walio wengi ambao ni mara 20 ya idadi yao. Ajabu ni kuwa hilo halizungumzwi bali la dini tu kuonyesha jinsi ambavyo hili swala ni muhimu kupewa kipaumbele. Tanzania kuna wapagani, hindu, Atheist, n.k kwanini hao hawakupewa kipaumbele katika k-dilute issues za uislamu na ukristo ambazo hata raisi mwenyewe amewahi kuongelea (swala la dini) na tumeona viongozi wa kiislamu wakilaumiana na wale wa ki-kristo kuhusu maswala ya kitaifa?

Mzee Mtei hapaswi kupuuzwa hata kidogo kwani alilolisema lina hold water na kwa reasonable person yeyote hawezi kukana kuwa hili swala ni la msingi kupatiwa ufumbuzi. Nitoe issue moja itakayo leta utata... Swala la OIC ni preference ya Zanzibar na waislam walio wengi na imesemekana Zanzibar ilishawahi kujiunga (Ref JF old posts) ikatakiwa kujitoa sasa leo hii tuseme linapendekezwa na kamati inalazimika kupiga kura kudecide kama liingizwe ama lisiingizwe je hapo unadhani katika referendum tutapewa option ya kudecide vipengele vipi tupigie kura ya ndiyo na vipi ya siyo? Kura ni kwa the whole document na kwa jinsi watanzania tulivyo tuko na emotional decision na siyo rational atleast attitude na behaviour studies zilizowahi kufanyika zinatuambia hivyo niambie kama hatutaingia katika sinto fahamu nyingine kama taifa? Je si busara ku solve hizi issues kwa kuwa pre-empty wenye mawazo haya mapema kabla hatuja complicate life yetu kama taifa nakuishia kukosa kabisa hiyo katiba tuipendayo? Think out of box na tukubali kusikia ukweli hata kama una uma vipi. In the same ways hata kama wa pagani na wasiomkubali Mungu ni wachache bado uki su-press sauti zao watatafuta vipaza sauti vya hatari ili wasikike na athari hizi hazitabagua walioshiriki na wasio shiriki. Ni vyema basi tukakubali kusikia busara ya mzee wetu huyu.
 
kauli ya mzee Mtei na mjadala unaoendelea humu unathibitisha kitu kimoja: kuna mushkeli kwenye mfumo wa Muungano. Hakun aubishi kwmba huko Zenj zaidi ya asilimia mia tisini ni Waislamu. Kwa hali hiyo watakuwa wengi katika mkusanyiko wowote ule, ikiwa ni pamoja na tume ya mchakato wa katiba. Bara inaweza kuwa hata nusu kwa nusu. Hata kama bara waislamu ni wachache, asilimia thethini ikuwajumuisha na Wazenj ni wazi watakuwa zaidi ya asilimia hamsini ya wajumbe wote wanaokusudiwa. Hivyo basi Rais Kikwete siyo wa kulaumiwa. Tunaelekeza mashambulizi yetu kusiko husika. Turudi kwenye hoja ya msingi ambayo ni mfumo wa muugano. Takafakari.
 
We na Mtei wako wadini wakubwa na roho zenu zina kutu mbaya kama chuma kilicho ardhin tangu mwaka 47. Nawe ni miongoni mwao wadini wakubwa.
mfichaficha maradhi kifo kitamuumbua.ukijaribu kujiweka nje ya box na kushirikisha ubongo wako vizuri unaweza kusema bila unafiki kwanini zanzibar hamna mjumbe mkristo hata mmoja?hakuna mkristo mwenye sifa ya kuwa kwenye hiyo tume?hii inaleta picha gani?...tuongelee facts na tuache kujadili watu na kutoa comment za kitoto.we are bulding the future of our nation for us and the coming generations....
 
Kama ni hivi, basi kosa lilianzia bungeni ambako zaidi ya nusu ya wabunge ni Wakristo. Walikubaliana muswada upite kwa nusu Zbar na nusu ya wajumbe wa tume watoke bara. Hili nalo wangefanyaje wakati wabunge wote ni CCM? Naona hapa ni vigumu kubalance cho chote nchi hii maana kila mtu ana mtazmo wake. Muhimu ni kutoa maoni yetu katika tume, na tuje tujadili maoni watakayotukusanyia, sio nani anayekusanya maoni...Tujadili nini tunakitaka ktk katiba sio nani yuko katika tume ya kukusanya maoni, tusipoteze muda miezi 18 ni michache sana.
 
Mtei kahitimisha ukweli unaosemwa kila siku kuwa CHADEMA ni chama cha mrengo wa kidini, amebainisha wazi na bla kificho. Hata mkatae vipi, I agree, Mtei hakufanya mistake, imebidi ahihirishe ukweli unaofichwa siku zote.

Hiki si chama cha kukiunga mkono, udini mtupu na watatuletea balaa kubwa kwenye nchi, wana nia mbaya kabisa.

Mtanzania yeyote asiye mdini hawezi kabisa kukiunga mkono chama hiki. Huo ni ukweli usiopingika.
mzee Mtei katoa maoni yake na siyo maoni ya chama...kwahiyo sioni point yako unapolazimisha kitu
 
Back
Top Bottom