Basi Nenda
JF-Expert Member
- Jul 29, 2017
- 20,175
- 45,897
Mkuu nitakuletea screenshot humu uoneMkuu nafikiri inatakiwa ujue hali ya siasa kuanzia 2015 kushuka chini ni tofaut kabisa na 2015 kuja huku juu.Ni mwaka 2015 vuguvugu la kisiasa lilikua kubwa sana toka taifa liitwe Tanzania. Utaona rate ya wafuatiliaji wa siasa saiz ni wengi mno kuliko kipindi hicho na kwa kipindi hiki Watanzania asilimia kubwa walihitaj CCM itoke madarakani lkn ndio hivo bado ipo.Utaona wanaomtukana na kumchukia jpm asilimia kubwa ni kundi lilelile toka uchaguz wa 2015 na ukifuatilia wengine ndio hawa kila mmoja ana maswaibu yake yamemkuta ktk baadhi ya mabadiriko ktk utawala huu.Mfano jirani yangu mmoja alikua anampenda sana jpm umwambii kitu na wakati huo mmewe alikua hataki kabisa mumsikia jpm.Baada ya sekeseke la Vyeti feki likamsomba Huyu mama, saiz ni hataki kabisa kumsikia jpm yaani hata kdg.Kwa mazingira haya kwanini namba ya wanaomchukia isiongezeke?
Na ukifuatilia mkuu hakuna mwenye hoja za msingi kwanini anamchukia jpm na hii ni wazi kwamba watu hawakuutaka huu utawala wa ccm uendelee, so kwa lolote atakalo fanya ni lzm apingwe tu.Utaona jpm kaanza kupingwa toka siku ya kwanza anaanza kazi.Je unataka kusema Tayar alikua ameshatumbua watu au vyet feki?Nachoweza kusema ni watu hasa upinzan kwa asilimia kubwa wameshindwa kurudisha majeshi nyuma.
Na kwa takwimu zako za fb au insta sijui labda kwenye page za huko upinzan tu,lkn ktk page ambazo ni Neutral sijaona kwamba ni utafiti sahihi eti watu wanamchukia. Shida nyingine nayoiona na bavicha kutoa maoni ya kwenye kundi la bavicha wenzie na kusema watanzania wanasema hivi.Kuna nilikua najadili naye nashangaa analeta habari ambazo nyingi anazitoa kwenye page ya chama chake, sasa nkamuuliza hayo ni maoni ya chama chako au watanzania wote?Huko insta au fb wanakoombea jpm afe ni bavicha katu huwez sema watanzania wote.
Sio page za upinzani ni page zote ITV,CLOUDS,AZAM nk
Ndio umesema kweli kuhusu watu kumchukia kisa yamewakuta ila ni baadhi sio wote
Wapo pia wanaomchukia kwa sababu hasa mbili
Uchumi na watu kutekwa /siasa chafu
Mkuu lazima ukubali ukweli kuwa JPM alipendwa sana 2015 mpaka mwanzoni mwa 2016
Ila tokea avuruge uchumi hakuna anayemtaka
Mimi binafsi mama yangu alikuwa na duka toka enzi za mkapa mpaka Jk
Ila amelifunga 2016
Wateja hakuna vitu vimeharibikia dukani mfano poda,maziwa,lotion nk
Hivi umewahi kuona soda zinakaa mpaka zinaharibika ? Sasa sisi yalitukuta