Hahahahahahahahhahaha!
Mimi nlidhani all this time unataka ukiwa mkubwa uwe kama
cute b !!!!
Dunia inakwenda kasi sana.



cute b si bado mdogo sasa
By the way nilishawahi kuandika humu kuwa hata mama yangu mzazi anajua kuvaa kuliko mimi yaani yeye na dada yangu wa kwanza pamoja na mdogo wangu anayenifuata wananishinda kwenye kuvaa
Yaani mimi najiona kabisa nitakavyofanikiwa mapema maana sipendi anasa sijui kuvaa, situmii makeup, sivai mawigi wala siweki kucha za bandia (maana hivi ndiyo vitu vinavyomaliza hela zetu wanawake kwa asilimia kubwa)
Yaani hata ndugu zangu wameshalijua hilo kwamba mimi napenda sana kusafiri kuliko kufanya hivyo vitu, nikiwa Mbeya nikienda kutembea milimani huko huwa nawapigia simu kuwaambia leo nimeenda kutembea sehemu fulani na fulani.
Nakumbuka kuna kipindi ajali zilifululiza kule Mbeya milimani huko, sasa kuna siku ilitokea ajali kubwa iliyowashitua watu, nakumbuka siku hiyo mama alinipigia simu kuniuliza kama mzima nikamuambia ndiyo akasema anhaa nimesikia kuna ajali imetokea, nikakupigia kujua kama ni mzima maana hauchelewi kuwa umeenda kuzurura milimani huko ikakukuta nikamuambia sikuenda.
Ninayeona kidogo ana hobby ya kusafiri ni dada yangu wa kwanza japo yeye anapenda sana safari za ndege na basi kidogo, mimi sichagui yaani ndege, basi, meli na treni vyote twende tu tena kama safari za Dar Mbeya nishapanda sana treni za tazara zile yaani vile tunavyokaa siku mbili njiani mie ndiyo napenda na hamna stress sababu mule ndani kuna kila kitu siyo ndege lisaa limoja tu tumefika khaa.