Mzee Kikwete, tulikukosea nini Watanzania?

UKWELI MAKUFULI NI BEST KULIKO WALIOTANGULIA MSEME MTAKAVYOSEMA LAKINI POMBE NI RAIS MZURI SANA KALETA HASHIMA KATIKA NCHI WATU WANAHESHIMIANA NA MAMBO MENGI NIKIELEZA HAPA ITACHUKUWA SIKU
Hovyo kabisa wewe,anyway Hata shetani anapendwa...
 
Nitamwombea tu kwa maana kila mamlaka imewekwa na Mungu.

Kuiongoza nchi si kazi ndogo. NI MZIGO.
Nyie huwa mnasoma Biblia kama Kitabu cha hadithi,pole sana mkuu...
"Itiini kila mamlaka,maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu"
Tafsri Sahihi: "Zitiini sheria zote nilizowapeni mimi Mungu wenu".
Neno mamlaka " Authorities " halimaanishi serikali .
Na siyo kila serikali Duniani imewekwa na Mungu,kumbuka Mungu si mwanadamu,kwa hiyo si muuaji...Mungu hawezi kusimika Dikteta,anayeteka watu na kupoteza wanaompinga...
1.Mobutu aliwekwa na Mungu?
2.Saddam aliwekwa na Mungu?
3.Bokassa aliwekwa na Mungu?
4.Samuel Doe aliwekwa na Mungu?
5.Idd Amin aliwekwa na Mungu?
6.Hitler aliwekwa na Mungu?
Ndugu Mungu si muuaji Hata aweke muuaji.
Kwa hiyo JPM hakuwekwa na Mungu, hiyo ni kazi ya Lucifer.
 
Dhaifu,professor busha,fisadi
Hahahahahahahah.....
Umesomea wapi ndugu?
1.Dhaifu ni tusi? (Dhaifu ni sifa)
2.Fisadi ni tusi?(Fisadi ni sifa,adjective)
3.Profesa Busha ni tusi? (Profesa Busha ni jina la mzaha,utani,)
Naona hujui matusi wewe,vijana wa Lumumba mmesomea wapi?maana akili zenu wote zinafanana.
 
Najua ya kwamba ulikuwa ukitupenda sana,japokuwa una mapungufu yako kama Binadamu wote tulivyo lakini ulijitahidi sana kutufanya wenye furaha.

Lakini Dakika za mwisho ukawa si wewe tena tuliyekuwa tunakujua,mwingi wa hekima,mpole,mwenye subira,mnyenyekevu na usiyependa makuu wala kujikweza.

Ni kitu gani tulikukosea hadi ukachukia?

Najua Mzee wangu huwa unapita humu kimya kimya,nami natarajia jibu lako kimya kimya.
Wewe utakuwa ulikuwa fisadi enzi za JK, sasa mirija yako imekatwa unalalama hapa kwenda huko, jk sitaki hata kumsikia
 
UKWELI MAKUFULI NI BEST KULIKO WALIOTANGULIA MSEME MTAKAVYOSEMA LAKINI POMBE NI RAIS MZURI SANA KALETA HASHIMA KATIKA NCHI WATU WANAHESHIMIANA NA MAMBO MENGI NIKIELEZA HAPA ITACHUKUWA SIKU
Safi kabisa mkuu wape ukweli hawa mafisadi, yaani mirija ya ufisadi imekatwa wanakuja kubwabwaja na bado
 
Na wewe tumia Hata akili za kuazima,mtu hawezi pendwa na wote,Hata awe mwema.
Huwa tunaangalia percentage ukimlinganisha huyu jamaa na JK,huyu anachukiwa mno,na hatakaa apendwe..
Duh tatizo huwa linaanziaga hapa ambapo mtu unajikuta una akili nyingi kuliko mwingine...eti nitumie hata akili za kuazima

Ila sio mbaya we ni M-Tz mwezangu naheshimu sana fikra zako
 
HAKUNA RAIS ALIEKUWA ANAPONDWA NA KUPATA KASHIFA MBAYA KAMA KIKWETE.ILA NASHANGAA KWA SASA NDIO ANAONEKANA BORA KAMA MALAIKA
KWA AKILI ZETU WANADAMU HUWA HATULITAMBUI JEMA HADI TULIKOSE
HUENDA,NARUDIA TENA HUENDA HATA MAGUFURI BAADAE TUTAKUJA KUANDIKA HUMU TUKIMKUMBUKA NA KUMMISS
Acha kutia chumvi kwa utashi wako na mapenzi yako binafsi kwa JK!!
Nani kasema JK alikuwa au anaonekana lulu au bora kama malaika? Hivi ukiambiwa uchague mnyama mmojawapo wa kukutananae njia kati ya Simba na Chui, mfano ukasema heri ya Simba atakuonea huruma atapita bila kukudhuru inamaana huyo Simba anabadilika kuwa Kondoo!
Hakuna umalaika au ukondoo, kinachosemwa na watanzania hapa ni "choose the the less dangerous/ less harmful na sio not dangerous au not harmful".
 
mzee huyo alisema"MUTANIKUMBUKA",mara baada ya maneno hayo akatoweka.......taarifa iliendelea kusema.
 
Mimi kabisa nikae nammiss huyu jamaa wa sasa

Huwezi jua ndugu!

Linaweza likaja lijamaa likasema kijiji chenu chote wake zenu wote ni halali ya lenyewe na marafiki zake kwa wiki nzima! Aaah, ni kama nakuona ulivyojikunja na kuknja mdomo!

Hebu hapo sasa,kwa jinsi nchi yetu hii ilivyo, hutaweza kukumbuka na kusema angalau kumbukumbu tu na mlinganisho wa wakati huo na sasa?

Na bado lijamaa linaweza kuwa na mabaya zaidi ya huo mfano; hata likitaka kuweka vichwa vya wapinzani wake kwenye jokofu, tutafanya nini; si itabaki kulinganisha na kukumbuka tu, na pengine kusema heri ya wakati ule (yaani sasa).

Kwa hali na uzoefu tulioupata ndani ya nchi yetu hii ni kwamba tunapompata kiongozi, mtu huyo anachukua madaraka makubwa mno na hatuna njia ya kuweka breki. Hatuna njia ya kuzuia asifanye anachotaka kwa wakati wowote, kwa yeyote, na kwa sababu anazozijua mwenyewe bila ya kuhojiwa na yeyote.
Hiyo ndio hali halisi.

Bado huamini?
 
Mauaji arusha, mwangosi, Ulimboka nk huenda ilikua ni kipindi cha Id amin
NAAMINI ILIKUWA MATUKIO YA POLISI HAYO UNAYOSEMA! ILA KWA SASA YAMEZIDI, KUNA WANAKUFA WAKIWA MIKONONI MWA HAO WANAUSALAMA NA WENGI WANATEKWA. FREQUENCY YA MATUKIO NI KUBWA MNO.
 
NAAMINI ILIKUWA MATUKIO YA POLISI HAYO UNAYOSEMA! ILA KWA SASA YAMEZIDI, KUNA WANAKUFA WAKIWA MIKONONI MWA HAO WANAUSALAMA NA WENGI WANATEKWA. FREQUENCY YA MATUKIO NI KUBWA MNO.
Acha unafki wewe, waliomtesa ulimboka ni wanausalama, mwangosi alikufa mikononi mwa vyombo vya usalama. Yale matukio yalikua na ushahid wa moja kwa moja. Haya yanatokea saiz ushahid unao?Kupotea kwa Ben saanane unaushahid kuwa ni serikali?Kubenea alikuambia kamuona saanane, vipi mliangaika kumhoji?Juzi Kubenea na komu walikua wanapanga kumteka Boni, ingekuaje kama wangefanikiwa?Ungekuja hapa kusema ni chadema au ungeendelea kuongeza idadi kuwa serikali imemteka Boni na hivi Boni aliwahi kwaruzana na makonda ndo kabisa ungepigia mstar.

Huna tukio hata moja unaloweza toka hadharani kwa ushahid na kusema serikali imefanya zaid ya kuungaunga vistory vya kwenye mtandao. Lkn huko nyuma kuna ushahid wa moja kwa moja serikali kuhusika. Tukianza Arusha, Iringa hadi kwa Dar. Ni awam ile tulishuhudia Upinzan ukitembezewa kichapo hadharani, kumbuka kipigo alichopata lipumba. Leo hii kisa mmejaa unafki na chuki ktk utawala huu mnasema kipindi hicho ilikua bora. Ubora wake upi?Uliwah sikia mtu kafukuzwa kaz baada ya mwangosi kuuawa?Au ndo mtu alipanda cheo?Usalama wa taifa ulihusishwa moja kwa moja kumteka ulimboka, je kuna mtu aliwakibika?Leo hii matukio mauchafu huko nyuma mnatumia nguvu kubwa kuyatenganisha na utawala wa jk, hii ni ajabu sana na matukio ya saiz mnatumia nguvu kubwa kuyafanya ni ya jpm.
 
Magu kamwe hatopendwa
Msiharibu historia
Jk ndio alikosolewa sana lakini hakuchukiwa
Mleta mada anaongelea mapenzi ya watanzania juu ya kikwete. Aliombewa afya hata alipoumwa
Ni nani uliona au unaota mitandaoni anamuombea JK kifo ? Hakuna ila huyu nanii huko mitandaoni watu wanamuombea mpaka kifo
Muwe mnapitia Facebook , twitter na instagram muone jinsi mkuu hapendwi

Narudia
MUACHE KUPOTOSHA HISTORIA
MZEE JK ALIKOSOLEWA NA WACHACHE HASA WANASIASA WA UPINZANI NA HAKUWAI KUCHUKIWA NA WATANZANIA WALA KUOMBEWA KIFO HIVO USIMFANANISHE NA MTU MWINGINE

JPM anapendwa zaidi, kwa kila mwenye akili timamu

jizi,vivu na fisadi kama wewe utaongea yote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom