Mwenzenu hii mimba.......!

Mwenzenu hii mimba.......!

Kwa uelewa wangu mgumba ni mwanamke asiyekuwa na uwezo wa kuzaa. Hapo alipo mwenzangu yule hana tena uwezo wa kuzaa kwa hiyo ni mgumba. Na huo ugumba kajitengenezea mwenyewe kwa makusudi ati kwamba wawili alionao wanatosha basi mwenzangu akaenda kwenye huo utaalamu wa kujiharibu kizazi kwa hiyo sasa hivi hata angetaka ni hazai tena, sasa sio mgumba ni kitu gani. Nami namwambia kama hazai basi mwenzie nazaa, avute subra inshaallah wanawe watampata mdogo wao.

Da sophy mi kwako najifunza maneno tu!
 
Thanks Ledwin. Yaani Binadamu sisi ni very strange beings. Hivi huwa tunajaribu kutafuta justification for improper behaviour (amoral). Halafu ambapo nasikitika ni character bashing au personal vendetta.

Her degrees, her whatever - she is the legal and lawful wife period. Atleast that should be respected.

Its quite easy to score with a married man or woman, lakini score with a single available man or woman then be proud of that...

Hata uje na viingereza vya wapi habari ndiyo hiyo
 
Da sophy mi kwako najifunza maneno tu!

Maisha yenyewe mafupi dada kwa nini nijibanebane. Wa kunioa nimekosa, hata wa kunipenda jamani tena kaja mwenyewe na miguu yake nimkatae kwa sababu gani? La msingi tunapendana, na mtoto anahitaji wazazi wanaopendana. Nampenda ananipenda tumeridhiana, sihitaji zaidi, uzazi ni majaaliwa nalo pia nimejaaliwa nalo nikatae kisa?
 
unajua mpo wangapi? akisema yupo kwa mkewe unauhakika anakuwa huko au anakuwa kwa mwingine kama wewe?

Huko kwa mkewe wapi? Au unamaanisha kule alikoweka cheti cha ndoa? Halohaloooo! Mimi sihitaji cheti nahitaji mwanaume ambaye ndiye huyu niko naye shida iko wapi?
 
Da Sophy, I'm diggin' your gusto in being a jump off......that's what's up!
 
Duh..kumbe mambo ya kutumia "ndumu" ni kitendawili cha kale sana kwa wengi...unaachije wazi wazi mzigo kwa mtu mwenye familia yake mpaka mimba!!!!, salalaaaaa!! khaha...

YouTube - Kosa la marehemu (remix)_Uswahilini Matola

sasa tukitumia hizo ndumu unazosema uzazi utapatikana wapi? Mimi pia ni sehemu ya familia yake kwa hiyo unaposema mwenye familia umeshanihesabu humo tayari.
 
sasa tukitumia hizo ndumu unazosema uzazi utapatikana wapi? Mimi pia ni sehemu ya familia yake kwa hiyo unaposema mwenye familia umeshanihesabu humo tayari.

hapo nimekusoma

hivi da sophy, sasa inakuwaje jamaa akitaka kwenda kwa mkewe wa makaratasi? (wa ndoa) unampa muda au inakuwaje?
 
hapo nimekusoma

hivi da sophy, sasa inakuwaje jamaa akitaka kwenda kwa mkewe wa makaratasi? (wa ndoa) unampa muda au inakuwaje?
BHT hapa kuna cha mda kweli...hii ni nonstop...
Labda jamaa ajiibe ili angalau apite home kuwajulia hali...then fasta kwa da sophy...
 
BHT hapa kuna cha mda kweli...hii ni nonstop...
Labda jamaa ajiibe ili angalau apite home kuwajulia hali...then fasta kwa da sophy...

duh, yanipishie mbali!!!
 
mnh wakina da sophy wote washindwe.ndio nyie mnasambaratisha familia za watu,afu mnaona ni ufahari.muone na majibu yake utajua ni mjeuri.sio ujanja kubomoa familia ya mtu.wanaume wapo kibao kama unataka mtoto kwa nini usijilengeshe kwa hao wako single?
 
mnh wakina da sophy wote washindwe.ndio nyie mnasambaratisha familia za watu,afu mnaona ni ufahari.muone na majibu yake utajua ni mjeuri.sio ujanja kubomoa familia ya mtu.wanaume wapo kibao kama unataka mtoto kwa nini usijilengeshe kwa hao wako single?
Akikosa wa kumwoa afanyaje Fab??? Surely she can't 'fast' forever..
 
Back
Top Bottom