Nami nampongeza sana zembwela. Pia napongeza uamuzi wa kuzuia bodaboda na bajaj katikati ya jijj. Lazima tuwe na utaratibu ili nasi tuonekane wastaarabu. Jiji gani kila mahali kunanuka? Jiji gani milokoteni inaingia hadi katikati ya jiji? Inawezekana kabisa kuwa na miji na majiji yaliyopangiliwa.Nyie msalimieni zembwela tu badala ya kuomboleza raba za mbao mtakazo pigwa mtaani wale watu wakikosa ajira!
mwenge imetakata kabisa baada ya kipindi cha east africa radio kinachoendeshwa na mwanahabari zembwela kukaripia kwa ukali sana uchafu na uwekaji mabanda pale mwenge stendi leo kumesafishwa kupo safi.ama kweli taaluma ya habari ikitumiwa vizuri huwa inaleta manufaa papo hapo. Asante zembwela kwa kalipio lako.
Mleta mada umeandika kama we ndio uloendesha oparesheni
mi nadhani pale mwenge n center nzur kwa biashara na lengo la serekali ni kuongeza ajira nchni,chukuen ushauri wangu huu hapa,nnsf wapewe eneo hilo wajenge kituo na majengo meng ya biashara ya kisasa,ili mkusanye kodi nyie wenyewe baada ya huyo babu kesi,ilo linawezekana,lengo letu n kupiga hatua kimaendeleo
Mwenge imetakata kabisa baada ya kipindi cha East Africa radio kinachoendeshwa na mwanahabari zembwela kukaripia kwa ukali sana uchafu na uwekaji mabanda pale mwenge stendi leo kumesafishwa kupo safi.
Ama kweli taaluma ya habari ikitumiwa vizuri huwa inaleta manufaa papo hapo.
Asante zembwela kwa kalipio lako.
Tatizo la serikali yetu ni kufanya mambo kama zima moto. Watajidai endelevu baada ya wiki moja utaona kimya na watu watarudi kwenye maeneo hayo kwa nguvu. Hata kwenye mafuriko ni hivyo hivyo. Mpaka mvua inyeshe ndipo utasikia kauli za kuwataka wahame. Wakati wa kiangazi wanawaona kabisa wakijenga hawasemi kitu. Imekuwa ni serikali ya matukio. Walipaswa pia kufanya doria hata usiku kwani kuanzia saa 1 ndipo biashara huanza kusogezwa maeneo yasiyoruhusiwa.