Anheuser
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 1,944
- 667
Huyo shangazi hafai, hana upeo na busara za kibalozi. Kwa sababu katika siku ya kuadhimisha jambo ambalo kwa sasa ni nyeti na linaligawa Taifa, utaletaje mtu divisive, mtu controversial, kuja kuwa mgeni rasmi kwenye shughuli ya kibalozi? Mahala ambapo panatakiwa kuwa pa kujenga madaraja ya mahusiano? Hii inakuonyesha kwamba huyu Mama hana busara au hana wherewithal ya kukataa kupokea watu wanaotumwa na mamlaka za Dar-es-Salaam.anasema Balozi wa Tanzania nchini Marekani Bi Liberata Mulamula alishindwa kuhutubia kwa mpangilio kwa kuwa alikuwa amepakia Tungi (Amelewa) vibaya mno.
Balozi anaeheshimu jina lake na mwenye balls angewaambia mabosi wake Foreign au CCM Dodoma na Ikulu kwamba jamani msiniletee mtu kama Mwigulu nyakati hizi kwenye shughuli ya Muungano. Lakini hii ndio hulka ya Kikwete, sehemu nyeti anaweka wanawake watiifu au watu legelege ambao hawana gravitas, ili wawaburuze kirahisi, Hazina, Ulinzi, Sheria na Katiba, Balozi wa Marekani, Waziri Mkuu Pinda, wote ni schleps ambao hawawezi kumfunika wala kukataa upuuzi, hawana utashi kama vile waziri wake mkuu wa kwanza, alipokuwa hajajifunza.