My cup runeth over ~ Na Kikombe changu kinafurika

Maringo na mama yake haoo hospital, kufika nyomi kibao, wazazi ma aunty baba wadogo uncles, eh wakaona hii balaa wakaamua kusepa waje skunyingine. Wakaenda bank kwa Maringo ku resign akafika akamshukuru Bank manager kwa kumsaidia sana lakini ameona a resign anaenda kumwuguza baba yake amepata stoke na yeye hana mama. Mmmh meneja akawa anawasiwasi ila kwa hali aliomkuta nayo Maringo ya kupaniki, akaamua kumpokelea barua akampa pole akampa dola 300 za kuuguza akawaaga akina Oga na Musa akaondoka. Akina Oga wanashangaa Maringo ndani ya Vx V8?! Mbona majanga?!
Wakatoka ofisini wakaenda nyumbani kwa Maringo Romaa! Mama mtu anashangaa mwanaume gani huyu kamficha mwanangu kha! Mbona hata mimi nimezidiwa?! Akawa hajisomi haipandi haijumlishikiki, akamwambia mwanae nionyeshe basi mkwe wangu, maana sio kwa ufahari huu uliopewa. Maringo akamwambia mama yake ngoja tu mama si upo mjini wala usiwe na wasi wasi! Wakashinda wote mama mtu akaamua kulala siku 3 hapo, Patric akimpigia anamwambia nipo kwa Mwanangu Roma, Patric anasinyaa!

Selina na wimbi la mawazo, wiki zimebakia 2 anatakiwa achezee karata zake vizuri ili apate hela ya kumweka kwenye high life. Akaona aende kwa mganga lakini akajua ya mganga sio yameshamtibulia kwa kibabu! Akaamua kwenda kwa Pendo kuomba msaada dukani kwake. Akakaribishwa uzuri wakawa wanaongea akamwambia jinsi gani mama yake alimfukuza kwake alipoenda. Pendo akajikausha me sijui jaman pole sana mama yangu bwana can be dramatic sometimes! Pole sana kumbe anajua ramani yote!

Wakaongea weee, Pendi ni msiri vibaya mbo Selina anashangaa hasemi chochote kuhusu joseph akitaka kumuanza anashindwa akaishia kumwambia nikopeshe mil 3 nina shida nazo nitakurudishia baada ya miezi 6. Pendo akaguna mmm. Akamjibu unajua duka langu halifanyi vizuri, ni majanga, ni balaa tupu hapa nadaiwa rent ya nyumba sijalipa wateja hamna sikuhizi sijui ni hali ya uchumi hapa natamani nifunge hii biashara nifanye ingine. Selina anashangaa! Akaondoka kichwa chini miguu chini! Anawaza ataishije! Akaamua kurudi kwa babu kuomba msamaha warudiane, kazini nako amekuwa mtoro mtoro keshapewa Warning kama 2 bado 1 afukuzwe Bsi akawa kama amechanganyikiwa Selina wa watu! Kufika kwa Mzungu hayupi, kesharudi kwao, sasa afanyaje?! Akapiga akili ya mwisho akiwa hotelini alipopanga!
Akajiambia nafsi yake, nijiuze au niwe jambazi? Maana high life imenifanya niwe addict! Hapa kuna mawili tu au naweza fanya yote! Akachora ramani wee akaona hapa ndio hapa akaanza kutega mingo yake, hooker by night, teacher by day, anajiuza kwenye ma strip club makubwa makubwa anapata angalau ka hela, maisha yakaenda anafanya kwa siri kwa muda wa miezi 3 akadunduliza akapata hela ya kurent nyumba ya kawaida, akatoka hotelini maisha yakawa yanasogea!

Soya na mitikasi yake ya kupata ile video kwa kumewe. Siku ya kwanza kamtegea mumewe akabambwa, siku ya pili kamwekea mumewe dawa ya usingizi akakuta simu haipo kaacha ofisini, funguo wa ofisini hajauona. Asbh mumewe kaamka saa 5 anashangaa imekuwaje! Akaanza kugombana na mkewake umeniwekea nini kwenye chakula mbona nimechelewa sana kuamka. Magomvi na wewe kipofu anaskiliza movie bila kulipia! Si ujaua tena vile vidude alichomeka chumbani kwao, wakawa wanamwona anavaa kitu kama hearing maskioni wakimwuliza anasema anaskiliza mziki kwenye simu!

Soya akatoka bila bila kupata ile video akarudi kwa manoa! Akamweleza kila kitu manoa akashtuka sana we mwanamke me nikifungwa itakuaje dah hapa kijijini sio pangu tena itabidi nihame kama mke alivyohama, nihamie lusaka kwa muda mpaka hasira ya ismail itakapoisha! Akamfukuza Soya ondoka tu mama tusijekamatwa tena hapa. Akampigia simu mtoto wake Luwi kuwa anaenda mjini kusalimia atakaa miezi 2 na kwa Hachikoko miezi 3! Luwi akajiambia tobaa sasa mzee namweka wapi?

Luwi ni mtoto wa Manoa na Rasheeda. Anaishi Lusaka na familia yake. Ndoa sio muzuri saaana baada ya mke wake kumfumania na Evelyne hotelini wanakula ubwabwa na maharage. Ugomvi na wewe yakaisha ila mkewe akawa hamwamini sana mumewe akamfukuza mume chumbani awe analala guest room, mume akakataa akamwacha akawa anamnyima unyumba! Luwi akaona isiwe shida, kila siku analala kwa mke wake lakini Evelyne analiwa kila siku! Akampangishia nyumba Evelyne karibu na mtaa wao, majirani kama kawa wakaja kumweleza mke wake. Mke akasubiri luwi ameshaenda kwa Evelyne, akamfuata na panga, ilo vurumai lililokuwa hapo Love and Hip Hop hollywood hawaoni ndani! Ngumi na wewe, evelyne akakatwa kucha za miguu, akachanwa paja, mume akaingilia kati akapiga panga la kibwa kwa kitako akavimba, ugomvi na wewe majirani wakajaa mapolisi nao hao, wakapelekwa polisi mke akataka kufungwa mume akawaambia polisi kuwa amesamehe akaachiwa. Mke kurudi nyumbani anataka talaka Luwi hataki kutoa! Maana kuna watoto pake na Luwi anawapenda watoto wke maisha! Evelyne akakasirika akarudi kwao Buki na Faso kupumzika, maana lile sakata sio la kitoto. Luwi akamdanganya mke wake kuwa ameachana na Evelyne akamwonyesha msg kuwa ameshaenda kwao, mke akasamehe mume akarudi nyumbani ila no unyumba! Luwi anawa mvumilivu kibishi miezi 3 hajaona mwanamke akawa anajipiga punyetoo usiku akilala na picha za Evelyne! Kha! Kweli WaZambia Noumer!
Ndio majirani kuongea ongea rafiki wa Rasheeda akasikia akamwambia mama yake! Mama yake akashukuru kwa Umbea lakini hakumwambia mwanae yeye kama mama anasubiri aletewe ubuyu.
Luwi akampigia simu Evelyne rudi tafadhali Eve akakataa! Akamsihi akakataa akazusha safari ya kikazi akamfuata Evelyne mpaka kwao, basi kiiila siku wanapugana miti! Anamoa hela Eve akanogewa na Bushelele! Wiki 2 kama honeymoon! Luwi akamwomba arudi Lusaka, atamtaftia nyumba nzuuuri ya kuishi awe mke wake mdogo mpaka hapo atakapotengana na mkewake! Evelyne akasita Luwi akamhakikishia kuwa hatokutana na yela matatizo tena! Eve akakubali akaanza kudemand antaftie kazi gari na nyumba nzuri, Luwi akakubali anamwambia acha niende nikakuandalie makao! Makao yalipokamilika akamwita Evelyne akaja. Eve akapangiwa nyumba Mass Media, pazuri kimtindo! Akapewa na gari Rav 4, akataftiwa kazi Real Estate akawa anaenda kazini anarudi lakini kuonana na Luwi ikawa mara chache sana! Na yeye Evelyne ana needs zake ujue, alipokutana na Musa akishukuru akaona akomae pale pale, lakini Luwi kama shetani guu moja akipata tu mwanaume anatokeza huyo! Akawa hana la kufanya maskini.

Baba mtu Manoa hajua A wala Z yeye kajipigia simu nakuja nakuja nakuja! Nitumie nauli nakuja unipokee nakuja, hela ikatumwa akatua Lusaka kwa mwanae Luwi akakaribishwa akajaaa hapo asubuhi kwa asubuhi akisogea sana kaenda kunyoosha miguu, anarudi ndani, mke akitoka kazini kupikia familia yote maana maids haruhusiwi kupika na halali ndani watoto mmoja yupo day mmoja boarding basi manoa miguu juu na tv tu! Na hivi nyumba ina a/c nzuuuri garden kubwa basi anakaa hapo wee mwanae akija wanaongea wee hadithi zaisha sikumoja akamwambia kuwa mama yake amempa talaka! Luwi anashangaa. Akamwambia mama yako yupo mjini hapa sijui kafichwa na nani?!embu mcheki akampa namba. MANOA Akamwuliza kuhusu dadake maringo, akamwambia yupo tu yupo alipata kazi bank sijamwona nina mwezi kama kweli mama yupo watakuwa wameshaonana na maringo. Manoa akadai apewe namba ya Maringo akapewa! Akampigia mwanae, si unajua akina baba na watoto wa kike, Maringo akafurahi Baba uje uishi kwangu basi upafaham nitakupeleka na kwa mama nikuzungushe me nipo likizo. Baba akasema Yes hapa ndio hapa! Wakakubaliana weekend aje amchukue. Maringo akaja siku 1 kabla ya weekend akashinda kwa kaka yake mpaka aliporudi wifi yake na kakake wakaaga akamchukua babake ndani ya V8, Luwi anamshangaa Maringo imekuwaje tena? Anamwuliza umepata wapi gari, Maringo anamwambia tena nina wiki 1 naanza kazi UN ndio nataka nizurure na baba alafu namrudisha wakaaga pale wakaondoka wifi (mke wa Luwi) akapumua!

Evelyne akatumiwa text na Musa wakawa wanachat pale na nini, wakati Luwi yupo kwa mke wake na akajua leo haji, Musa akamkaribisha Evelyne kwake Eve akaenda! Kufika wale walikuwa washapendana! Wakaanza kupandiana, wanagandana, dyu dyu duduni! Miti mitini! MUSA anaona kama muujiza! Tena bila kinga!? Akakazana kupiga miti Eve hoi, kweli serengeti boys noumer! Luwi hakuona ndani kwa Musa! Evelyne akampenda Musa bure ikawa ndio michezo yao Luwi akiwa kwa mkewe Eve anaenda kwa Musa, au wanakutana hotelini

Ikawa jioni ikawa usiku ikawa asubuhi siku ya j2

ITAENDELEA SAA 11 JIONI
 
Hii hatari zaidi ya salama,familia yote ipo town,mbaya zaidi wote wazee wa kutembeza papuchi na dudu,mchezo ndo kwanza unaanza,big up penny
 
Soya ameachwa na mumewe Ismail na kwenda kwa Masoud anaogopa maana anajua muda wowote atapigwa mguu wa kuku ( atapigwa bastola). Akaamua kijituliza na mwanae wa hiari Betty! Akawa anapika ontime, anafua anafanya usafi anaongea vizuri na Betty! Mambo yanaenda Betty anashangaa mamwenye nyumba vepee?! Ismail akajua mkewe amebadilika aka doubt akijua tu manoa akirudi mambo bam bam asijue hata Masoud anamla mkewe! Kirui!

J2 Maringo na Baba yake Manoa wakaingia church, mama yake akaja anaendeshwa na deteva wa Patric ambae wana siri na mke wa Patric! Akasubiriwa mpaka ibada imeisha! Akaends kumsalimia Mtalaka wake,
Rasheeda: umekuja kunifuata huku umeona kijiji kilivyo shida kile ee?
Manoa: ah wapi me nimekuja kupumzika kilimo kikianza naondoka!
Rasheeda: hamna cha kilimo wala nini! Maringo utaniambia ataondoka baada ya mwaka, kwanza ulivyokondeana usijemtesa na kumnyonya Maringo na kaka zake uote kitambi ndani ya wiki mbili kama wewe mwanaume panga nyumba au nunua ukae!
Manoa: ah we mwanamke sasa naelewa kwanini tuliachana upo controlling kama mwanaume basi jioe. Yule bwege ndio anakunesa nesa kama kitenesi kwenye lile kioo?
Rasheeda: inaitwa Discovery 3 Darling! Labda tukupe lift umwache mtoto akazurure!
Manoa: akacheeeka! Haki ya nani kweli mwehu kawezwa! Discovery 4?! Aya mama me nasubiri kukuzika kijijini kuna sehemu yako utakuja unaumwa tuone kama utapendwa milele
Rasheeda: sikulaumu haukujua thamani yangu ukaanza kutembea na kila mtu kijijini mpaka Soya! Ngoja niende mimi na maneno yako yashindwe kwa Damu ya Yesu! Akaondoka mawowowo yanacheza kama magodoro dodoma
Manoa akawa anaiangalia chura ya miaka yote ikiingia kwenye kitenesi, Discovery 4!

Maringo akaenda kumsalimia Oga, wakawa wanaongea pale wakati wazazi wake wanaongea walipomaliza akamuaga tutaonana akaondoka na baba yake. Njiani anamwuliza baba yake mnarudiana lini na Mama?! Manoa akajibu akirudi Yesu labda! Kama Yesu hatorudi basi tena tutarudisha hesabu Mbinguni!

Maringo akamwangalia baba yake akajua ka mind ile divorce hakuielewa elewa akaamua asiingilie kwa maswali kujua kwanini waliachana lakini roho ikakataa
Maringo: ilikuaje mkatalakiana na mama Baba? Mbona me nimeshachanganyikiwa?!
Manoa: mama yako tangu nimuoe anapenda high life na mimi nikashindwa kumpatia uzeeni kwasababu nilifukuzwa kazi! Na sikuajiriwa kwengine kokote nikaamua kurudi kijijini nikisingizia naumwa natakiwa kukaa kijijini bila stress nikakuacha uishi na Luwi na Hachikoko! Sina cha kufanya zaidi ya kumwachia Mungu afanye yake sina nguvu tena ya kumlazimisha mama yako abaki na mimi. Itabidi watoto mzoee tu!
Maringo akamwangalia baba yake kwa huzuni na uchungu anajisemea moyoni sasa baba atarudije kukaa mwenyewe kijijini lazima akae hapa nikianza kazi UN namnunulia nyumba abaki hapa kule kijijini tunapangisha awe anaenda kufanya kilimo hapa na pale! Akamwambia baba usijali me nitaongea na mama mrudiane, ikishindikana basi utabaki hapa hapa mjini nitakutaftia nyumba uishi uwe unaenda kule kuangalia kilimo ila kuanzia leo unakaa na mimi mpaka utakapopata nyumba yako
Manoa akafurahi sana, akajikausha hapana mwanangu usihangaike. Maringo akamwambia hapana baba kule utakufa kwa pombe za vilabu na stress nitaongea na kaka zangu tukuchangie upate nyumba. Manoa akanyamaza alafu akajibu nashukuru Mwanangu, moyoni anashangilia Ismail na Masoud hawatamwona tena! Kweli zali la mentali, mapenzi ya baba kwa mtoto wake wa kike hayana mpinzani. Wakaelekea hotelini kula lunch Maringo so proud na baba yake baada ya hapo akamwambia tikitoka hapa tunaenda kukutaftia viwalo hivi hapana na saloon nakupeleka wakupake zaazoo au easy black baba yangu upendeze! Uwe wa mjini. Kwakweli kwa Manoa ilikuwa ni ndoto akashukuru Mungu akubariki sana mwanangu usipungue hata 100.Maringo anacheka tu!

Kungwi akamtext Drogba! Drogba akatia timu kwa Kungwi, Drogba anashangaa mama huyu ana nyumba mzuri kweli, kwao lugha yao ni moja tu, leta mechi or go home! Mapenzi baadae hapa mechi tu!
Mechi ikapigwa hapo weee j2 kama siku ya dhambi, Kungwi alipokaa sana wakaagana na Drogba! Drogba anashangaa huyu mama jini nini mbona kila siku nafungwa kiboya boya?! Akitaka kuuliza anashindwa maana makubaliano yao ni mechi tu hakuna cha umekula umekunywa umelala umejamba umekunya! Hapo dyu dyu tuu!

Selina na shughuli za Stripping! Siku wametoka out Oga na Drogba, Drogba analalamika kapata jimama linamtoa knock out hamwelewi nu binadamu au jini?! Akawa analalamika pale Oga anameambia achana nae kama haumwezi utaanza kujiona duni na kujichukia wale watu wa zima washaona mengi appreciate her talent na adapt or go home and drop dead!
Kiru Drigba akachoka akakubaliana na ushauri wa Oga! Mara anamwona Selina anacheza kwenye ringi huku anatupiwa hela akamwuliza Oga isnt it that Sellina?! Kuangalia tobaa ni yeye akaensa kumsalimia akaomba aongee nae selina akakataa. Oga akamwambia nitakulipa akakataa. Akaenda kuongea na meneja wake akamwambia nakulipa dola 2000 namwona selina kwa nusu saa tu, Meneja akamwambia hata ukimtaka siku nzima ni wako! Oga akalipa pale akaenda kuitwa selina kavimba kweli kweli anamkemea bwana unanikosesha wateja shift yangu hii!
Oga: nimeshainunua meneja anampandisha mwengine njoo tuongee akamvuta wakaenda kuongea na kaka yake Drogba! Stori stori na wewe Maswali kibao
Selina akawa anamjibu tu Only God can Judge me and He Seems Quiet Impressed! Wakawa hawaelewi amechanganyikiwa au?!
Selina: kama umemaliza niende home nikalale au bado unataka kunilala?!
Oga akamwambia aache iyo kazi sio nzuri kabisa, sio kwamba nataka kurudiana na wewe hapana lakini sio kwa kazi hii
Selina: akarudia kauli yake maana alikuwa haongei kabisaa Only God can Judge me and He Seems Quiet Impressed
Eh wakamuacha wakijua labda hazimo kidogo akaondoka kwenda kuchukua begi lake meneja akamlipa dola 1000 akaondoka amefurahi kweli kweli
Oga na Drogba wakawa wanashangaa wanaongea jinsi ta kumsaidia selina! Drogba akamwuliza Oga are you sure haumpendi tena Selina mrudiane? Oga akasema hata uniue upendo kwa Selina ulishafutika kabisaa me namsaidia kibinaadam tu basi!

Manoa ndani ya barber shop anapata transformation! Maringo akapigiwa simu na Patric kuwa anataka waonane!
Maringo: leo sitaweza mpenzi, nipo na baba yangu mzazi ngoja kwanza nimseti nitakufuata, hata kesho ndio kwanza katoka kijijini! Hapa natoka kumchukua stendi ya bus acha nikutafute mimi usije kwetu huku Roma maana naishi nae!
Patric akachoka maini maana alimtamani Maringo mbayaa! Akaamua kubaki na nyege zake kwa mke wake Mary, huduma ya ndoa kwenye ndoa yao ilifungwa 5yrs ago Mary hamtaki Patric na Patric hamtaki Mary! Basi akajifunika shuka akalala!

Bank meneja akamtext Maringo
Bank Manager: mambo?!
Maringo: poa bods
Bank Manager: naweza kukuona?!
Maringo: hapana. Kuna tatizo lolote kwani?
Bank Manager: hapana! Nilitaka tuongee tu binafsi
Maringo: nitakutafuta boss ake! Leo nimetingwa na mambo ya kifamilia! G9t

Pendo na Caroline ndani ya mjengo mara baba Joseph huyoo ndani ya mjengo! Caroline akafurahi Daddy Daddy umerudi! Babake shhh! Yupo wapi Pendo?!
Caroline: amelala chumbani. Wakawa wanaongea baadae mtoto akalala, akamfuata Pendi chumbani akamkuta kalala fofofo akaingia kuoga akarudi kumwangalia pendo fofofo akawa anamwangalia hammalizi, alfajiri Pendi akashtuka kuangalia anamwona Joseph amelala, akafurahi akaanza kumchokoza! Uchokozi uchokozi na wewe! Mechi ya ukaribisho ikapigwa wanaifungua kwa eary morning sex also known as Champaigne! Kuja kukaa sawa Caroline anaondoka anaenda zake shule school bus imekuja! Joseph akawa anamshukuru Pendo kwa kumtunza na kumwangalia mtoto wake yupo kwenye hali nzuri tena kanenepa kidogo! Ikampandisha minyege Joseph na kuongeza mapenzi kwake! Baada ya chai wakachapana cha mezani, Pendo maipwiru yote yakaisha! Josepg akatoa pete akapiga magoti anamwuliza Pendo will you Marry me?
Pendo macho yanamtoka, haelewi anamwangalua Joseph kama Bundi! JOSEPH akamsukuma wewe amka acha kuota me naumia huku magotini, Pendi akaanza kulia, haelewi ndoa na mechi wapi na wapi!
Akajibu aliopaswa kujibu Yes i will Marry you! Akawa kama amepata mshtuko! Kha! Haamini maskini wa Mungu, wote wakiwa uchi na hakuna mwenzake aliemwonea aibu mwenzie, kama bustani ya Eden vilee! Uuuuwiiii!
Zambia Mojaaaaaa! Oyoooooooooo!

Ikawa Asubuhi Ikawa Mchana siku ya 3

Itaendelea Kesho saa 5 asubuhi
 
hahahaaaa majibu ya rasheeda kwa mtalaka wake manoa ni sheeeda,

mwanamke uyu sijapata kuona, eti kama wewe ni mwanaume panga nyumba hahahaaa ka namuona vile anavomshushua manoa jamani na ile hali yake ya ukijijini
 
hahahaaaa majibu ya rasheeda kwa mtalaka wake manoa ni sheeeda,

mwanamke uyu sijapata kuona, eti kama wewe ni mwanaume panga nyumba hahahaaa ka namuona vile anavomshushua manoa jamani na ile hali yake ya ukijijini

Ni sheedah!
 
Selina akashukuru Mungu, dola 1000 sio ya kitoto hata akinengua wiki nzima hapigi dola 1000. Akasnza kupiga akili atafute nyumba apange maana sio kwa kukaa kule

Akahangaika na nyumba akaipata, akalipa kodi ya miezi 7 huku anajitafuta. Asubuhi anaenda kufundisha usiku stripping! Maisha yakawa yanaenda ivo ivo buzy na mambo yake. Yeye na pendo hawawasiliani hata kidogo!

Pendo yupo engaged! Haaamini wala hajawahi kuota! Kwanza alijua hatoolewa, miaka 37 hana mtoto hana bwana huyo Jose tangu ampate ana mwaka tu. Akachukua simu ampigie mama yake akaona haitanoga mama akapokea akamwambia nakuja huko mchana naona Jose ameenda ofisini! Akajiandaa kwa mama mojaa!
Mama akafika anasubiri aambiwe ubuyu Pendo akamwonyesha kidole mama wooooow jaman mwanangu akamkumbatia eee bora na mie niozeshe uuuuwi jamaani Mungu asaaante jamani nimefunda wengi na mie mwanangu namtoa kimasomaso mara anapanga harusi ifanyike wapi mara hivi mara vile eh mama mbona hata hatujapanga tarehe za harusi afu yule ujue ni mjane sidhani kama atataka mambo makuuuubwa simple tu church watu 10
Kungwi: watu 10?! Hapana labda harusi ila sendoff lazima nitikise kijiji!
Pendo akakosa pozi! Kha! Hapa kazi ipo akamkubalia tu sawa mama hii ni show yako ila kitchen pati wala staki
Kungwi: nini?!hapana asee kpati lazima nifanye kijijini yani ya nguvu kubwaa!
Pendo anazidi kuchooka
Kungwi: kwani unajua kila kitu kuhusu ndoa mwanangu?! Staki aibu mie, unaolewa unarudishwa baada ya siku ya 3! Hapana asee!
Pendo akawa mpole kama jongoo akasema sawa tutakwambia tarehe ya harusi na siku ya mahari sasa hivi siwezi hata kuuliza itakuwa mapema saana. Eh kungwi kafurahije sasa anaozesha anapiga mahesabu nani wa kumfunda mwanangu maana mtoto anauma sio kitoto! Akaona ampeleke kwa Rasheeda kubwa la maadui wake, mkali wake, mjanja wake

Manoa keshakuwa supa wa mjini mjini! Kapendeza Maringo kampendezesha ukimwona utadhania pedeshee. Maringo akaitisha family meeting kwake bila mama yake. Wakaja kaka zake Hachikoko na Luwi! Wakakaa wanne na baba yao!
Maringo akawaambia baba kule kijijini ameshatengana na mama, akikaa kule atakufa lazima tumlete hapa! Lazima apangiwe hapa, atafutiwe kibarua, kodi ya miaka 2 tunailipa sisi, misosi sisi, usafiri sisi, kwa ufupi pocket money ni sisi!
Kaka zake wanamwangalia baba yake kabadilika kawa handsome kweli, wakawa wanashangaa ivi Maringo hii nyumba unamiliki vipi na hilo gari wakauliza kakaz!
Maringo: hayo baadae kwa sasa twamtaka baba apate nyumba awe na uhuru wake sio vizuri mtoto wa kike kuishi na baba yake tuu!
Kakaz wakakubali wakapiga mahesabu yote wakaja kugawa kwa 3, kila mtu akarnda kutafuta hela yake, ndani ya siku 3 baba kapangiwa nyumba Leopard Hills huki mashambani wakamwekea na ng'ombe na mbuzi awe anachunga, wakamtengea kasehemu analima hapo! Akafurahi mwenyewe ingawa sio karibu na home. Kila weekend wanapeana zamu ya kwenda kumwona baba yao, wanaenda na wajukuu wanaenda alone wanaenda kama picnic sikunyingine wanamwalika mama yao Rasheeda aje anakataa ah basi tu maisha yanaenda, Manoa kawa wa mujini, akanunuliwa na gari Rav 4 awe anazinguka zunguka
Manoa akajiongeza akawa anafuga na kuku akazungukia supply hapo mjini mahotelini na kwenye nyumba za watu akapata tenda ya mayai, kuku, ng'ombe akakaa sawa.
Kijijini akaweka mtu mashambani akivuna mavuno anakuja kuuza mjini anapata hela, nyumba ya kijijini akapangisha

Siku moja anatoka kwenye mizunguko yake akakutana na kungwi anatembea barabarani akamfuata na Rav 4 yake, nakuona mrembo umevamia jiji la Lusaka, Kungwi kumwangalia haamini! OMG! Manoa?! Kha! We manoa wewe umekuwaje?! Umekuwa handsome katoto?na gari unaendesha?! Kweli dunia duara!
Manoa: nipo baby naishi Leopard Hills nikupeleke kwangu ukapaone. Wewe unaishi wapi?
Kungwi: naishi hapo mbele nipe lift nikakuonyeshe akapewa lift wakaondoka huku wana catch up ya kijijini mpaka mjini. Kufika kwa Kungwi Manoa anashangaa mbona anaishi pazuri, Kungwi akamwambia hapa kwa mwanangu pendo ameniachia nikae yeye aneshachumbiwa anaishi na bwana wake si unajua tena haya mambo ya mjini me nimemkataza amekataa yani aibu tupu
Manoa: hongera sana Kungwi kwa kupata mkwe
Kungwi: asante hapa nasubiri mahari nirudi zangu kijijini!
Manoa: ok sawa hongera sana nyumba nzuri sana. Wakawa wanaongea pale masaa kibao kushtuka saa 11 jioni manoa akaaga. Me naenda kwangu mbali, Kungwi akamwambia karibu tena si ushapajua hamna neno
Manoa: asante, karibu na wewe kwangu hata leo twaeeza kwenda kesho nikakurudisha
Kungwi kuambiwa hivyo kama amewashwa mota chini! Akapaki fasta fasta utadhani anaenda mkoa wakaondoka wote mpaka kwa manoa anatoa tu macho palivyo pazuri kuliko kwake. Anamwuliza Manoa ivi inafanya shughuli gani?! Manoa anamwambia ufugaji na kilimo kidogo tu

Maringo akaanza kazi UN kila mtu anamshangaa lile body tinga tinga! Maringo nae yupo noma kwenye kazi sio kitoto, anapiga mzigo hatari! She is a very hard working girl, akapata msg kwa Bank manager: bebi umenitupa kabisa! Tangu uniahidi haujatokea!
Maringo: usijali jioni basi ntakucheki love!
Bank manager akajaa midadi kisa kaitwa love
Usiku Patric akatia timu kwa mara ya kwanza kwa Maringo, eh! MAaringo kapiga hot pants patric akachoka zaidi, hamba cha maongezi wala nini akamvamia maringo wa watu, piga miti miti na wewe, du! Patric weeee! MUNGU anakuona! Yani anachanganya mama na mtoto, kweli wanaume wengine ni wagonjwa waliotoroka milembe!

Joe bado yupi Hospital, Kandi akajipa kibarua cha kila siku kwenda kumwona ex wake maana hakuwa na msaada mwengine zaidi ya wazazi na ex wake! Joe akaanza kupata relief, akimwona Kandi na wazazi wake anawatambua wote, akaanza mazoezi ya therapy kidogo kidogo Kandi yupi benet anamsaidia keshamsahau Drogba akipigiwa hapokei simu hajibu sms Drogba akapotezea akawa amebakia na Kungwi tena kungwi mwenyewe mpaka amwite basi taabu tupu! Mary na Neema hawamcheki tena akajiona ana gundu, akawa yupo buzy na kazi basi

Siku moja akafunga safari kwenda kwenye strip club! Akiwa amejaa minyege akamkuta selina, anapiga mipombe huku anamwangalia selina! Eh si akaenda kumlipia! Akalipa dola 500, kweli Nigerians wana mawe hatarious! Selina kuitwa kumbe Drigba akagoma akamwambia meneja mrudishie hela yake huyu shemeji yangu meneja kurudisha hela akakataliwa akaambiwa hapokei aongee na selina mpaka akubali
Selina akamwuliza meneja kwani kalipa ngapu akajibu dola 500 yako 250. Selina akiangalia anaitaka na shida zake kem kem akakubali!
Drogba akambeba mpaka chumba cha ndani akala mzigo! Selina roho inamuuma dah kweli kazi ya uchangudoa tuwaachie wazoefu sie tunaojaribu dhamira zetu hazijafa ni sheedah! Akavumilia ivo ivo mpaka Drogba akamaliza akaondoka zake kurudi home.

Zikapita siku 2 Selina akiwa ofisini anaendelea na shughuli zake kama kawaida akaja kuitwa Selina una mgeni wako, selina akaguna akatoka! Kuangalia ni Drogba! Tobaaa kasahau nini tena huyu mwanaume? Dyu dyu lake au?! Akaenda kumsikiliza kwa aibu reception
Selina: nambie Drogba! Kuna kitu umesahau au umekuja kufuata chenji maana me sikulipwa hela jana niliikataa
Drogba: sahau kuhusu hela, nataka kuongea na wewe!
Selina: nambie lunch yangu inaisha after 1 hr
Drogba: naomba tuongelee kwenye gari, wakatoka kwenda kwenye gari Selina akawa anajua anaenda kuliwa
Drogba: selina unajua sijapenda kaka yangu alivyokufanyia! Me sijafurahi kabisa lakini nimekaa siku 2 hivi nimeshindwa nimeona nije kukwambia kuwa me nakupenda sana naona uwe mpenzi wangu!
Selina: tobaa! Hii ya leo kali sasa napigwa mpira toka kwa kaka mtu mpaka mdogo mtu, we Drogba ni mkichaa au?! Unataka kuniletea aibu me kwenu?! Oga akijua itakuwaje?!
Drogba: ah haijalishi bwana me nimekupenda kikwelii sio kwasababu umenipa mechi kali wala nini hapana ni kwasababu tu nakupenda!
Selina: haya nimekusikia
Drogba: naomba namba yako
Selina: sina simu
Drogba: naomba nije kukuchukua baada ya kazi nikupe lift mpaka kwako
Selina: hapana me sina nyumba nalala tu kule kazini naamkia hapa nikitoka kazini hapa sina nyumba
Drogba: dah! Selina jaman, naomba unieleer
Selina: na wewe naomba unielewe nipo kazini lunch inaisha baada ya nusu saa hata sijala hapa
Drogba: unatoka kazini saa ngapi?!
Selina: saa 10
Drogba: naomba basi niambie muda wako wa kutoka wa kikwelii
Selina: eh na wewe! Saa 11 jioni
Drogba: saa 11 nipo hapa!.
Selina: sawa kwaheri akawa anataka kufungua mlango Drogba akamzuia! Akatoa pochi akampa dola 200 hii utakula leo, Selina akaipokea kama ni last money yake! Akashuka akamwambia asante akaondoka!
Drobga anamwangalia tu anavyoondoka na yeye akaondoka. Saa 10 Drobga yupo getini, Selina hajatoka akakaa kumsubiria mpaka saa 11 akatoka akamfuata, nimekuja mpenzi kukuchukua, walimu wenzake wanamshangaa mpenzi wa Selina hawajawahi ona selina anakuja chukuliwa na mwanaume kwenye gari nzuri kama ile. Drogba uongo dhambi alikuwa na gari kali.
Selina akameza mate akamfuata, yani Drogba hatuelewani mbona unanifanyia vurugu lakini?! Drogba akamshika selina kwa nguvu akambusu mdomoni, walimu wenzake wanachukua selfie na video, Selina akajichomoa kwa Drogba akamchapa kibao, niache akaondoka. Drogba anamfuata nyuma anamkimbilia walimu wenzake wanashangaa hili la leo picha la kihindi! Nehi nehi chori chori acha acha! Kuchi kuchi hotaee!

Wakatembea wee maili moja selina mbele Drogba nyuma Selina anajiuliza kwani leo Drogba kapatwa na nini jamaa! Au ana mapepo?! Akawa haelewi Drogba akamkimbilia selina akampata akamshika akamnyanyua juu akambeba, Selina mwenyewe mwembamba na Drogba kajazia miraba 4 Selina anampigapiga mangumi kwenye mikono Drogba niachieeee! Nakwambia niachiee! Drogba anazidisha mwenda mara akimbie mara atembee wakafika kwenye gari yake akafungua akamtupa nyuma ya seat selina akafunga gari akapumua.

Baada ya dk 10 Drogba akaingia kwenye gari Selina anamwambia Drogba tafadhali naomba niache niende kazini me sina kipato kingine zaidi ya hii kazi yangu tafadhali, niache abeg!

Drogba akanywa maji kwanza, akamwambia nakupeleka kazini kwako under one condition. Iyo kazi unaacha! Kuanzia leo haufanyi iyo kazi! Selika akabakia mdomo wazi kizungu mkuti haelewi!
Selina: Drogba haya ni maisha yangu unataja nikale polisi au?! Huku Drogba anaendesha gari!
Drogba akamwambia hapo nyuma kuna mfuko uchukue ufungue uangalie kuna zawadi yako, selina kuangalia kumbe simu! Akaambiwa aiwashe akaiwasha ina line iliosajiliwa,
Drogba: hio simu na laini vyote ni vyako! Akaambiwa aangalie ndani ya Boxi akakuta risiti ya nyumba imelipiwa kodi miaka 2! Selina alipochoka zaidi eneo alilolipiwa sasa ndio alipochoka, nyumba kapangishiwa Mass Media Lusaka! Kha! Kwa wazungu na wenye hela zao me mbona naona kama naota anajiambia moyoni! Wakawa wanakaribia ofisini kwa Selina, Selina haamini analia tu kwani kuna nini Mungu mbona unanijaribu namna hii anajiongelesha moyoni anashangaa kuna nini simu ya maana iphone sijui hata kama anajua kuitumia!
Kufika Drogba anamwambia unataka kwenda au unaacha kazo hapa hapa nambie mapema nikiondoka sirudi tena!
Ukiacha kazi nitakutaftia kazi ya kufanya sio hii kama unataka kazi 2 sawa kama unataka vinginevyo sawa kafikirie unaifute kwangu, akamuelekeza, hela hizi hapa dola 1000 za kwako za kuanza maisha, kwaheri!
Selina akashuka anashangaa Drogba kawaje ana mapepo au akaenda zake ndani
Baada ta masaa 4 Drogba amekaa nyumbani kwake anaangalia Tv anamuwaza Selina, kampenda kweli kweli, mara anaskia hodi akainuka kwenda kufungua ni Selina!
Selina akamwambia Ok let's give it a try! Drogba akafurahi akamkumbatia

ITAENDELEA SAA 12 JIONI
 
Back
Top Bottom