My upcoming trip to Jordan

My upcoming trip to Jordan

Ukiwa unaelekea airport. Please tell me where are you flying to??

By the way ahsante kwa kuusikiliza

Nooh sio kwamba sasa hivi ndo naelekea airport hapana bali huwa nasikiliza ule wimbo wa wizi kid kipindi nna safari na nikiwa natoka nyumbani kuelekea airport na wakati wa kurudi nikiwa natoka hoteli kuelekea airport huwa nausikiliza huo wimbo. Pia nikifika salama nilikokuwa naenda (hotelini huwa nausikiliza huo wimbpo na kucheza, sasa nilipousikiliza huu wa Konde Boy ndo nikasema asante kwa kuniongezea playlist kwenye nyimbo zangu nikiwa anelekea airport.

Safari bado hazijaanza, ntakuja kuweka hapa kuelezea uzoefu wangu kwa vacation nilizoenda kipindi cha nyuma.
 
Nooh sio kwamba sasa hivi ndo naelekea airport hapana bali huwa nasikiliza ule wimbo wa wizi kid kipindi nna safari na nikiwa natoka nyumbani kuelekea airport na wakati wa kurudi nikiwa natoka hoteli kuelekea airport huwa nausikiliza huo wimbo. Pia nikifika salama nilikokuwa naenda (hotelini huwa nausikiliza huo wimbpo na kucheza, sasa nilipousikiliza huu wa Konde Boy ndo nikasema asante kwa kuniongezea playlist kwenye nyimbo zangu nikiwa anelekea airport.

Safari bado hazijaanza, ntakuja kuweka hapa kuelezea uzoefu wangu kwa vacation nilizoenda kipindi cha nyuma.
Ohhh kumbeeee. That's nice!

Uni-tag ukija kuweka huo uzi aiseeee. Sisi ndio wadau wenyewe
 
Hao habshi ndiyo wahabesh??
Habshi ni waafrika waliopo India...ni jamii ya East Africans waliofikishwa India miaka mingi iliyopita kiasi kwamba hata lugha na baadhi ya tamaduni za Kiafrika ziliwaondoka na wengine wakachanganya damu na wahindi...

Wahabeshi ni Waethiopia, wapo hapo kaskazini ya Kenya katika taifa la Ethiopia
 
Relief Mirzska, Wowww wooww woow
You have made me read the whole thread. Nothing captivates me like reading and travelling maana zote zafungua my sense of imagination and see things beyond my present world.

Kwangu priority ni kusafiri na kuishi a simple and comfortable life. I like to hussle ila sio kukamia maisha 365 days a year bila kubreath. Kama wengine wanavyosave kununua prado and all that my soul gets better na kusafiri ( of course baada ya mahitaji muhimu kuwa met)

I have on my bucket list ( muda ukiruhusu ipp siku nitashare my two most amazing experience za Greece na Egypt maana zimeacha alama moyoni

1 Switzerland...Done
2. Egypt ....done
3. Indonesia ...bado
4. Rome ....bado
5. Greece....Done twice and still wish to repeat
6. Ethiopia....done
7. Australia...bado
8. Belize...bado
9. Israel....bado
10. Lebanon...bado
11. Moroco...bado

Tz
LUSHOTO...Done
Ngorongoro..bado
Mbeya hills ..bado


The feeling mtu unapata ukifanikiwa kutembelea sehemu mpya is so refreshing , mind opening.
 
Umetembea mkuu. Heshima kwako.

Tatizo langu mimi I have only 30 days leave in a year, hapo nipange kila kitu bila kusahau kuspend sometimes in Tanga with parents.

Ila no worries ntawahi ku-retire ili niweze kuizunguka dunia

Mkuu hizo safari ni miaka mingi sio kuwa lazima kila mwaka niende kutembea zingine namalizia home
Ila kwa likizo ya mwezi mbona nyingi tu maana huwezi kukaa nchi ya ugeni kwa zaidi ya wiki 2
Hapo wiki mbili zinatosha sana kwa kutalii
Na mbili zingine unaenda home kwa ndugu na wazazi
Kila la kheri
 
Inapendeza sana pale tunapopeana hamasa kwenye mambo kama haya. Ubarikiwe sana.

Kwasasa mimi nina mpango wa kutembelea mikumi, ngorongoro na Mt Kilimanjaro. Serengeti, manyara na Tarangire tayari nimeshatembelea.

Nilikuwa napata aibu na pia kuchekwa kipindi nipo nje, na rafiki zangu wa pale wanaijua Tanzania kuliko mimi ninavoijua.
Na hizi ziara ninazozifanya hapa ni ule motisha nilioupata kutoka kwa friends ambao kila kipind kimoja cha mwaka huwa wanakuja kutembelea Africa. Nikasema na mimi sikubali lazima nitembelee ili wakiwa wananiuliza kuhusu Tanzania nipate cha kusimulia.

Kwasasa tuna ratiba ya kwenda
- Singapore.
-Germany specifically Bavaria.
-Norway.
-Spain, specifically Barcelona.
 
Tofauti kati yetu na Wazungu sisi hatutalii wao wanatalii. Mzungu akija Afrika anakuja kwenye vivutio vya utalii. Sisi tukienda kwao twaishia hotelini kupiga picha za kuringishia watu.
Kingine ni kuwa sisi huko Ulaya au nje ya tanzania hatuendi kutalii bali kutembea tu
 
Duh! Wewe mkali
Seriously, sema tu science ikajaga kunishinda nikaona nidrop lakini ningekaza ningekujaga kusomea aviation na hatimaye kuja kusomea astronomy japo wazee walikuwa wanapenda nije kuwa doctor ila niligoma.

Nilipokuwa mdogo ndoto zangu zilikuwa ni kuja kuwa pilot ili tu niwe nasafiri kila siku yaani hadi leo nikiona ndege inapaa au inatua airport huwa naiangalia muda mrefu na huwa napata furaha ya ajabu sana, lakini I'm proud mdogo wangu anayenifuata ndiyo kaja kusomea aviation na anaiwezea japo yeye hataki kuwa pilot sababu hapendi kusafiri yeye anataka tu kuwa aviation engineer.
 
Back
Top Bottom