Ni kweli kabisa maneno yako.Daaaa hongera sana tena sana mkuu naamini kuna mafanikio mengi sana ndani ya nyumba endapo mtakaa na kuelewana.......
Mkuu, nuksi ni jinsi wenyewe mnavyoendesha maisha yenu, mkiendesha kwa ubinafsi na kutosikilizana na kujaliana kweli mtayaona maisha ya ndoa kama nuksi, lakini ni wenyewe kwenye ndoa ndio mnaoweza kutengeneza maisha ya furaha au kuraha.ndoa yenu ni mfano wa kuigwa hiyo.
Lakini pia kuna watu ndoa zao ziko kama zina nuksi, mkosi na mabalaa.zimejaa chuki, ghadhabu na kukasirikiana.
Ahsante mkuuHongera sana sana Mkuu
Nashukuru sana kwa dua yako mkuu.Hongera sana mkuu. Nawaombea muendelee kudumu pamoja.
Nami nasema nawe pia Mwenyezi Mungu akupe furaha na maisha marefu yenye afya na siha njema, wewe na familia yako Insha'Allah.Hongera sana mkuu.Mungu awaongezee miaka mingi yenye furaha tele.
Ahasnate sana Fe Lady.Hongera sana 12 si mchezo.
Hayo ndio mambo yanayotakiwa kwenye ndoa, ukiweza kusamehe na kujisamehe mwenyewe, ni moja ya dawa nzuri sana ya kujiepusha na maradhi makubwa kama vile magonjwa ya shinikizo, sononi (depression) na hata magonjwa ya akili, maana mwili wako unakuwa haujengi sumu ndani kwa ndani, wataalam wanasema kuwa mwenye kupenda kuchukia wenzake na asiyependa kusamehe wenzake basi anakaribisha maradhi ya unyonge na kuufanya mwili usiweze kufanyakazi vema.Hongera sana umenipa motisha sana na umeongea kwl tupu ndoa ukiipenda lzm ikutendee haki cn miaka mingi sana ndani ya ndoa lkn cjawah kujuta kuolewa kiac hata ikitokea mume kanikosea namsamehe kabla hata hajaomba msamaha. Mungu awajalie maisha marefu zaidi.
King'asti shukran sana kwa maneno yako mazuri na ya kutia moyo.Hongera sana x-paster kwa hatua hii kubwa na kwa kumjulia mkeo. Mpe hongera zake pia kwa kukujulia na kuuteka moyo wako kiukweli. Mungu awajaalie maisha marefu zaidi, I am so proud of u kama kichwa cha nyumba kwa kuthubutu na kuweza kuongoza meli yako. Big up!
Oh! my brother long time no see, umepotelea wapi wewe, karibu tena kaka.Kiongozi, Allah (SW) awape baraka na amani tele, na pia awakuze watoto kayika misingi ya Unyenyekevu.