My cup runeth over ~ Na Kikombe changu kinafurika

My cup runeth over ~ Na Kikombe changu kinafurika

Usiku uliofuata OGa akamtext Maringo
Oga: mambo mrembo
Maringo: poa nani mwenzangu
Oga: aaah swahiba hata namba yangu haukusevu tena
Maringo: hapana kazi zilikuwa nyingi
Oga: ah basi me ni Oga wa ofsini
Maringo: ah mambo boss za mida
Oga: salama boss dogo sasa mpendwa wangu unaonaje tukatoka out nini?! Nikupeleke hata Fawty Towers au Avani Victoria falls resort
Maringo: sawa nashukuru ila kwa leo wala wiki hii hapana nipe muda wa kufikiria
Oga: asante kwa kukubali mrembo ngoja nijiandae we ushapata msosi usiku huu
Maringo: ndio asante usiku mwema
Akawa anayawaza na kuyawazua, yani Joe anatembea na Kandi, makubwa! Sasa nitafanya mimi kazi yenyewe nimetaftiwa na Joe, akili zote zikamwishia, akachukua simu akampigia mama yake
Maringo: shikamoo mama
Mama: marahaba mwanangu za mjini
Maringo: salama mama unakuja lini?!
Mama: me nipo mjini wiki ya 3 sasa
Maringo: hee! Na baba umemwacha wapi?!
Mama: yupo nyumbani nimekuja kupumzika huku
Maringo: eh umefikia wapi sasa au kwa Luwi au Hachokoko?!
Mama: hapana nimepanga tu nyumba akamwelekeza alipo akamwambia aende kumwona
Maringo: sawa mama nitakuja ijumaa nikitoka kazini naja kulala huko nina ma stress hapa hamna mfano
Mama: eh yapi tenaa?!
Maringo: Joe mama ana cheat na ex wake!
Mama: mh huyo Joe me hata simjui labda unielezee
Maringo: kama nilivyokwambia ndio nasonga mbele, ana ex wake pale ofisini last weekend sikumpata kumbe huyo ex alimfungia kwake
Mama: akacheka kama shetani pori, mwanangu na wewe! Sasa umeamuaje?!
Maringo: hata sijui maana yeye ndio kanitafutia kazi hapa nakaa yeye ndio kapanga yani hapa hela yangu inasimama yeye ndio kila kitu
Mama: sasa mama shida ipo wapi labda?!
Maringo: nampenda mama ameniumiza moyo wangu sio kitoto! Hapa nashinda kulia tu
Mama: pole mwanangu! Pole sana wanaume ndio walivyo, sasa itabidi uje tuongee ila kwa Joe usipunguze mapenzi kabisaa! Hata tone wala asishtuke kuwa umejua. Na huyo ex jaribu kukaa nae mbali kwanza mpaka utakapokuja akikuzoe nenda nae mdogo mdogo mpaka tutakapoongea!
Maringo: sawa mama nimekuelewa huku analia. Simu ikakatwa
Mama: akawa anajichekea tu, watoto bwana ila nashukuru wangu ameamua kuniganda akija nampa darasa huku na refer nala babake mzazi ili asinione muhuni, akaingia zake kulala
Lakini Maringo hakulala analiiia lia na wewe, Joe kweli wa kunifanyia mimi hivi?! Haya bwana maskini me sijui naenda wapi mie!
Simu ya Joe ikaingia hakupokea akaiangalia kama Tv. Ikapigwa 5 missed calls na sms 10 hakujibu hata 1. Baadae akaona simu ingine inapigwa akajua joe kabadilisha namba hakuipokea
Akaendelea kujiandaa na kesho akapigiwa tena simu imeandikwa unknown! Mh akaamua kupikea haloo
Simu: habari mrembo
Maringo: salama nani mwenzangu!? Tumbo joto akijua ni Joe
Simu: me naitwa Patric
Maringo: ok me sikufahamu lakini
Patric: tutafahamiana tu hamna neno, napenda tuonane lunch kesho, unasemaje
Maringo: hapana haitawezekana nipo kazini
Patric: najua ndio maana nikakuomba
Maringo: lunch tunakulaga ofsini
Patric: hapana sio lazima hata kutoka unaruhusiwa, we niamini mimi kesho nakuja kukupitia na nawahi kukurudisha
Maringo: sawa ukifika nipigie nitatoka
Simu ikakatwa Maringo bado kabakia kichwa panzi kazama kwa Joe, akaingia zake kulala akamute sauti

Asubuhi kumepambazuka Selina akaenda kijijini na picha ya Jose aliiiba akaenda ndani ndani huko Ndola. Akafika kwa Mganga wake akamwelezea matatizo yake mganga akamwambia nipe mil 3. Akazitoa. Akamwambia sema unachokitaka. Akaanza kufunguka
Kuna bwana nimempenda ghafla, anaitwa Joseph,
Mganga akashtuka Joseph yupi?!
Selina: anafanya kazi Oil and Gas.
Mganga: mh yule nimeshaletewa picha yake na wadada 50 wanamtaka, yule jamaa ameokoka wala sitamuweza jaribu pengine na hela yako nenda nayo
Selina: mganga jaman mbona kwa mkuu wa mkoa umeweza na kwa Mnigeria Oga!
Mganga: haya tujaribu ila nikianza kazi sirudishi pesa
Selina: pesa makaratasi mganga we tupige kazi tu hapa
Mganga akafanya yake na nini akapewa dawa akaambiwa akatupe kitandani kwa Jose akiwa amelala usiku saa 6 juu ta alama ikipita dk 1 utamkosa. Dawa inatenguliwa muda kama huo huo ulioweka dawa
Selina: saw mganga
Mganga: ikishindikana jaribu kwengine me nitakuwa nimeshindwa. Wale wengine hawana ulinzi wa Mungu lakini joseph anao mkubwa sana siuwezi labda ujaribu vijiji vya Mpika au Chima au Chingola au Livingstone
Selina: sawa mnganga akachukua dawa akaondoka, njiani anasema lazima show niicheze kininja akawa ana plan pale jinsi ya umpata Jose.

Jose akafika nyumbani kwake akamwita Pendo aje, mtoto alikuwa amelala akamficha chumbani kwake, anataka apate maelezo amejuanaje na Masoud!
Pendo: jamani mpenzi hausahau tu si yameisha
Joseph: akiwa amefura nambie bwans si uliniahidi mwenyewe
Pendo: mmh sasa mpaka ukasirike mpenzi?
Jose: ah bwans mbona unazunguka kwani kuna nini na huyu babu?
Pendo: eh amekuwa tena babu?! Wakati yupo handsome kinyama
Jose: eh handsome tena?!haya bwans akajifunika shuka analala
Pendo: jamani mpenzi wangu usifanye ivyo jaman akawa anampetipeti anamchumu Jose nafura
Akamwinua juu akamweka kwenye mapaja yake
Pendo: unajua mimi nina mazazi mmoja, baba yangu alifariki wakati nipo darada la 5. Alikuwa mkristo, mama yangu baada ya miaka 3 akapata bwana akaolewa wa kiislam ndio huyu Mzee Masoud!
Jose: akainuka kwenye mapaja ya pendo?! Acha basi mzaha pendo
Pendo: sasa me nikwambie mzaha gani au unataka nimpigie maza asbh uongee nae? Mbona unanifanyia vituko ivyo leo una nini!?
Jose: akanyamaza kwa muda akamwambia basi yameisha mpenzi nakuamini
Pendo: na wewr umemjuaje Masoud baba yangu wa kambo!?
Jose: ah alikuja tu ofisini ni rafiki wa boss wetu, akikumbuka tishio la mzee masoud kuwa akisema imekula kwake
Pendo: ok basi hamna neno si unaona tunaongea vizuri yanaisha afu na wewe mambo ya kupaniki kha!
Jose: si unajua nakupenda baby sasa nikikukuta na mapedeshee ndio Nachoka si unajua kwako me mazima mazima na wala sina wengine zaidi yako akampetipeti Pale ligi ikapigwa ya kibishi!

Asubuhi Kungwi akafika Lusaka, akampigia Pendo, mwanangu upo wapi mbona napiga hodi sikupati?!
Pendo: anajiandaa fasta fasta nakuja mama nipe dk20 nipo hapo nilienda sokoni akamuaga Jose akakimbia alfajiri saa 12, mama amekuja amesubiri sana ngoja niwahi akakimbia
Kufika wakasalimiana na mama yake akamkaribisha ndani
Kungwi: yani umeniweka hatari!
Pendo: pole mama karibu sana akamkaribisha pale kampikia chai wakaanza kuongea
Pendo: mama umemwacha wapi mzee mwenzio!? Mbona uko hapa?!
Kungwi: babako mdogo si yupo hapa Ludaka hajakwambia?!
Pendo: hapana wala sijaongea nae (akadanganya)
Ila jana nilienda kumsalimia rafkiangu tukaonana hatukuongea saaana maana sikutaka rafkiangu ajue yule ni nani!?
Kungwi: wapi ulimwona?!
Pendo: kwenye ofisi moja uko mjini inahusika na mambo ya oil and gas
Kungwi: mh baba yako anamfahamu nani pale sa ajabu ameenda kuomba hela tu pale omba omba mkubwa ila na aombe tu, kama ataomba ili atuletee msosi huku nyumbani sawa tu
Pendo: akaguna mmmh!
Wakaendelea na maongezi yao palee na nini Pendo akamwambia mama yake, Mama unajua nipo na Mpenzi wangu anaitwa Joseph. Ni mjane mkewe alifariki akaacha mtoto m1 ananipenda sana mpaka mwenyewe roho yangu ina vibrate kupendwa kule
Kungwi: enhe hongera sana anafurahi mwanae amepata bwans soon ataozesha na yeye
Pendo: lakini mama kuna shogangu selina huyo ni mwisho wa matatizo anamtaka sana mchumba wangu na hivi hajui kuwa nipo nae juzi ananiambia atamfuatilia mpaka ampate, ila sijui bwana nafanyaje maana hata mtoto ananipenda anasema nimefanana na marehemu mama yake kwa kila kitu
Kungwi: tobaaa asalaaalaaa! Asta kafululahi rwahimu, ati nini? Mh akaguna tu. Mwanangu huyu selina sijui asali embu kaa nae mbali hapa hata roho yangu ime vibrate kwa huzuni, atakuibia mume kwa style ya uchawi hapa napoongea kama namwona kaenda kwa mganga na kapewa dawa aje amuwekee Joseph. Mama kama unasali we sali mpaka mwisho wako umwombe huyo Yesu sijui nani akuokolee naona kiza kingi usipopambana mama utakuja kunililia kijijini sitakuwa na msaada kwako
Pendo: sawa mama hata hapa kwangu hapafahamu anakujaga tu dukani
Kungwi: kwani tabia ya marafiki uliipata wapi me nakujua we msiri saana una fight kivyako sasa mzoga Selina umeuzoa wapi?!
Pendo: ah tulikutana tu huko wizarani tunafuatilia matokea akanigaaanda mpaka wa leo sijasoma nae wala nini basi tu
Kungwi: ngoja kwanza nitulie ntakufundisha ujanja
Pendo: sawa mama ngoja nijiandae kwenda kazini me nakuacha akaanza kumwelekeza nyumba na chakula na nini ukishindwa kitu nipigie ngoja niwahi kufungua duka. Akaondoka kwenda ofisini
Kungwi: mambo si ndio haya! Cheki jumba hili zuriii kha! Kweli Mungu si athumani kamlipia mwanangu na bonge la bwana maisha yanaenda

Kungwi akakaaa akaboreka akachukua simu akampigia Rasheeda. Uko wapi mami naskia ulikuja Lusaka
Rasheeda: nipo hapa Lusaka akataja mtaa kumbe ni jirani na kwake Rasheeda akamwambia basi nakuja hapo kwako napafahamu angalau tupige mawili matatu
Kungwi: haya karibu mzazi mwenzangu
Baada ya dk 10 Rasheeda akafika kwa kungwi wakapiga umbea kila mtu na yake!
Kungwi: sasa kupewa talaka tu ushaingia mjini
Rasheeda: ndio maanake na wewe imetalakiwa nini nyumba nzuri hivi unawezaje imudu yani Masoud kakufukuza kwa kitu gani na hapa kwa nani?!
Kungwi: hapa kwa bwana wangu m1 ivi wa mjini nikimmiss nakuja ananipa raha narudi kwangu. Enhe na wewe nani anakupa raha
Rasheeda: kitoto kim1 ivi kinasoma chuo kipo tempo hapo ofisi ya raisi ndo kimenifungia na nini wakaongea weee baadae Kungwi akamchota akili
Kungwi: ivi unajua Soya mke wa Ismail anatembea na mumeo?!
Rasheeda: hata sijui kitu jamani yule mama kumbe joka la kutupwa bora nimemuachia mzoga ule maana sio kwa ushenz alionifanyia manoa anatembea na kila mwanamke kijijini hata mwl mkuu wa shuleni kwako anatembea na manoa
Kungwi: akachoka eh hata boss wangu!? Kweli kazi ipo! Akachoka mwili na roho maana kwa Manoa alikuwa ameshafika na kuweka jamvi sass kuskia mwl mkuu tena akachoka mazima

ITAENDELEA SAA 5 ASUBUHI KESHO
 
Nice story! Though umejaribu kufanya kitu kimoja ambacho nafatilia kwa umakini if you will be able to pull it off. Umeenda out of the box kwa kuleta COMPLEX STORY. Story flani kama caliber ya Daniell Steel na Jackie Collins. Kama movie itakuwa ya Quentin Terantino kunakuwa na characters wengi, wanatokea na kupotea, hapo wanaweza kuzuka wapyaaa, yaani mpaka ufike mwisho wa story ndo uelewe mwanzo, sometime mwisho unaweza kuwa mwanzo hapo hapo ila mpaka ufike mwisho ndo ujue mwisho ulikuwa mwanzo. Ni story tamu ila ngumu kwa wasomaji. Inatakiwa uvumilivu.

Wasomaji wengi wamapenda ku fall in love na characters, na ni wavivu wa kufikiri kujua zaidi. Ndo maana wanalalamika, ila naamini kwa sisi tutaofika mwisho tutafaidi sanaaa. Cause really mpaka hapa i cant tell where the story is going which is everything i need kuendelea kusoma.
 
Nice story! Though umejaribu kufanya kitu kimoja ambacho nafatilia kwa umakini if you will be able to pull it off. Umeenda out of the box kwa kuleta COMPLEX STORY. Story flani kama caliber ya Daniell Steel na Jackie Collins. Kama movie itakuwa ya Quentin Terantino kunakuwa na characters wengi, wanatokea na kupotea, hapo wanaweza kuzuka wapyaaa, yaani mpaka ufike mwisho wa story ndo uelewe mwanzo, sometime mwisho unaweza kuwa mwanzo hapo hapo ila mpaka ufike mwisho ndo ujue mwisho ulikuwa mwanzo. Ni story tamu ila ngumu kwa wasomaji. Inatakiwa uvumilivu.

Wasomaji wengi wamapenda ku fall in love na characters, na ni wavivu wa kufikiri kujua zaidi. Ndo maana wanalalamika, ila naamini kwa sisi tutaofika mwisho tutafaidi sanaaa. Cause really mpaka hapa i cant tell where the story is going which is everything i need kuendelea kusoma.
UmeoIangalia vizuri. Kuna boya humu hadi ushauri katoa kisa anataka stori inayolandana na yeye.......... FU..CK!!
 
Story nzuri na inaeleweka jamani my be MTU utaki kuupa kazi ubongo ila inaeleweka vizuri tu ukitaka kuielewa na ukiisoma taratibu matukio yanaeleweka
 
Nice story! Though umejaribu kufanya kitu kimoja ambacho nafatilia kwa umakini if you will be able to pull it off. Umeenda out of the box kwa kuleta COMPLEX STORY. Story flani kama caliber ya Daniell Steel na Jackie Collins. Kama movie itakuwa ya Quentin Terantino kunakuwa na characters wengi, wanatokea na kupotea, hapo wanaweza kuzuka wapyaaa, yaani mpaka ufike mwisho wa story ndo uelewe mwanzo, sometime mwisho unaweza kuwa mwanzo hapo hapo ila mpaka ufike mwisho ndo ujue mwisho ulikuwa mwanzo. Ni story tamu ila ngumu kwa wasomaji. Inatakiwa uvumilivu.

Wasomaji wengi wamapenda ku fall in love na characters, na ni wavivu wa kufikiri kujua zaidi. Ndo maana wanalalamika, ila naamini kwa sisi tutaofika mwisho tutafaidi sanaaa. Cause really mpaka hapa i cant tell where the story is going which is everything i need kuendelea kusoma.

Kubwa la Maadui, Heri ya Mwaka Mpya!

Nimependa sana jinsi unavyofuatilia story za wenzio na kutoa positive comments, so inspiring.
 
Me mwenyewe macho yamenitoka hapa yaani dah! Kizunguzungu kwa kweli.

Kha! Wa Tz changamsheni Ubongo basi jaman mbona mnaniangusha!?

eti shetani pori, hahaha😀

Hehe

Nice story! Though umejaribu kufanya kitu kimoja ambacho nafatilia kwa umakini if you will be able to pull it off. Umeenda out of the box kwa kuleta COMPLEX STORY. Story flani kama caliber ya Daniell Steel na Jackie Collins. Kama movie itakuwa ya Quentin Terantino kunakuwa na characters wengi, wanatokea na kupotea, hapo wanaweza kuzuka wapyaaa, yaani mpaka ufike mwisho wa story ndo uelewe mwanzo, sometime mwisho unaweza kuwa mwanzo hapo hapo ila mpaka ufike mwisho ndo ujue mwisho ulikuwa mwanzo. Ni story tamu ila ngumu kwa wasomaji. Inatakiwa uvumilivu.

Wasomaji wengi wamapenda ku fall in love na characters, na ni wavivu wa kufikiri kujua zaidi. Ndo maana wanalalamika, ila naamini kwa sisi tutaofika mwisho tutafaidi sanaaa. Cause really mpaka hapa i cant tell where the story is going which is everything i need kuendelea kusoma.

Umeona eee! Asante wangu kuwasaidia watz maana ni sheeddah! Wanataka watafuniwe na kumeza wamezeshwe! Kiruuu

Hii story iko poaa yaani hizi ndio aina nazipendaga usisaau kunitag tuuu jaman

Poa poa wangu

UmeoIangalia vizuri. Kuna boya humu hadi ushauri katoa kisa anataka stori inayolandana na yeye.......... FU..CK!!

U know! Wacha tutaenda nao mdogo mdogo ki kokoroo zaidi!

Story nzuri na inaeleweka jamani my be MTU utaki kuupa kazi ubongo ila inaeleweka vizuri tu ukitaka kuielewa na ukiisoma taratibu matukio yanaeleweka

Preeeeeeeeaaaaaaach

Kubwa la Maadui, Heri ya Mwaka Mpya!

Nimependa sana jinsi unavyofuatilia story za wenzio na kutoa positive comments, so inspiring.

Amen!
 
Stori zikaenda enda na wewe! Rasheedah yupo vlueless kuwa Kungwi anatembea na mumewe mtalaka, kungwi akaomba ushauri na maujanja kwa Rasheeda.
Kungwi: asee nimechoka ya kijijini huwezi nitaftia kiserengeti kimoja kikaninyooosha?! Kulalia mazee nahisi nazidi kuzeeka hata ma ujanja sina tena yote yameisha. Sisi wanawake tunaakili nyingi ila kwangu naona zinaisha!
Rasheeda: akacheeeeeka sana, Kungwi bwana kungwi wewe unachukuaje ujuzi kwa raia wa kawaida sasa?! Akampa maujuzi na nini pale Kingwi akaomba poo, kweli wajinga ndio walaji sio walwaji! Akajisemea Kungwi kimoyomoyo. Basi nimeshakuelewa ngoja aje mwanangu Maringo nitamwulizia ulizia afu nikuforwadie. Wakabadilishana namba za simu Rasheeda akaondoka zake.

Lunch time Maringo akapigiwa simu akatoka kwenda lunch na Mkuu wa mkoa, mkuu wa mkoa kakodi gari lingine akijua pale ataonwa na Mrembo, kweli mchezo wa karata 3 aliuweza. Maringo akaingia kwenye mchuma V8 gari lote linatikishika, big body kama K.Michelle wa Marekani, chura wa kumwaga! Mkuu wa mkoa anachizika kampeleka Royal Livingstone! Lunch na wewe Patric anamwaga ung'eng'e
Patric: unajua tangu nimekuona nimekupenda ghafla, usiku silali nakuwaza wewee
Maringo: we si umenitamani ndio maana haulali
Patric: hapana mpenzi huku anamshika mkono! Me nimekupenda bure kwa mapenzi yote
Maringo: na mkewako je
Patric: ah mke wangu yupo si tutafanya kwa siri!
Maringo: siri hiyo inakuwaje?! Uchi nakupa kwa siri alafu?! WhaT next?!
Patric: kwani wewe unataka nini?!
Maringo: unauhakika utaniweza?! Si unaniona?! Me najua umeoa na wala staki matatizo na mke wako kabisaa! Na najua umenitamani, ukishanibabua unasepa na sitakuwa na pa kukupata kwahiyo ombi lako nimelikataa! Hata mimi natamani pia kuwa na familia! Sio unitwange weee nizeekee Lusaka bila watoto
Patric: familia hata leo nakupa wala usiwe na wasiwasi ukitaka nyumba, gari, kazi nzuri kama hiyo ya bank anazingua meneja nakuhamisha kokote unakotaka
Maringo: akakumbuka jinsi Joe alivyomtenda kwa Kandi akaona huu ndio muda wa kulipiza! Akamjibu naomba nikufikirie j2 tuonane nikupe jibu akijua kesho anaenda kuongea na mama yake ampe maujanja! Little did she know!
Patric: nashukuru sana mpenz wakala pale akamrudisha ofisini akaondoka moyoni anafuraha kuwa sasa kile chombo anakitendea haki

Weekend ikafika Drogba Oga na Didie wakakutana kwa Oga wakaweka kambi kama kawaida! Stori stori na wewe
Oga akawa anajigamba kapata chuma kipya nyomi ya kufa mtu, wenzake wakamwuliza Selina vipi?!
Oga akawaambia Selina bwana hata simwelewi elewi muds mwingi nipo alone ila kwa huyu demu hapa nimenasa mpaka namdindisha ndotoni namfakamia mashambulizi ya kufa mtu nikiamka hamna kitu naota
Wenzake wakamcheeka oooo abeeeeeg! Oga abeeeeeg! U cray Ooooo! Huku wanaendelea kucheka!
Baadae Drogba akafunguka juu ya Selina kuna siku nimemwona yupo na mkuu wa mkoa wanaingia hotelini pale mjini me nilitoka kufuatilia vitu vya ofisini kwa hotel meneja alikuwa ananunua hisa za pale ofisini. Basi nikawaona ila wao hawakuniona wameshikana viuno na nini
Mdogowangu utakufa yule mkuu wa mkoa kitombi hatari anatembea na mama na kadada kamoja pale benki kwenu akaanza kukaelezea, Oga akajibu si Mrembo huyo! Dah kumbe mrembo nae anajidai hayumo kumbe yumo! Akajisemea Oga
Drogba akazidi kufunguka pia kampangia nyumba kamama kamoja kametokea kijijini kuna rafkiangu ni jirani wa huo mtaa wa kimada wa mkuu wa mkoa basi ni balaa tupu! Namhurumia mkewake Mary.
Didie akadakie Mary ndo yule nilitembea nae skuile au?!
Oga: eh na Didie nae anatembea na wake za watu!? We Drogba utammaliza mdogowako, i hope ur using protection oooo! My braza i dont want u to die oooo! I don't!
Drogba akampa ramani yooote waliopanga na pacha mwenzie didie, ah me wakati mwengine nakuwa nipo taiti nimefungia mtu sa huyu labda Kandi, Oga akashtuka Kandi tena?! Drogba akamwambia u know Kandi ey my gurl! Oga akachoka tangu lini? Akamwambia a month naaaaaw! Oga akajibu eiiii! Chinekeee i tell you naaaaw Droga you will die ooooo, stop it oooo!
Drogba akaendelea so wakati nipo na Kandi ma mchungaji Neema, Oga akajibu Neema Ooo! Mama Pastor Oooo! You Drogba sikufahamu! Aseee me sio ndugu yako oooo! This is too much oooo, Drogba Please Ooo! Stop this nonsense ooo abeg! Please my bro aaa, Didie talk to your half. He will go to hell Ooo! Didie hana usemi na yeye mgeni kwenye gaMe inabidi awe mpole
Drogba akafunguka unajua me angala nina 3 na natumia protection so nikizidiwa namgaia si unajua Yesu kasema tusiwe wachoyo so namgawia nusu yangu Didie hapa nae afaidi si unajua tunavyofanana hamna anaeweza notice tofauti yetu upo mbali sana, kwenye balls, mmoja ana balls ina kovu la rangi jeupe mwengine balls zake hazina kovu! Eh Oga akachoka! Labda kwasababu yeyr anajua kuwatofautisha kwasababu wamekua pamoja akaona hii kali

Wakaanza kudiscuss mambo ya kazini Drogba akamwambia Didie vipi mzee Masoud naskia ana expand horizon yake to Dubai and Accra Ghana na Lagos Nigeria! Mbona mambo yatakuwa mwake naskia mnasafiri nae pamoja na Joseph Braza hongera sana you being a finance manager Didie lazima upo proud!
Didie akajibu ndio am proud nimeiletea kampuni feza nyingi sema bado ngoja kwanza tutengeneze branch tutapata hela za kuwachapa watu. Kamamwuliza Oga vipi benk haujapata big fishes au upo buzy na Maringo?!
Oga: so far wapo 40 lakini kwa sasa ngoja kwanza wafike 100 ndio itakuwa nzuri kuendelea na plan yetu. We Drogba vepee?!
Drogba: ah me kwangu HR pale hamna kitu si unajua nipo Real estate hamna vitu kiviile ila wakija tutapanga deal. Drogba akaendeleza plan yake ya kuwazungusha michepuko wake. Oga akameuliza lini uta dettle down na uta settle down na nani?!
Drogba: this is not the time for settlement, bado sisi vijana wasogo sana, miaka 35 bado kabisa damu inawaka

Musa nae akajiskia mpweke, miaka 2 sasa hana demu, upwiru mwingi, hana pa kumpata demu akaamua atoke zake out angalau apunguze stress! Akaenda kulala Kayube Estate! Usiku amenda Dinner anakutana na mrembo anawaka kapiga bonge la makeup! Akaona uzalendo usimshinde akaenda kumsalimia, wakawa wamekaa pale wanakunywa lakini msichana alikuwa uncomfortable! Musa akawa haelewi kwanini, akamwuliza wewe ni Mzambia?! Akajibu hapana mimi nimetokea Mbuki na Faso! Akiwa katika maongezi akasikia mtu anamwita Evelyne! Njoo huku nimeshafika. Dada wa watu akamuaga Musa akaondoka. Musa akasema dah kweli me sina bahati, nikama nimeshika dhahabu alafu nikapokonywa ndani ya nusu saa! Akawa anamwangalia tu Evelyne anavyoishia.

Selina kama kawaida anamfundisha Caroline mambo yao ya ballett! Caroline amesha catch up na baba yake Jose ametoka, skuhiyo darasa lilipigwa saa 11 jioni mpaka saa 2 usiku ili tu abaki afanye alichoambiwa na mganga. Caroline anashangaa mwalimu aondoke leo?! Selina akaanza kujifanya anaumwa pale na nini! Akaomba alale anajiskia kizunguzungu, Caroline na huruma za kitoto akampeleka kulala guest room, Caroline akaendelea na mambo yake pale na nini akamsahau mwl akaingia kulala, Jose hakurudi sikuoyo alifichwa na Pendo. Usiku saa 6 kasoro kufika akashtuka anaelekea chumbani kwa Joseph anakuta hamna mtu, akakaa mpaka saa 7 usiku mtu hajarudi akazodoka, asubuhi akaamka fasta fasta akaandika kinoti kuwa amepata nafuu anaondoka akaweka mezani akasepa, Caroline kuamka akakuta kinoti, akasoma akacheka tu akakitupa kwenye dust-bin!

Maringo akatua kwa mama yake Rasheeda, wanaongea ongea na wewe, akampa ubuyu wote wa beans wake Joe alivyotembea na office mate akamwambia naona ofisi chungu mama roho yauma kama inataka kunitoka
Rasheeda: anamhurumia kweli lakini hana jinsi akamwambia hayo ndo taliyonifanya niondoke kwa baba yako, keshanipa talaka yangu sasa nimekuja kukaa hapa mjini, nikajapata bwana mzuuuri sana ananipenda hivi nilivyo
Maringo: akakasirika mama hapana asee hii ni ndoa sio relationship haukupaswa kuondoka sio vizuri kabisa! Huki analia maskin! Umefanya vibaya sana kaka Hachikoko na Luwi wakiskia hawatoelewa kwani umewaambia?!
Rasheeda: hata hawajui ndio maana nimekuja kutafuta nyumba nikapanga! Nitulie kwanza baada ya miezi 6 niwaite mje
Maringo: analia hakupenda wazazi waachane lakini atafanyaje sa ndio imetokea! Akawa analia pale anabembelezwa!
Rasheeda: mwanangu nashukuru kwamba umekua na umewaona wanaume walivyo, inabidi u fight for your happiness hata hawa viongozi wa dini na wa serikali hii ndio michezo yao. Wewe komaa kupata amani na furaha yako hizi tv na cartoons na fairy tale stories zinawaharibu watoto sana mnatafuta happily ever after ila hamjui happily ever after inapitia wapi? Inapatikanaje?! Ina fightiwaje?! Ina sacrificiwaje!? Hivyo hawaonyeshi kwasababu movie ni madaa 2 mpaka 3 labda kama sasa hivi naona kuna series ndio wanaeleza ukweli wa maisha!
Maringo: mama kichwa hapa kunaniuma sana wala usiongeze dozi nimeshajaa
Rasheeda: hata bado sijamaliza. Kakako Luwi nae ndo ipo juu ta mawe siku nitamwita naskia amechanganywa huko na kidada kimoja tatizo hamwongei na sisi tuwasaidie ila nashukuru kuwa umekuja na tutayamaliza hapa hapa.
Sasa una mabwana wangapi wamekutamkia wanakupenda?!
Maringo: so far 2 na Joe wa 3
Rasheeda: hapo ndio napopataka, mama Mungu kakupa kiiila kitu, tumia hizi fursa we mwana, embu nipe status za hao dagaa wako
Maringo: kuna baba limoja sijui linani ngoja nikionana nae kesho nitakwambia ila ni Mzambia.
Mwengine anaitwa Oga tunafanya nae kazi bank ni Mnigeria, mama akaguna mmh! Mwengine ni bank manager ila nimeambiwa anaukimwi naogopa hata kumshika
Rasheeda: akacheeeka dah kweli mtoto sinae hapa! Enhe na joe wa 4 sio?!
Maringo: ndio mama
Rasheeda: yani hapo usiache hata kimoja! Kila mmoja mtumie kwa nafasi yake ila usiwagongeshe, ukiwagongesha either watakuua au watauana, na kila mtu kamata maneno yake kisawa sawa! Na usichanganye neno la oga kwa bank manager wala hilo zee nenda nao sawa hakikisha unapewa kiiila kitu roho yako inataka usisahau kutumia condom, habari ya mchezo wa kitandani ajiri kungwi au nenda kwa mama Pendo namba yake hii atakupa somo zuri la kitandani, kesho amkia kwake urudi me mamako siwezi kukupa somo la kitandani ni najisi!
Ila wote wakamate usiache hata moja kitandani ufanye vizuri ukamate ahadi zao na uzidai, ohoo! We shangaa mjini hapa itarudi kwa babako Manoa kijijini ukalime me nishasema sirudi kabisaa! Alafu mambo ya marafiki hata usi entertain kabisaa! Hao ndo wachawi wakubwa kaa mwenyewe kivyako vyako ukishindwa niite mie mamako nitakuja kukupa kampani! Ukijidai unashika moja utakonda roho wewe! Joe akicheat unakonda roho utaporomoka kiafya utachukia wanaume wote kwa selfish ya mtu mmoja, mwanangu me mama yako nakwambia find your happiness kwa akili usije pata magonjwa ya moyo na ma kisukari yasio na sababu kisa unapenda na kuwaza umetendwa acha huo ujinga fight for your happiness narudia fight for your happiness kila mtu anakufa hakuna kinachobaki hata hawa wamama wa dini nao wanakitembeza sana si tunawaona bwanaa ndio ivyo kinga lazima la hasha mkapime mkiwa wote sio mmoja anaenda mwengine anabaki ndio mwanzo wa kunadilishiwa majibu ukauzoa ukimwi shauriako
Maringo: akachoka na ushauri wa mama yake huenda divorce ilimsumbua sana na akili zake haziko sawa. Akaona bora aongee na kungwi huenda yeye ndo kidogo akili zipo sawa

Usiku wamekaa wanaangalia Tv wanaskia mtu anafungua mlango, mama hana wasiwasi anajua ni Patric, Maringo anashangaa mwizi nini?! Kuingia tobaaaa ni Patric! Maringo anashangaa, Patric hakumwona maana alipoingia alienda moja kwa moja kwa Rasheeda akaanza kumshika shika anambusu! Rasheedah kumzuia Patric anashangaa leo vepee akamwambia anataka kukuintroduce kwa mtoto wangu wa kike na wa pekee huyu hapa, Patric kumwona tumbo lilijaa mavi, Maringo kumwona akachoka mara 100, mama mtu hajui hili wala lile, anaendelea tu Maringo huyu ndio mpenzi wangu anaitwa Patric! Patric huyu ni mwanangu anaitwa Maringo, Patric akampa mkono nimefurahi kukufahamu. Maringo akamwangalia akaanza kushikilia tumbo na mdomo anaskia kutapika akatapika matapishi mengine yakaangukia kwenye mkono wa Patric Bwaaaaaaaaaaah!

ITAENDELEA SAA 11 JIONI
 
Binafsi napenda story kama hizi,story inakuwa kama tamthiliya hivi so inakuwa na mvuto wa kuamsha ubongo,money penny nipo na ww toka mwanzo mpaka mwisho

Asante sana boss kubwa nashukuru kwa support
 
Hatari lakini salama huyo patric ashaumbuka haah haah patamu hapo,paka anapopiga kinanda na mluzi
 
Back
Top Bottom