Mkuu 'Econo', mimi siujui u-'smart' wa Mwigulu, lakini nimevutiwa sana na huo msemo chini ya jina lako.Mwigulu ni Waziri smart kuliko Mawaziri wote
"Agoal without a plan..." ukanifanya niyakumbuke mengi ya nchi yetu.
Nchi yetu inayo malengo, na wengi wa hao viongozi watakwambia 'plan' pia zipo kedekede.
Tulikuwa/tuna malengo ya 2025 tuliyojipangia toka 2020; na sasa yanatayarishwa mengine ya 2045(?), hata bila kujua haya tunayoyahitimisha tumeyatekeleza kwa ufanisi kiasi gani!
Bila kutaka kukuchosha, mkuu wangu, nadhani hayo maneno ya mstari huo chini ya jina lako hayatuhusu sisi. Sisi ni viumbe tofauti sana na hao wanaoweka malengo na kuainisha mipango ya kuyakamilisha hayo malengo.
Tatizo letu kubwa kama nchi linaanzia hapa, na natumaini kutakuwepo na siku utaleta mada hapa JF tuijadili kuhusu hayo maneno uliyoweka hapo.