Da Womanizer
JF-Expert Member
- May 24, 2010
- 1,577
- 148
Haya kazi kwako, ushaambiwa hapa YESU atakulinda.
ndibalema pole sana ndugu yangu.
Ondoa hofu maana umeiweka hapa hii hoja na ni jukumu letu kusaidiana.
Awali kabisa nakushairi usihame hapo unapoishi. Ila fanya yafuatayo.
Unapoingia kulala fanya sala (sikupi maneno ya kukariri ila vigezo vya sala) kwa mtiririko ufuatao.
nakwambia ukiomba kwa kuamini hakika ahsubuhi kesho utatuletea new story hapa.
- tumia dakika mbili mpaka tano ukimwomba msamaha mungu kwa yale yote uliyoyafanya kinyume na mapenzi yake.
- tumia dakika tano hadi saba au zaidi kuwaombea ndugu zako walale salama, na usisahau viongozi wa nchi walindwe mwombee ulinzi na huyo mwenyeji wako.
- tumia dakika tano hadi kumi kuomba mungu akupe ulinzi wewe utakapopanda kitandani, kataa ndoto za kishetani, kataa kutumiwa kichawi lakini kikubwa zaidi mweleze mungu kwamba unapokuwa unakitumia chumba hicho unavunja mikataba yoyote iliyowahi kufanywa ndani ya chumba hicho na nyumba hiyo, vunja mikataba yote ya kishetani ya kichawi hata ya kihalifu.
- mweleze mungu kuwa unapolala atume malaika walinzi wakulinde na walinde boma.
Kuhusu kuchanjwa just do it ktk maombi kuvunja mkataba na chain yoote iliyoungwa ili kukuconect. Kataa kwa jina la yesu nawe utakuwa salama, zaidi ya hapo tegemea maumivu.
Nb. Utakaposema uhame, huko uendako wanakungoja hakuna pa kujificha mbele ya shetani zaidi ya kumkimbilia mungu kupitia yesu kristo
@ Cheusi Mungu au Yesu? Maana naona kila mtu kasema Yesu sijajua nani ana nguvu zaidi kwa hao walio sema Yesu naomba nifahamishwe....