Mwigulu: Mfumuko wa bei Tanzania ni nafuu kulinganisha na nchi jirani

USSR

JF-Expert Member
Jul 15, 2015
9,896
22,666
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amesema hali ya mfumuko wa bei wa Tanzania ni nafuu ukilinganisha na nchi nyingine Duniani ambazo bei za bidhaa mbalimbali hupanda kila baada ya masaa machache.

Akizungumza wakati wa Vikao vya Bunge Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Watanzania wawe na imani na njia zinazochukuliwa na Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwenye kukabiliana na Mfumuko wa bei kwa kuongeza uzalishaji kwenye Sekta mbalimbali.

"Mfumuko wa Bei ni tofauti na bei mfumuko wa bei ni kiwango cha kubadilika kwa bei, mfumuko wa bei Tanzania si kama nchi nyingine ambazo kila saa unabadilika, na huo ndiyo mfumuko wa bei ambao ni tatizo kubwa kwenye uchumi" Amesema Waziri Mwigulu Nchemba

Aidha Waziri Mwiguli Lameck Nchemba ameongeza kuwa kwenye kukabiliana na mfumuko wa bei Rais Samia ameagiza kuchukuliwa kwa hatua mbalimbali ikiwemo uongezaji wa uzalishaji kwenye nyanja mbalimbali ikiwemo Kilimo kwa kutoa ruzuku ya mbolea

"Kama tatizo ni kupanda kwa bei zinatatuliwa kwa hatua ambazo Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amezichukua hasa kwa kuongeza uzalishaji" Ameongeza Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba
 
Sisi tunalalamikia mfumuko wa bei hapa Tanzania na wala siyo nchi nyingine. Huwezi kutuua kwa kutulisha kinyesi kisa nchi nyingine wanafanya hivyo, huo ni ujinga uliopitiliza mipaka. Kama serikali ina viongozi wenye upungufu wa uelewa kama huyu Waziri wa fedha ni heri turudi kwenye uchaguzi.
 
Yaani kwa kuwa baba wa familia anatupatia milo miwili ya uji wa chumvi saa nne asubuhi na ugali na kisamvu saa 11 jioni ndiyo iwe halali kulingana na majirani ambao wao wanakula mlo mmoja tuu?!!??
 
kumbe nimegundua kwa nini ukiwa mtanzania kupata passport ya kusafiria ni kazi sana.

Wanatumia nchi za nje kisiasa sana, kwa hiyo diaspora mkiwa wengi hofu ni kuwa lolote laweza kutokea.
 
Tukiwaambia Kenya na Ghana Wana Katiba nzuri mnatufokea hamtaki kujilinganisha na nchi nyingine. Tukiwaambia mfumuko wa bei ni mkubwa Wananchi Wana maisha magumu mnaleta hoja ya kulinganisha na nchi nyingine. Ila nyie ni wachawi, vigagula walozi.
 
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amesema hali ya mfumuko wa bei wa Tanzania ni nafuu ukilinganisha na nchi nyingine Duniani ambazo bei za bidhaa mbalimbali hupanda kila baada ya masaa machache.

Akizungumza wakati wa Vikao vya Bunge Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Watanzania wawe na imani na njia zinazochukuliwa na Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwenye kukabiliana na Mfumuko wa bei kwa kuongeza uzalishaji kwenye Sekta mbalimbali.

"Mfumuko wa Bei ni tofauti na bei mfumuko wa bei ni kiwango cha kubadilika kwa bei, mfumuko wa bei Tanzania si kama nchi nyingine ambazo kila saa unabadilika, na huo ndiyo mfumuko wa bei ambao ni tatizo kubwa kwenye uchumi" Amesema Waziri Mwigulu Nchemba

Aidha Waziri Mwiguli Lameck Nchemba ameongeza kuwa kwenye kukabiliana na mfumuko wa bei Rais Samia ameagiza kuchukuliwa kwa hatua mbalimbali ikiwemo uongezaji wa uzalishaji kwenye nyanja mbalimbali ikiwemo Kilimo kwa kutoa ruzuku ya mbolea

"Kama tatizo ni kupanda kwa bei zinatatuliwa kwa hatua ambazo Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amezichukua hasa kwa kuongeza uzalishaji" Ameongeza Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba
 
Watanzania tuna lalamikia mfumuko nchini kwetu, huwezi kutuagiza kwa majirani utulinganishe nao.
Je income yao ni sawa na kwetu?
Mbona Zambia mafuta ya magari ni rahisi kuliko hapa kwetu na wana yachukulia kwetu?
Au na rais wao awaambie ana pandisha bei kwa sababu majirani bei ni juu. Majibu mepesi kwenye mambo magumu. Phd holder.
 
Tukiwaambia Kenya na Ghana Wana Katiba nzuri mnatufokea hamtaki kujilinganisha na nchi nyingine. Tukiwaambia mfumuko wa bei ni mkubwa Wananchi Wana maisha magumu mnaleta hoja ya kulinganisha na nchi nyingine. Ila nyie ni wachawi, vigagula walozi.
Sasa nani mchawi hapo

USSR
 
Tukiwaambia Kenya na Ghana Wana Katiba nzuri mnatufokea hamtaki kujilinganisha na nchi nyingine. Tukiwaambia mfumuko wa bei ni mkubwa Wananchi Wana maisha magumu mnaleta hoja ya kulinganisha na nchi nyingine. Ila nyie ni wachawi, vigagula walozi.
Umemaliza mkuu
 
Sifa siyo kujifananisha matatizo na jirani zako ili uweze kuhalalisha visingizio, na pia kukwepa kuwajibika, sifa ni kukabiliana na changamoto ili uweze njia sahihi za ufumbuzi na kisha kuzitatua.

Sifa siyo kujifananisha na matatizo ya jirani yako aliyekuzidi maarifa na uwezo wa kiuchumi, na kisha kuanza kujifariji na kusema naye anapigika sawa sawa na wewe! Ukweli ni kuwa mnazungumza vitu tofauti na tena kupitia lugha mbili tofauti kabisa, na hata kwa hali na mali.

Msoto wa kiuchumi kwa wenzetu waliotuzidi maendeleo si sawa na wa hapa kwetu Bongo. Wakati viongozi wao ni wakweli na wanaumiza vichwa ili waweze kujinusuru, wa hapa kwetu ni waongo na wenye kutafuta visingizio ili tu wakwepe kuwajibika, kwa mtazamo finyu kuwa na hili nalo pia litapita kwa kudra za Mola.
 
Nimepata shule nzuri sana ya uchumi kutoka kwa mchumi. Dkt.Mwigulu anaitendea haki kweli taaluma ya uchumi
 
Tukiwaambia Kenya na Ghana Wana Katiba nzuri mnatufokea hamtaki kujilinganisha na nchi nyingine. Tukiwaambia mfumuko wa bei ni mkubwa Wananchi Wana maisha magumu mnaleta hoja ya kulinganisha na nchi nyingine. Ila nyie ni wachawi, vigagula walozi.
Waambie hata 2025 wafoke sana wasije wakapiga magoti wakatuudhi
 
Huyu jamaa kichwani sijui huwa amejaza Cow dung, msomi wa Phd mwenye uwezo duni wa kufikiri
 
Back
Top Bottom