Mwigulu Nchemba: Mfumuko wa bei upo chini ya 5%

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
1686820533121.png

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba leo Bungeni Dodoma amewasilisha Bungeni taarifa ya Hali ya Uchumi wa Kitaifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa Mwaka 2023/2024 ambapo moja ya mambo aliyoyasema ni kwamba mfumuko wa bei nchini umeendelea kuwa ndani ya lengo la wigo wa kuwa chini ya asilimia 5.

“Mwaka 2022, mfumuko wa bei ulifikia wastani wa asilimia 4.3 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.7 mwaka 2021, aidha mfumuko wa bei hadi mwezi Mei, 2023 umebaki kama ilivyokuwa katika kipindi hicho hicho mwaka 2022 ikiwa ni wastani wa asilimia 4.0”

“Hali hii imesababishwa na kuongezeka kwa uzalishaji na usambazaji wa bidhaa na huduma na kuongezeka kwa upatikanaji wa mazao ya chakula katika baadhi ya maeneo nchini na Nchi jirani kulikosababishwa na upatikanaji wa mvua katika maeneo yanayotegemea mvua”
 
Huwa tunapenda ku-complicate mambo simple (hence kumchanganya layman)

Nadhani hata mfumuko ungekuwa 100% cha maana ni mtu wa kawaida kutokana na income yake anamudu maisha ?; What wana Disposable Income ?

Hayo mengine ni kuchanganyana tu..., hii naweza kuita sawa na Putting Lipstick on a Pig...
 
Wakati huu ni wa mavuno lakini bei ya unga na mchele imebadirika kidogo sana, yani ni kama imeshuka kwa 2% pekee!
. Subirini kiama ikifika oktoba na kuendelea.

Hatuna viongozi tuna midoli tu
Wauza sura kwenye Mabango

Poda kwa wiiingi!
 
Wakati huu ni wa mavuno lakini bei ya unga na mchele imebadirika kidogo sana, yani ni kama imeshuka kwa 2% pekee!
. Subirini kiama ikifika oktoba na kuendelea.

Hatuna viongozi tuna midoli tu
Wewe ulitakaje? Kama unajua bei ya mazao ndio huleta tofauti ya Mfumuko wa bei Sasa Mwigulu Huwa anaingiaje bei zikipanda?
 
Kuna mfumuko ulioletwa na kuadimika kwa dola, majuzi nimenunua oil filter kwa elf 35 iliyokuwa inauzwa elfu 15 miezi kama mitatu tu iliyopita........utasemaje huo ni mfumuko wa asilimia 5? madelu bhanaa....
 

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba leo Bungeni Dodoma amewasilisha Bungeni taarifa ya Hali ya Uchumi wa Kitaifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa Mwaka 2023/2024 ambapo moja ya mambo aliyoyasema ni kwamba mfumuko wa bei nchini umeendelea kuwa ndani ya lengo la wigo wa kuwa chini ya asilimia 5.

“Mwaka 2022, mfumuko wa bei ulifikia wastani wa asilimia 4.3 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.7 mwaka 2021, aidha mfumuko wa bei hadi mwezi Mei, 2023 umebaki kama ilivyokuwa katika kipindi hicho hicho mwaka 2022 ikiwa ni wastani wa asilimia 4.0”

“Hali hii imesababishwa na kuongezeka kwa uzalishaji na usambazaji wa bidhaa na huduma na kuongezeka kwa upatikanaji wa mazao ya chakula katika baadhi ya maeneo nchini na Nchi jirani kulikosababishwa na upatikanaji wa mvua katika maeneo yanayotegemea mvua”
Mzee wa fix
 
Wakati huu ni wa mavuno lakini bei ya unga na mchele imebadirika kidogo sana, yani ni kama imeshuka kwa 2% pekee!
. Subirini kiama ikifika oktoba na kuendelea.

Hatuna viongozi tuna midoli tu
Bora midoli inauzwa bei mkuu...
 
Back
Top Bottom