Mwenge stend leo ni vunja bomoa ondoa

Mwenge stend leo ni vunja bomoa ondoa

si umesema mji lazima ujengwe kwa kuzingatia mipango, na wao wawe wamepata vibali kutoka kwa mamlaka husika..,hao watoa vibali na mamlaka husika au wanaohusika na mipango miji ni nani kama sio SERIKALI?....USIWE KICHWA MAJI yani kama tz tuna mijitu mingi isiyofikiria kama wewe itachukua mda mrefu sana hadi kuendelea

Kwamba mji ni lazima ujengwe kwa kuzingatia mipango, na ni lazima kuwe na mamlaka husika bado haijamaanisha kwamba Tanzania kuna serikali.

Inawezekana mji haufuati mipango kwa sababu mamlaka husika hazifanyi kazi, in an endless vicious cycle of degeneration.

Yours is a logical non-sequitur.

Nikisema nafanya party, all white affair, kuja ni lazima uwe umevaa nguo nyeupe, hilo halimaanishi nimesema unayo nguo nyeupe. Inawezekana huna na tangazo langu litakusaidia kununua nguo nyeupe uje kwenye party.

Unachosema wewe ni kwamba, kwa vile nimesema kuja kwenye party ni lazima uvae nguo nyeupe, basi nimesema unayo nguo nyeupe.

Tofauti.

Kuna mjinga mwingine alinitukana kwa kuniita kichwa maji hivyo hivyo kama wewe.

Wataalam wa ubongo wanasema ubongo una maji takriban 78%

Nani anakurupuka sasa?

Labda kichwa chako kina ukosefu wa maji.
 
Mwenge kuwa kituo siku zake zikocouning its better Wafanyabiashara wakajipanga kuja mitaa ya makumbusho mapema.
 
Posta Mpya na Kariakoo nako nimeona kuna safisha safisha imefanywa...

Pembeni ya Soko Kuu la Kariakoo mbele ya duka la Tahfif kulikuwa na soko mshenzi, naona limevunjwa na pale mahali ni safi hata kabumbu unaweza lisakata...
 
... na lengo la serekali ni kuongeza ajira nchni,chukuen ushauri wangu huu hapa,nnsf wapewe eneo hilo wajenge kituo na majengo meng ya biashara ya kisasa,ili mkusanye kodi nyie wenyewe baada ya huyo babu kesi,ilo linawezekana,lengo letu n kupiga hatua kimaendeleo
Hawa hata wakijengewa jengo hawahamii, solution ni kuwatimua tu warudi mikoani. Huwezi ukaharibu utaratibu wa jiji halafu watu wakawa wanaona tu. Big up City Authorities, go ahead, go!
 
Kosa moja halihalalishi kufanyika kwa kosa jingine. Kama mamlaka za Jiji zilizembea kuzuia ujenzi holela, hilo ni kosa, lakini haina maana kwamba mtu mwingine ana ruhusa ya kufanya kosa la kujenga bila utaratibu!

Sawa, kosa moja halihalalishi kosa jingine. Lakini haki iko wapi?

Hao wengine waliofanya makosa mbona hatuoni wala kusikia na wao wakichukuliwa hatua?

Nani kafukuzwa kazi kwa kushindwa kufanya kazi yake? Nani kachukuliwa hatua za kisheria kwa kuruhusu au kuzembea hadi watu wakajenga vibanda sehemu ambazo hawatakiwi?

Miaka nenda rudi hivyo vibanda vimekuwepo hapo. Wahusika wako wapi?

Unajua wakati mwingine watu wakiona haki inatendeka hata kulalama kwamba wanaonewa wanaweza wasifanye.

Lakini haya mambo ya kuwaadhibu wanyonge (kwa kinachodhaniwa ni makosa yao) halafu watu wengine (vibosile) wakikosea hatuoni wakichukuliwa hatua stahilifu kwa makosa yao, lazima tupige kelele za uonevu.

Si sawa hata kidogo walichokifanya.
 
Posta Mpya na Kariakoo nako nimeona kuna safisha safisha imefanywa...

Pembeni ya Soko Kuu la Kariakoo mbele ya duka la Tahfif kulikuwa na soko mshenzi, naona limevunjwa na pale mahali ni safi hata kabumbu unaweza lisakata...

Atakuwa anakuja David Cameruni hivi karibuni rais alienda kumkaribisha Juzi kati
 
Leo ukifika MWENGE lazima ushangae kwani ni kweupeee hakuna msongamano wa watu wala daladala stendi ni nyeupe mpaka raha.
hakuna kukanyagana tena wala kupigana vikumbo.

Leo asubuhi na mapema polisi FFU na baadhi ya mgambo wameendesha operation ya bomoa bomoa meza na mabanda yote ya wamachinga yaliyopo ndani nje nayaliyo karibu na MWENGE STENDI.

kiukweli wamefanya KAZI nzuri sana hasa ni baada yakuzifuata mpaka meza zilizokuwepo zimehifadhiwa.

sababu wangeziacha jioni wanazibeba na kujakufungua biashara na kuwapa pesa watu wanaojiona kama MWENGE STENDI ni yakwao Mali yao wakiongozwa na babu kesi.

haina jinsi wakulaum mtalaum ila inabidi tukubali tu kuwa kitu kisipokuwa mahari pake ni uchafu.

kuna watu wanalipa mamilioni ya kodi ila hawa wangine kodi yao wanalipa kwa KESI yeye ndio tra WA mwenge

Hata Kariakoo, Temeke, Mbagala Hali Ni Hiyohiyo Kwakweli Kunapendeza Mno! Lakini Ni Muhimu Wakatafutiwa Sehemu Za Kwenda La Sivyo...!
 
Nipi week mtaona hali itarudi kama kawaida kinachofanyika pale hao wanoweka mabanda pale wanalipa kiasi fluni kwa qale waaimamizi kila siku iki wendelee na biashara yao pale.

Kurunzi Kwa Vyovyote Unatumia Screen Touch Na Bado Hujawa Mtaalam Nayo
 
Hawa hata wakijengewa jengo hawahamii, solution ni kuwatimua tu warudi mikoani. Huwezi ukaharibu utaratibu wa jiji halafu watu wakawa wanaona tu. Big up City Authorities, go ahead, go!

Wengine tumezaliwa na tumekulia town mnataka twende wapi! "metupa hasara kubwa lakini tutabounce back! Labda mtupeleke maisha mabovu!
 
Nami nampongeza sana zembwela. Pia napongeza uamuzi wa kuzuia bodaboda na bajaj katikati ya jijj. Lazima tuwe na utaratibu ili nasi tuonekane wastaarabu. [color =red ]Jiji gani kila mahali kunanuka?[/color] Jiji gani milokoteni inaingia hadi katikati ya jiji? Inawezekana kabisa kuwa na miji na majiji yaliyopangiliwa.

Mkuu unaamini kwa kufungia bodaboda kuingia katikati ya jiji kutapunguza harufu mbaya.?
 
Tatizo serikali yetu ni kurupukaji tu Haina mipango endelevu.!
 
Serikali imechemka ingetafuta mbinu mbadala ya hawa watu vitendo vya ualifu vitaongezeka sasa
 
Khaaah!ss inaman zembwl alijua huo ujio?!
Kwl km tu mtot ni mchafu akion wazazi ndo anakimbia kukoga nchi ni hatareeeee.....
Usafi mpk mtu mkubwa awe anakuja...nomaaa...
Shkmoo zembwela lkn.
 
namkubali sana kaka yangu zembwela ila kwa hili yupo wrong na hao waliovunja..,.mnajua madhara yake, ngojeni roba za mbao, kuibiwa visim vyenu

kwahiyo nyie mnataka ufanyike ujinga kuogopa roba??

hii haikubaliki kabisaaa mwisho WA siku mtatuambia tuukubali ushoga kwa kuogopa kutopewa misaada??

kila kitu inatakiwa kiwe na utaratibu wake hivi inakuwaje machangudoa wakienda kujiuza kanisani au wafuga nguruwe wakafugie msikitini??
 
TUKIO KATIKA PICHA: BOMOA BOMOA YA VIBANDA VYA BIASHARA MWENGE LEO, MAKUBWA YAVUMBUKA.!

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetublogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

SIKILIZA TONE RADIO HAPA


[video]<iframe width="480" height="302" src="http://www.ustream.tv/embed/9555115?v=3&wmode=direct" scrolling="no" frameborder="0" style="border: 0px none transparent;">    </iframe> <br /><a href="http://www.ustream.tv/" style="padding: 2px 0px 4px; width: 400px; background: #ffffff; display: block; color: #000000; font-weight: normal; font-size: 10px; text-decoration: underline; text-align: center;" target="_blank">Live streaming video by Ustream</a>[/video]


Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com


Ilikuwa Mida ya Saa tatu za asubuhi ambapo Magari zaidi ya 10 ya Jiji yalikuwa yamejipanga eneo la mwenge Huku kukiwa na Ma Askari wa FFU wa kutosha pamoja na Migambo wa Jiji huku wakiongozwa na watu wa Jiji kwa ajili ya Kukamilisha swala zima la bomoa bomoa vibanda vyote ambavyo havina mpangilio.. zoezi hilo lilianza kwa utulivu na kuendelea kwa utulivu kutokana na ulinzi mkubwa uliokuwepo huku wananchi wakiendelea na kazi zao kama kawaida na kukatazwa kukatiza katika eneo la tukio kwa usalama wao..

Hata hivyo Baada ya vibanda hivyo kutolewa kumegundulika kuwa kulikuwa ni kuchafu kupindukia kutokana na uchafu uliokuwa umezagaa kila kona..

Kulia ni Magari mbalimbali ya Serikali yakiwa yamepaki eneo la Mwenge huku zoezi likiendelea



Hili ni eneo la ndani ya Mwenge ambapo wamebomoa vibanda vyote


Akina Mama eneo la Mwenge ndani ndani kiasi wakiwa wanahaha huku wakihangaika kutoa vitu vyao baada ya Bomoa Bomoa kupita... Hawa ni wale wauza Chai na Supu asubuhi
Huwezi amini lakini ndio hali halisi sasa eneo jirani na Kituo cha Mabasi Mwenge hakuna tena Adha ya vibanda , lakini umebaki uchafu uliopitiliza na kugundulika kuwa hawa watu walikuwa wakifanya Biashara katika maeneo ambayo si salama
Hili ni eneo ambalo lilikuwa ni Maarufu kwa ajili ya kuuza vitu mbalimbali kama mitumba na viatu lakini kwa sasa hakuna kitu ni peupe


Huu ni uchafu uliopitiliza
wakiendelea kukusanya mabaki ya Mabanzi katika eneo hilo la mwenge
Kwa wale akina dada hili lilikuwa eneo maarufu sana kwa ajili ya Kutengenezea nywele na saloon bubu ambazo zote zimevunjwa vunjwa kwa sasa
Hapa juu mwanzo kulikuwa na mabanzi ya kutosha na wakina dada wengi walikuwa wanapenda kuwa hapa wakitengenezwa nywele zao wasijue kuwa walikuwa wakikaa katika eneo chafu kama hili.
Gari hili likijiandaa kuondoka baada ya somba somba
Kwa kuliangalia Eneo hili utasema ni chafu sana lakini ndio ambalo lilikuwa maarufu hasa kwa akina mama na akina dada kutengenezea kucha zao na kusuguliwa miguu, Je kama wangejua ni pachafu hivi wangeweza kugusa hata kuja kutengeneza kucha?


Bomoa bomoa ikiendelea

Baada ya kufanya manunuzi watu hutupa takataka tuu, zilikuwa zikijificha kulingana na mkusanyiko wa watu lakini hii ndio hali halisi sasa


Hakuna Vibanda lakini adha imebakia sasa ni ya uchafu
Je hapa tutapona magonjwa ya mlipuko?
Peupe hata kuna nafasi ya kutembea kwa miguu
Huu ni upande wa pili wa kuelekea Mikochemi ambapo bajaji Hupaki napo wamesafisha kwa kubomoa vibanda vyote hapa ni Shwari peupe



Picha hizi mbili ni eneo maarufu sana ambapo watu walikuwa wanauza Vifaa vya umeme na DVD, Sub Woofer pamoja na Radio bila kusahau TV sasa pamebaki kama hivi, Je walikuwa hawajui kama ni pachafu kiasi hiki?
Mgambo wakiwa wamemaliza kazi yao hapa ......

Picha na Pamoja Blog/ Dar es salaam yetu Blog
 
Mkuu unaamini kwa kufungia bodaboda kuingia katikati ya jiji kutapunguza harufu mbaya.?

hili inabidi tulikubali tuu haiwezekani kabisa njia kubwa kama morogoro rod ikawa na bajaji na pikipiki.
katikati ya jiji watu wanaingia na bajaji na pikipiki.waanze kwa hawa then ikiwezekana na wale wenye magari nao waingie mjini kwakuyalipia.coz foleni zingine huwanizakujitakia.
 
Loo naionea huruma ile mijanaume mibonge ya pale getini ambayo badala ya kukaa getini ,imekuwa ikikusanya hela za mle ndani ya stand,sijui itakula nini sasa kama wamachinga wameondolewa,au Obama karibu anakuja TZ
 
Back
Top Bottom