Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Arusha, Elisa Mungure, ametoa wito kwa Mwenyekiti Mstaafu wa chama hicho ngazi ya taifa, Freeman Mbowe, kujitokeza hadharani na kuunga mkono kaulimbiu ya chama ya “No Reforms, No Election”, kwa kuwa ndiye mwanzilishi wa msimamo huo.
Mungure amesema kauli mbiu hiyo ilianza kutumika chini ya uongozi wa Mbowe akiwa Mwenyekiti wa Taifa, ambapo ilipitishwa na Kamati Kuu ya CHADEMA na kusambazwa kwa mikoa yote ya chama hicho.
Amesema: “No Reforms, No Election imeanzia kwa Freeman Mbowe. Nikiwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa, nililipokea kama agizo la Kamati Kuu. Kwa hiyo kiukweli anatakiwa atoke na aseme kauli hiyo kwa sababu yeye ni kati ya waasisi wa msimamo huo.”
Ameongeza kuwa Mbowe ni miongoni mwa viongozi waliopambana kwa dhati kuhimiza mageuzi ya kisiasa nchini, hivyo ushiriki wake wa moja kwa moja katika kusimamia kauli mbiu hiyo ni muhimu kwa mustakabali wa demokrasia.
Ikumbukwe kwamba Mungure alikuwa miongoni mwa viongozi wa CHADEMA waliomuunga mkono Mbowe wakati wa kampeni za uchaguzi wa ndani wa chama hicho.
Mungure amesema kauli mbiu hiyo ilianza kutumika chini ya uongozi wa Mbowe akiwa Mwenyekiti wa Taifa, ambapo ilipitishwa na Kamati Kuu ya CHADEMA na kusambazwa kwa mikoa yote ya chama hicho.
Amesema: “No Reforms, No Election imeanzia kwa Freeman Mbowe. Nikiwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa, nililipokea kama agizo la Kamati Kuu. Kwa hiyo kiukweli anatakiwa atoke na aseme kauli hiyo kwa sababu yeye ni kati ya waasisi wa msimamo huo.”
Ameongeza kuwa Mbowe ni miongoni mwa viongozi waliopambana kwa dhati kuhimiza mageuzi ya kisiasa nchini, hivyo ushiriki wake wa moja kwa moja katika kusimamia kauli mbiu hiyo ni muhimu kwa mustakabali wa demokrasia.
Ikumbukwe kwamba Mungure alikuwa miongoni mwa viongozi wa CHADEMA waliomuunga mkono Mbowe wakati wa kampeni za uchaguzi wa ndani wa chama hicho.