Mzee baba, pakacha limeanza kuvuja ujue...

Mzee baba, pakacha limeanza kuvuja ujue...

Tapata wapi Vitabu vya fasihi ili niweze elewa nyuzi hizi,Vitabu vyenye fahihi zifuatazo karumekenge,mfalme ****,Kibanga ampiga mkoloni, ngoswe,wagagagigikoko,adili na nduguze nk
Sijui mkuu
 
A name or username or user ID can mean a lot in our life.. And it can affect us in a very strange way... Just like word crippled... Direct Swahili translation is kilema... If in any case this word appears in your name or username it may lead to a crippled mind....

kilemakyaaro ni kilimanjaro!!!kwa kichaga!!!
 
Andika kiswahili wala sijakuelewa umepoteza muda mpare
Alimaanisha hivi; kwakua ID yako ina neno kilema, vile vile Mind yako itakua na ka ulemavu (kilema ) fulani hivi coz Bashite (au sijui Makonda) uliyemzungumzia humu hakutajwa na mtoa mada, ( hata kama ID yako ya kilemakyaaro = kilimanjaro) na kilimanjaro hatuna mazwazwa kama wewe wasiojua kupambanua mambo
 
Alimaanisha hivi; kwakua ID yako ina neno kilema, vile vile Mind yako itakua na ka ulemavu (kilema ) fulani hivi coz Bashite (au sijui Makonda) uliyemzungumzia humu hakutajwa na mtoa mada, ( hata kama ID yako ya kilemakyaraaro = kilimanjaro)
Huyo Mshana yeye anawazaga matunguke yake ya upareni tu
 
Iweke kama user ID, na sio jina la mahali.. Pia naomba rudia mstari kwa mstari nilichoandika
vyovyote iwavyo haina uhusiano na neno kilema au upungufu wowote kama ulivyotaka kutanabaisha!!tafuta namna nyingine za kumponda huyo jamaa lakini sio kudhalilisha lugha za watu za heshima za mababu na mababu zao
 
Tuhuma ni tuhuma tuu... Lakini kwangu tuhuma zisizothibitika wala kuthibitishwa zinabaki kuwa uzushi.... Na mimi sina kaliba na uzushi.... Sijui nini kilinipelekea kukumbuka riwaya ya Ngoswe... PENZI KITOVU CHA UZEMBE... Dah nikayakumbuka ya kudamka alfajiri na mapema kwenda kule kilimani kumuona cheupe dawa... Si adhabu hii jamani... Mateso bila chuki... Kiroho safi kabisa... Hongera mzee baba... Hongera cheupe....

Kuna wale wazee na kawimbo kao kalikokosa udhamini wa kuingia studio... Naambiwa singo yao ile haikidhi vigezo... Kale kawimbo ka MATEMBELE NI MATAMU.... Kweli Ngoswe aliona mbali... Na mtunzi wa MATEMBELE aliona karibu....

mzee baba huku kwenye chama la wana hali si shwari... Wanachonga waziwazi sasa hivi... Hawana shukrani na hawana upendo kwa wageni.. Kwao wao mgeni ni siku ya kwanza tuu... Sasa wnalalamikia uwingi wa wageni... Wenyewe wanawaita wakuja.. Wanawaita mizigo... Wanawaita wadekaji.... Hali si shwari sana pakacha limeanza kuvuja....

Mkubwa mpya wa usalama wetu Barabarani naye kaharibu... Japo ndio kutenda kwa weledi... Anapingana na dhana ya kukusanya mapato yetu ili kibubu kitune... Wanakaya wamemfurahia sana... Hakuna tena kutoza faini za kijinga... Kwahiyo hapa hakuna tena viwango elekezi vya kukusanya kwa siku wiki hata mwezi... Wanakaya wamepata mkombozi hatimaye... Mungu naye hujibu maombi kwa wakati wake....!!!!... Ila zile mbwembwe za jeshi la polisi kujivunia kuwa mwezi huu wamekusanya billion ngapi zitakoma.. Wao sio kitengo cha mamlaka ya mapato.. Faini za uonevu kwishney....

Mzee baba pakacha limeanza kuvuja... Wameanza kupambana na wewe... Mbwa anataka kula mbwa... Filamu ya half ray imedoda... Ile ya viongozi 20... Filamu ya nabii Tito imechacha.. Wanakung'ong'a.. Kikulacho ki nguoni mwako... Wasikupake mafuta kwa mgongo wa chupa..... Ni wanafique

Uliyasikia ya Benedict ? Yule mtia nia?
Uliyasikia ya Nnauye Jr?
Uliyasikia ya bwana Ole ?
Umeyasikia ya Riz moko?
Wote wametoa ya moyoni halafu wakakana lakini neno likitoka limetoka ni kama risasi haina rivasi.... Basi ndio hivyo mzee baba... Hao wote ni kiwakilishi cha wengi ndani ya chama la wana...pakacha limeanza kuvuja... Naamini halijasababishwa na Ngoswe.... Inatosha tu kusema.... MATEMBELE ni MATAMU....!!!!
Tatizo mzee baba anatumikia upande usio na mwangaza, halafu ahadi alizotoa akapewa ufalme ndo zinamtesa saivi.

Anakula fahari ya ufalme kwa nje ila kwa ndani anatumikia kiapo ambacho hakitamwacha salama.

Angejua asingenadi nafsi.
 
Hallooo!!! Mkuki kwa nguruwe mtamu, ila kwa binadamu mchungu kama nini!!

Huu mkuki uko kifasihi zaidi, pole kwa aliyeguswa.

Asante Max na team yako ya jamiiforums la sivyo magereza zingekuwa pomoni!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom