Mwinjilisti amvaa Rais Magufuli, amuonya

Mwinjilisti amvaa Rais Magufuli, amuonya

Kweli tupu.

Mbegu zinazopandwa ni hatari sana pale zitakapomea.
 
Hakuna matamko hatarisha kama ya watu wadini ,wachungaji,mashehe,mapandre,n.k.


Labda huyo so mchungaji ni mwanasiasa.
Hao watu wanasikilizwa mno na wananchi.
 
Tatizo ni kwamba je, huyo mwenye mamlaka anatambua kwamba Mamlaka hiyo aliyonayo imetoka kwa Mungu? Maana tatizo ndio huwa liko hapo. Huwa tunakuwa wepesi kunukuu huo waraka kwa Warumi kwamba mamlaka yote inatoka kwa Mungu, tunasahau wajibu wa utawala kwa Mungu ambaye ndio asili ya Mamlaka yote. Kama mtawala anatambua kwamba mamlaka aliyonayo imetoka kwa Mungu, basi atafuata haki, maana Mungu ni mwenye Haki. hatawabagua watu wake, maana anawatawala kwa niaba ya Mungu mwenyewe. ajiulize kwamba je, kama angekuwa ndio Mungu mwenyewe anatawala, angewabagua watu wake hivyo? Aliwakemea waisraeli wasiwabague hata wageni, sembuse waisraeli wenzao?
Kama kweli ungemjua MUNGU vzr usingesema maneno dhaifu,kuna nyakati MUNGU amenyanyua watu wakorofi kwa makusudi maalumu juu ya jamii au juu ya kikosi cha vita.kusema na kudhani MUNGU hua anawateua wapole na wakarimu pekee umejidanganya.
 
Taifa linahitaji kuwa viongozi wa dini kama huyu ambaye anaweza kusema ukweli bila kuogopa siyo kama wale wanafiki wanaona nchi inaendeshwa kwa tamko ya mtu mmoja wananyamaza kimya hongera sana mtumishi wa Mungu.
 
Huyu u
Kama kweli ungemjua MUNGU vzr usingesema maneno dhaifu,kuna nyakati MUNGU amenyanyua watu wakorofi kwa makusudi maalumu juu ya jamii au juu ya kikosi cha vita.kusema na kudhani MUNGU hua anawateua wapole na wakarimu pekee umejidanganya.
Huyu ukali wake kwa wanyonge tu!LUGUMI,IPTL,CHENGE,LOWASSA AMEWASHINDWA
 
Mchungaji gani asiyejua mamlaka iliyopo inatambuli mpaka kwa MUNGU?hajielewi huyo,wala kwenye uzi huu sirudi tena
Ongozwa na tumbo udhani nchi hii ni ya mama yako au ya familia yako,pa kinuka hutapata muda wa kuongea utumbo huu kengele wewe.
 
Kama kweli ungemjua MUNGU vzr usingesema maneno dhaifu,kuna nyakati MUNGU amenyanyua watu wakorofi kwa makusudi maalumu juu ya jamii au juu ya kikosi cha vita.kusema na kudhani MUNGU hua anawateua wapole na wakarimu pekee umejidanganya.

Biblia imejaa mifano lukuki ya watawala ambao pale tu walipofanya tofauti na mpango wa Mungu, aliwaadhibu mara moja. Mungu alimsifia sana Mfalme Daudi kwa sababu hata kama alianguka mara nyingi, alitubu mara moja.

Daudi alikuwa hataki hata kuwagusa "maadui wake", namzungumzia Mfalme Sauli. Huyu alipanga kumuua Daudi mara nyingi, lakini hata pale Daudi alipopewa na Mungu nafasi ya kumdhuru Sauli, alimwachia kwa kuheshimu kwamba "huyu ni mpakwa mafuta wa Mungu".

Lakini Mungu alimwadhibu Daudi pale alipomnyanyasa na mwisho kumuua Uria. Pia alimwadhibu pale alipoamua kufanya sensa kinyume cha maagizo ya Mungu. mara zote hizo Daudi alitubu. kuna ile ishu ya Shimei ambaye alimlaani Mfalme Daudi pale alipokuwa anamkimbia mwanae mwenyewe wa kumzaa, Absalom [2Sam.16:5-13]. Makamanda wa Daudi walitaka kumuulia mbali, bali Daudi akasema mwacheni, pengine katumwa na Mungu huyu, na mimi kwa kuvumilia pengine Mungu atanisamehe maovu yangu.

Ni kweli, Mungu alimwita mfalme mpagani na katili sana, Nebukadreza, "mtumishi wangu" [Yeremia 27:6] lakini kumbuka Mungu alishasema mwanzo kwamba pale atakapotumia taifa ovu kuadhibu taifa teule, hao taifa ovu wawe makini sana kutambua kwamba wasingeweza kufanya lolote kwa taifa teule, pasipo kuwezeshwa na Mungu.

lakini kwa upumbavu wao, watajiona wamefanya hayo kwa nguvu zao wenyewe, na hapo ndipo Mungu atakapowaadhibu na wao [Kumb. 32:21-36].

Kwa hiyo hata kama Mungu huwatumia pia watawala waovu ili kuadhibu taifa lake, bado hao watawala waovu imewapasa kuifuata sheria ya Mungu. imewapasa kumtambua, wafanye tu kile alichokusudia Yeye alipoamua kuwatumia, pamoja na uovu wao. hapo tu ndipo nao watakuwa salama.
 
Hakuna matamko hatarisha kama ya watu wadini ,wachungaji,mashehe,mapandre,n.k.


Labda huyo so mchungaji ni mwanasiasa.
Hao watu wanasikilizwa mno na wananchi.
Ni vizuri mtu anapokosea ukamueleza lakini kunyamaza kwako hakumsaidii ni kuzidi kumpoteza
 
Hivi Karama Kusupa ni mzaliwa wa mkoa gani vile Tanzania? Mmh
 
Ahsante kwa uchambuzi mzuri na wenye lengo la kuleta mustakabali wa amani ambayo ni sisi pekee raisi akiwa mstari wa mbele kuirinda
 
Tii madaraka yaliyowekwa na MOLA. ..
 
Back
Top Bottom