Mwinjilisti amvaa Rais Magufuli, amuonya

Mwinjilisti amvaa Rais Magufuli, amuonya

Kwa kweli nimempenda sana huyu Mwinji. Haya ni maneno yaliyojaa hekima kwa wenye masikio tu kuyasikia.
 
Mchungaji gani asiyejua mamlaka iliyopo inatambuli mpaka kwa MUNGU?hajielewi huyo,wala kwenye uzi huu sirudi tena
mtumishi WA kanisa la kwanza LA Mungu.... Ndio maana anauthubutu wa kukemea... Wengine wanafiki hawana roho wa Kweli wa Jehovah
 
Nakushukuru angalau kiongozi wa dini umejitokeza na kusema neno la kuitakia nchi yetu mema bila unafiki wa CCT, TEC etc!
Kamara Kusupa ni zaidi ya mwinjilisti, huku ni mwanaharakati kitambo ukifanikiwa kusoma vitabu vyake utaligundua hilo
 
" watanzania niombeni, hii kazi ya urais ni ngumu sana, najuta kwanin nilichukua fomu"

Sasa em jaribu kufanya maombi hapo ulipo, utamuombea kwa lipi na lipi hutaliombea ..?!

Unyenyekevu ni muhim sana, hasa wa kufuata taratibu na sheria ..!!
Mimi nilipenda @TL Marandu alivyomuombea. Nilisahau kucopy ile sala ningeisali kila siku
 
Asante sana ndugu mwinjilisti, nadhani kuna haja ya viongozi wakuu wa kidini kuliona hili na kulisemea kama huyu mwinjilisti
 
Mchungaji gani asiyejua mamlaka iliyopo inatambuli mpaka kwa MUNGU?hajielewi huyo,wala kwenye uzi huu sirudi tena

Na usirudi kwa vile hujasoma uzi bali umeishia kusoma kichwa cha Uzi. Mchungaji hajamdharau rais wala mamlaka yake bali ametoa ushauri kwa nia njema,tatizo lenu wapiga filimbi mnakurupuka na hii ni hulka ya wanaccm wa sasa.
 
Pengo anapiga jaramba, soon atalipuka na kukabiliana na yule jina lake linaanzia na Gwa
 


Kamara Kusupa, Mwinjilisti wa makanisa ya kipentekoste hapa nchini, amesema marufuku ya mikutano ya hadhara na maandamano kwa vyama vya upinzani iliyotangazwa na Rais John Magufuli itavuruga amani ya nchi.

Kusupa ambaye ni miongoni mwa watu walioshiriki katika harakati za kuishinikiza serikali kurejesha mfumo wa vyama vingi mwanzoni mwa miaka ya 1990, amemuandikia barua Rais Magufuli yenye kichwa cha habari; “Msimamo wako utachochea maasi”.

Akizungumza na wanahabari mapema leo, Kusupa amesema, kauli za Rais Magufuli ikiwemo ile kusema watakaoandamana ‘watakiona’ na kusema, ‘mimi sijaribiwi’ ni kauli zinazothibitsha namna rais huyo anavyokosa unyenyekevu wa kiuongozi.

“Ukiwa binadamu huna namna ya kuepuka majaribu, asiyejaribiwa ni Mungu pekee. Ndio maana hata mwokozi wetu Yesu alijaribiwa na pia alitufundisha kwamba tunaposali tumwombe Mungu atuepushe na majaribu.

Mheshimmiwa rais haki inayokuwezesha kuzunguka Manyoni, Singida, Nzega na Mwanza kwenye viwanja vya Furahisha ukifanya mikutano ya hadhara kuwashukuru wananchi waliokuchagua, ni haki hiyo moja ndiyo waliyonayo Lowasa, Mbowe na wanasiasa wengine,” amesema.

Amemtaka Rais Magufuli, asiwaoneshe watanzania kwamba haki ya mwenyekiti wa CCM taifa inaanzia pale zilipoishia haki za wanasiasa wa vyama vingine kwani kufanya hivyo ni kuchochea maasi.

“Rais Magufuli anapaswa kuhakikisha, taifa halizalisahi wakimbizi kama yalivyotokea maafa ya tarehe 27 Januari, 2001 baada ya Chama Cha CUF kuandaa maandamano na Serikali kuyasambaratisha na kuchochea vurugu zilizozalisha wakimbizi, waliokimbilia nchi mbalimbali ikiwemo Kenya,” amesema Kusupa.


Chanzo: Mwanahalisi

mungu akubariki kwa kumuonya pilato
 
Mchungaji gani asiyejua mamlaka iliyopo inatambuli mpaka kwa MUNGU?hajielewi huyo,wala kwenye uzi huu sirudi tena
kwenda nzako wewe mnafiki mamalaka za duniani ziko chini ya shetani,mungu sio mwanasiasa jifunze kuwa na nidhamu
 


Kamara Kusupa, Mwinjilisti wa makanisa ya kipentekoste hapa nchini, amesema marufuku ya mikutano ya hadhara na maandamano kwa vyama vya upinzani iliyotangazwa na Rais John Magufuli itavuruga amani ya nchi.

Kusupa ambaye ni miongoni mwa watu walioshiriki katika harakati za kuishinikiza serikali kurejesha mfumo wa vyama vingi mwanzoni mwa miaka ya 1990, amemuandikia barua Rais Magufuli yenye kichwa cha habari; “Msimamo wako utachochea maasi”.

Akizungumza na wanahabari mapema leo, Kusupa amesema, kauli za Rais Magufuli ikiwemo ile kusema watakaoandamana ‘watakiona’ na kusema, ‘mimi sijaribiwi’ ni kauli zinazothibitsha namna rais huyo anavyokosa unyenyekevu wa kiuongozi.

“Ukiwa binadamu huna namna ya kuepuka majaribu, asiyejaribiwa ni Mungu pekee. Ndio maana hata mwokozi wetu Yesu alijaribiwa na pia alitufundisha kwamba tunaposali tumwombe Mungu atuepushe na majaribu.

Mheshimmiwa rais haki inayokuwezesha kuzunguka Manyoni, Singida, Nzega na Mwanza kwenye viwanja vya Furahisha ukifanya mikutano ya hadhara kuwashukuru wananchi waliokuchagua, ni haki hiyo moja ndiyo waliyonayo Lowasa, Mbowe na wanasiasa wengine,” amesema.

Amemtaka Rais Magufuli, asiwaoneshe watanzania kwamba haki ya mwenyekiti wa CCM taifa inaanzia pale zilipoishia haki za wanasiasa wa vyama vingine kwani kufanya hivyo ni kuchochea maasi.

“Rais Magufuli anapaswa kuhakikisha, taifa halizalisahi wakimbizi kama yalivyotokea maafa ya tarehe 27 Januari, 2001 baada ya Chama Cha CUF kuandaa maandamano na Serikali kuyasambaratisha na kuchochea vurugu zilizozalisha wakimbizi, waliokimbilia nchi mbalimbali ikiwemo Kenya,” amesema Kusupa.


Chanzo: Mwanahalisi


Ahsante simu ya Tochi kwa kuweka hii habari ya Mwinjilisti. Ningewashauri pia vyombo vya dini vya kiislamu navyo vikatoa mawazo yao. Mwinjilisti ameeeleza vizuri sana bila ya kuogopa anavyoona jinsi hali inavyokwenda ktk kubinywa "political and democratic space" Viza vz kampeni ya UKUTA ya tarehe 1 septemba.

Lakini uzoefu unaonesha kuwa hawa BAKWATA hawawezi wakaeleza jambo bila ya kuegemea upande wa chama dola. Wamekuwa wakijifanya kama ni Idara maalum ya CCM.

wajibu wa viongozi wa dini ktk kukuza amani ya nchi ni kama mfano huu ambao mwinjilisti ameonesha na sio kukaa kimya kama kwamba hakuna ubaya wowote unatokea nchini.

Ningewashari BAKWATA jamaa zangu kiimani wakaonesha mfano wa kutoa mawazo yao ya kupelekea kuimarisha amani nchini kufuatia kampeni ya UKUTA ya tarehe 1 septemba.

Mfano wa maandamano ya Pemba ya mwaka 2001 ni mfano mzuri wa kujifunza kama nchi. Mwinjilist kupitia video yake ameeleza vizuri yaliyotokea na athari zake kwa taifa.

Binafsi nimepoteza ndugu yangu wa karibu katika kadhia ile ya Pemba na wengine walikimbia nchi mpaka leo hii hawajarudi . Ni lazima wadau wa amani nchini kama viongozi wa dini, wanao mchango mkubwa ktk kuhakikisha serikali wanafikia maelewano na chadema ili kuepusha athari inayoweza kutokea.

katika kulikabili hili busara inahitajika na sio kauli za ubabe. Tukumbuke vile vile kufanya kufanya siasa ni haki ya vyama na tusijidanganye , popote pale haki inapokosekana au inaposhindwa kutolewa basi amani nayo inatoweka.

Suala la vyama kufanya mikutano na maandamano ni haki ambayo imetolewa kwa mujibu wa sharia ya vyama vya siasa.

Hivyo nafikiri serikali ingeonesha ustaarabu wa kuviruhusu vyama vya siasa vikaendelea na harakati zao za kisiasa kama sharia inavyotaka badala ya kuweka mazingira magumu na yasiyokubalika .
 
ndungu wana JF pamoja na maoni mengi mnayotoa lakini msisahau yale tuliyoyasema sisi kina gogo la shamba kwamba,miaka hii mitano ni miaka ya kusikia na kuona mambo mengi ya ajabu
 
Wakosoaji wanaongezeka lakini mzee Uchwara bado ameziba pamba masikioni.
 
Mleta uzi, tumia lugha laini. Kumvaa mtu ni kama vile kuna mapambano be it ya maneno au silaha! Hakumvaa, ameeleza hisia zake kwa nia njema kabisa.
Yuko sahihi KUMVAA NDO SAHIHI! Mtu anayeminya uhuru wako ni wa namna gani?
 
Sijaona kama amemvaa, naona kama ameshauri kwa nia njema na ya kiistaarabu kabisa
 
Yale yale ya udini yanaanza kuingilia taratibu mamlaka nyingine za utawala.
Watumishi wa Mungu pale wanapoishia ndipo mamlaka nyingine za kidunia ndipo zinapoanzia.

Ukisoma katika Biblia Takatifu kitabu cha Warumi 13:1 'Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.'

13:2 'Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu. '
Unaweza kuendelea 13:3-14.
 
.....hajielewi. Hawa ndiyo wachungaji fake, walituaminisha mwaka jana mungu kawafunilia eti mamvi ndiyo rais, wanafiki sana
 
Back
Top Bottom