GwaB
JF-Expert Member
- Mar 19, 2014
- 3,617
- 4,706
Uongozi ni pamoja na kuchunga ulimi wako usikupotoshe. Lakini ulimi hauwezi kutamka kile usichopanga kusema akilini. Madiru amewatangazia walipakodi wasiotaka kulipa Kodi za Tanzania wahamie Burundi. Ni tamko linalohitaji ujasili kulitamka hadharani kwa kiongozi tena Waziri la fedha.
Mwelekeo wa mkuu wa nchi ni kuifungua na kuisimamisha nchi kiuchumi na hii kauli aliitoa hadharani na Madiru alisikia. Najiuliza tu, kama hawa walipakodi wakihamia Burundi huyu waziri
atakusanya kodi kutoka vyanzo gani?.
Hivi tunarudi kutegemea misaada ya wafadhili kuendesha nchi? Najiuliza pia, hivi mkuu wa nchi hii alilenga nini kuwaasa waliohamishia biashara nje ya nchi warudi nyumbani huku waziri wake mkusanyakodi akikejeli watu wanaopaswa kuchangia kujenga nchi wahamie nchi jirani?
Nadhani kuna kitu hakiko sawa. Viongozi hawaongei lugha moja.
Jana tu Madiru ameendelea kula matapishi yake kwa kuwaomba watanzania wasikimbie nchi wakati yeye ndie aliyetoa ushauri huo, hivi anadhani anaongoza watoto wa chekechea?....... Du nchi inayumba Sasa!.
Mwelekeo wa mkuu wa nchi ni kuifungua na kuisimamisha nchi kiuchumi na hii kauli aliitoa hadharani na Madiru alisikia. Najiuliza tu, kama hawa walipakodi wakihamia Burundi huyu waziri
atakusanya kodi kutoka vyanzo gani?.
Hivi tunarudi kutegemea misaada ya wafadhili kuendesha nchi? Najiuliza pia, hivi mkuu wa nchi hii alilenga nini kuwaasa waliohamishia biashara nje ya nchi warudi nyumbani huku waziri wake mkusanyakodi akikejeli watu wanaopaswa kuchangia kujenga nchi wahamie nchi jirani?
Nadhani kuna kitu hakiko sawa. Viongozi hawaongei lugha moja.
Jana tu Madiru ameendelea kula matapishi yake kwa kuwaomba watanzania wasikimbie nchi wakati yeye ndie aliyetoa ushauri huo, hivi anadhani anaongoza watoto wa chekechea?....... Du nchi inayumba Sasa!.