Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Thanks!!!!!!!Heshima yako kaka Billy.
Nakupongeza kwa ujasiri wako wa kuthubutu kuandika juu ya chama chenye wapenzi wengi sana nchini. Una uthubutu.......
Ngoja nikuonyeshe ulitakiwa kufanya nini kabla hujaandika. Itakusaidia sana siku za usoni. Unaposema....
- Mwenyekiti wa Chama cha kuwakomboa wananchi, anapotumia magari kama ya watawala, inasema nini kuhusu huu ukombozi? VX8, tena sio moja, Wasaidizi, Dreva, MABENDERA, KUCHELEWA KUFIKA UWANJANI, bado hajashika nchi, je akishika tutegemee nini tofauti, maana haya si ndio ya kawaida kwa watawala? Kwenye kuvaa kombati sawa lakini mengine hayo mbona sawa na watawala?
- Umeonyesha kuwa upeo wako unahusisha utekelezaji wa sera zenye kasoro na kutumia magari ya kifahari, walinzi, bendera na kubwa zaidi dereva as if magari yalitakiwa yawe co piloted (labda unaangalia sana sinema za sciencefiction)
- Bendera ni identity! Hata wakati ukiwa baharia wa meliza SINOTASHIP, nazo zilikuwa na bendera
- Walinzi ni jambo liko wazi kabisa unless uwe unalindwa na watu wasioonekana kama alivyosema mtabiri Fulani
- Kimoyoni uko Chadema nadhani maana umependa kombati!
- NAOMBA KUTOA HOJA, MAANA WAKOMBOZI KINA CASTRO, CHE GUEVARA, MAO, NA SAVIMBI HATUKUWAONA NA MA-VX8, AU WASAIDIZI AU NI UKOMBOZI TOFAUTI?
- Itabidi ukae chini usome tofauti kati ya political party na resistance movement. Unachanganya masomo. Tafuta kitabu kinaitwa Waging Nonviolent Struggle: 20th Century Practice and 21st Century Potential cha Gen Sharp. Utajua kwanini siku hizi hakuna mapinduzi kama zamani. Lazima ujue kutofautisha zama, madhumuni ya mapambano na watu walio katika mfumo
- KUONGOZA SI NI MFANO ZAIDI? MUNGU AIBARIKI TANZANIA!
USHAURI:
- Kuongoza ni mfano zaidi. Sasa wewe ambaye ulitaka kuongoza halafu unamiss such basic stuff? Haiyumkini kura hazikutosha
- Soma sana uongeze maarifa. Kwa sasa, umepwaya sana. Kama itakupendeza….tutakusaidia vitu vya kusoma
- Take time to think kabla hujasema au kuandika. Maandishi huwa hayafutiki. Tutakuja kukuonyesha what you wrote ukiwa popote pale unagombea nafasi yeyote ile. Hili ni la muhimu sana kuzingatia
- Wahenga walisema " A silent fool is counted wise"