MWONGOZO: Zingatia haya unapoweka tangazo lako!

Bora mmetoa ufafanuzi maana humu watu huwa wanatoa matangazo ya biashara kama wanakimbizwa.
 
Ndugu wadau wa Jukwaa pendwa la Matangazo Madogo,

Tunafarijika kuona mnaendelea kutumia vizuri jukwaa hili katika kufanya biashara ndogo ndogo.

Hata hivyo, kuna changamoto kwa baadhi ya wenzetu kushindwa kuzingatia vigezo vya kuweka matangazo yao hivyo kupelekea matangazo yao kuondolewa hewani.

Yafuatayo ni masharti na vigezo vya msingi unavyopaswa kuzingatia kabla hujaweka tangazo lako;

  1. Elezea huduma/bidhaa unayouza kwa maelezo machache yanayojitosheleza
  2. Kama ni bidhaa, elezea hali yake (mpya au imetumika muda gani) huku ukiambatanisha na picha yake halisi.
  3. Taja bei
  4. Taja mahali huduma/bidhaa hiyo inapopatikana pamoja na mawasiliano yako.
  5. Weka taarifa mpya kuhusu bidhaa hiyo kwenye uzi husika, usianzishe uzi mpya.
  6. Usiweke tangazo moja mara nyingi.
Ni vyema kuzingatia hatua hizo chache. Kinyume na hapo, tangazo lako litaondolewa hewani.

Karibuni kwa maswali na ufafanuzi zaidi..

Mkuu naomba kuuliza nawezaje kuedit thread title?? au haiwezekani kufanya hivyo??
 
Naomba ufafnuzi wa hili "You have been banned for the following reason: We do not allow Spamming and Hotlinking[OFA YA MWEZI: Jipatie Website kwa Bei Nafuu!!!" hiyo ni akaunti ya jama microsafi imefungwa
Hiyo sababu uliyoitaja ipo kinyume na sheria za JF. Adhabu yake ndio hiyo(Ban)
 
Swali langu kuna akaunti ya jamaa microsafi imefungiwa kwasababu ya hot link ya matangazo, je lipoje ili nimfikishie

pia huo uzi wa zamani unaupataje, kwani unakuta umepost wiki imepita

Naomba ufafnuzi wa hili "You have been banned for the following reason: We do not allow Spamming and Hotlinking[OFA YA MWEZI: Jipatie Website kwa Bei Nafuu!!!" hiyo ni akaunti ya jama microsafi imefungwa

Ujumbe huo hutumwa kwa mtu aliyeweka link ya kwenda kwenye site yake ama anayesambaza ujumbe mmoja mara nyingi (ndiyo maana ya spamming and hot-linking) ambako ni kosa kwa mujibu wa JamiiForums Rules

Asante.
 
Ndugu wadau wa Jukwaa pendwa la Matangazo Madogo,

Tunafarijika kuona mnaendelea kutumia vizuri jukwaa hili katika kufanya biashara.

Hata hivyo, kuna changamoto kwa baadhi ya wenzetu kushindwa kuzingatia vigezo vya kuweka matangazo yao hivyo kupelekea matangazo yao kuondolewa hewani.

Yafuatayo ni masharti na vigezo vya msingi unavyopaswa kuzingatia kabla hujaweka tangazo lako;

  1. Elezea huduma/bidhaa unayouza kwa maelezo machache yanayojitosheleza
  2. Kama ni bidhaa, elezea hali yake (mpya au imetumika muda gani) huku ukiambatanisha na picha yake halisi.
  3. Taja bei
  4. Taja mahali huduma/bidhaa hiyo inapopatikana pamoja na mawasiliano yako.
  5. Weka taarifa mpya kuhusu bidhaa hiyo kwenye uzi husika, usianzishe uzi mpya.
  6. Usiweke tangazo moja mara nyingi.
Ni vyema kuzingatia hatua hizo chache. Kinyume na hapo, tangazo lako litaondolewa hewani.

Karibuni kwa maswali na ufafanuzi zaidi..

Hiyo namba 2 na 3 ndo pasua kichwa kwa makanjanja, utaletaje tangazo bila bei, ikiwezekana muwapige ban kabisa
 
Pia naomba kuuliza baadhi ya matangazo licha ya kuwa yamekidhi vigezo huwa yanafutwa, ni kwanini na ukiangalia katika uzi husika hulikuti
 
Pia naomba kuuliza baadhi ya matangazo licha ya kuwa yamekidhi vigezo huwa yanafutwa, ni kwanini na ukiangalia katika uzi husika hulikuti

Matangazo ambayo huondolewa ni yale yanayokiuka vigezo tajwa hapo juu au yanavunja JamiiForums Rules..

Unaweza kutupatia mfano wa tangazo lililoondolewa ambalo unadhani limeondolewa kimakosa?!

Karibu..
 
Umefafanua vizuri sana. Wale wanaosema nifuate PM muwe mnawapiga ban kabisa. Tangazo la biashara linatakiwa kuwekwa lote
 
Mathalani, Tangazo langu na taka kulirejea wiki nzima yaani kwa siku mara 1, je uzi ule niliotumia naweza kuupataje
 
Ni moderators pekee ndiyo wenye uwezo wa kufanya hivyo. Wapo online, watumie ujumbe kueleza suala lako.

Je, una swali lolote kuhusiana na Jukwaa la Matangazo?
Karibu..
kwahyo kama nikitaka kuchange thread title naweza kuwaona moderators??
 
Sawa kwa muongozo,nina mswali mawili nahitaji majibu.
1)kwanini kufungua acc mnachelewa sana ku acept? Kuna ndugu anasubiri toka juzi na bado hakuna majibu.
2)nitumie njia gani kubadilisha jina langu humu na maombi kupokelewa haraka?
 
Kama mnafatilia swala la kuwekwa matangazo hapa jukwaani je ni hatua zipi nyinyi jamii forum mnazichukua endapo mtu akatapeliwa ama kuuziwa kitu feki...???
 
Back
Top Bottom