TANZIA Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei afariki Dunia

TANZIA Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei afariki Dunia

Kila nafsi itakutwa na mauti.No more no less. Muda ukifika ndio umefika hakuna cha laana wala matambiko.
 
Wakuu,

Heche kupitia mtandaoni ametangaza kifo cha mwasisi wa chama chao CHADEMA, Mzee Edwin Mtei baada ya familia kuthibitisha huku mipango ya mazishi ikiendelea nyumbani kwake Tengeru, Arusha.

=====

View attachment 3532056

Baadhi ya mambo muhimu kuhusu Ediwin Mtei ambayo pengine ulikuwa hufahamu

Elimu,"Shahada ya Sanaa (Political Science, History, Geography) - Makerere (1957)"
BoT, Gavana wa kwanza (1966–1974)
Uwaziri, Waziri wa Fedha (1977–1979)
Siasa, Muasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA (1992)
Tawasifu, From Goatherd to Governor (2009)

1. Safari ya "Kutoka Chini"
Mtei alizaliwa mwaka 1932 huko Marangu, Moshi. Katika tawasifu yake (autobiography) iitwayo "From Goatherd to Governor", anaelezea jinsi alivyokulia katika mazingira duni, akichunga mbuzi baada ya masomo ya "bush school". Alisoma katika shule za Old Moshi na Tabora Boys kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwaka 1953.

2. Gavana wa Kwanza wa Benki Kuu (BoT)
Wengi wanaijua CHADEMA, lakini hawajui kuwa Mtei ndiye alikuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakati ilipoanzishwa mwaka 1966. Alisimamia mchakato wa kwanza wa kutoa sarafu ya Tanzania (shilingi) baada ya kuvunjika kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki. Alishikilia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minane (1966–1974).

3. Msuguano na Mwalimu Nyerere
Mtei alikuwa Waziri wa Fedha katika serikali ya Mwalimu Julius Nyerere. Hata hivyo, alijiuzulu nafasi hiyo mwaka 1979 kutokana na kutofautiana na Nyerere kuhusu sera za kiuchumi, hasa mapendekezo ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ambayo Nyerere aliyakataa. Kitendo chake cha kujiuzulu kwa hiari kilihesabika kama ujasiri mkubwa wa kimaslahi wakati huo.

4. Nyadhifa za Kimataifa
Kabla ya kuingia kwenye siasa za ushindani, alihudumu kama Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na pia alifanya kazi katika Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kama Mkurugenzi Mtendaji (Executive Director) akiwakilisha kundi la nchi za Kiafrika.

5. Kuasisi CHADEMA
Baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa mwaka 1992, Mtei alikuwa mmoja wa waasisi wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Alihudumu kama Mwenyekiti wa kwanza wa chama hicho na alitumia rasilimali zake na ushawishi wake kukijenga tangu kikiwa kidogo hadi kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.

6. Uhusiano wa Kifamilia na Freeman Mbowe
Jambo ambalo wengi hulitolea macho ni uhusiano wake na aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Edwin Mtei ni mkwe wa Freeman Mbowe (Mbowe amemuoa binti wa Mtei, Lillian). Hii mara nyingi imekuwa ikitumiwa na wapinzani wao wa kisiasa, lakini ndani ya chama inaonekana kama muendelezo wa misingi aliyoiweka.
My sincere condolences.
 
RIP Mzee Edwin Mtei. Poleni sana familia, ndugu, marafiki, waTanzania na wanachama wote wa CHADEMA

1768900495654.jpeg

Picha maktaba: Mzee Edwin Mtei.
 
Wakuu,

Heche kupitia mtandaoni ametangaza kifo cha mwasisi wa chama chao CHADEMA, Mzee Edwin Mtei baada ya familia kuthibitisha huku mipango ya mazishi ikiendelea nyumbani kwake Tengeru, Arusha.

=====

View attachment 3532056

Baadhi ya mambo muhimu kuhusu Ediwin Mtei ambayo pengine ulikuwa hufahamu

Elimu,"Shahada ya Sanaa (Political Science, History, Geography) - Makerere (1957)"
BoT, Gavana wa kwanza (1966–1974)
Uwaziri, Waziri wa Fedha (1977–1979)
Siasa, Muasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA (1992)
Tawasifu, From Goatherd to Governor (2009)

1. Safari ya "Kutoka Chini"
Mtei alizaliwa mwaka 1932 huko Marangu, Moshi. Katika tawasifu yake (autobiography) iitwayo "From Goatherd to Governor", anaelezea jinsi alivyokulia katika mazingira duni, akichunga mbuzi baada ya masomo ya "bush school". Alisoma katika shule za Old Moshi na Tabora Boys kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwaka 1953.

2. Gavana wa Kwanza wa Benki Kuu (BoT)
Wengi wanaijua CHADEMA, lakini hawajui kuwa Mtei ndiye alikuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakati ilipoanzishwa mwaka 1966. Alisimamia mchakato wa kwanza wa kutoa sarafu ya Tanzania (shilingi) baada ya kuvunjika kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki. Alishikilia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minane (1966–1974).

3. Msuguano na Mwalimu Nyerere
Mtei alikuwa Waziri wa Fedha katika serikali ya Mwalimu Julius Nyerere. Hata hivyo, alijiuzulu nafasi hiyo mwaka 1979 kutokana na kutofautiana na Nyerere kuhusu sera za kiuchumi, hasa mapendekezo ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ambayo Nyerere aliyakataa. Kitendo chake cha kujiuzulu kwa hiari kilihesabika kama ujasiri mkubwa wa kimaslahi wakati huo.

4. Nyadhifa za Kimataifa
Kabla ya kuingia kwenye siasa za ushindani, alihudumu kama Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na pia alifanya kazi katika Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kama Mkurugenzi Mtendaji (Executive Director) akiwakilisha kundi la nchi za Kiafrika.

5. Kuasisi CHADEMA
Baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa mwaka 1992, Mtei alikuwa mmoja wa waasisi wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Alihudumu kama Mwenyekiti wa kwanza wa chama hicho na alitumia rasilimali zake na ushawishi wake kukijenga tangu kikiwa kidogo hadi kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.

6. Uhusiano wa Kifamilia na Freeman Mbowe
Jambo ambalo wengi hulitolea macho ni uhusiano wake na aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Edwin Mtei ni mkwe wa Freeman Mbowe (Mbowe amemuoa binti wa Mtei, Lillian). Hii mara nyingi imekuwa ikitumiwa na wapinzani wao wa kisiasa, lakini ndani ya chama inaonekana kama muendelezo wa misingi aliyoiweka.
Nice fupi na inaeleweka historia ya Mzee mtei
 
Mtei alikataa ujinga wa sera za ujamaa zilizofilisi nchi huku viongozi wakineemeka na ndiyo sababu ya yeye kupingana na Nyerere na hatimaye kuondoka Serikalini
Huo ubepari alioutaka unaihangaisha dunia nzima hivi sasa, maandamano kila kukicha huko USA maana yake sera hizo pia zinafeli tena kwa kasi.
 
Nasikia Samia ametuma salamu za rambirambi. Kiprotokali, ilitakiwa aiaddress kwa Mwenyekiti wa sasa wa CHADEMA. Sijui kama protokali imezingatiwa.
 
Nchi imempoteza mwamba wa demokrasia. Apumzike kwa amani, mzee Mtei.
Hata hivyo, kisha kula chumvi nyingi sana! Dunia yetu ilivyo kwa sasa, watu wakifikia nusu tu ya umri aliofikia mzee Mtei, wameshachoka kinyama!
 
Zilizoungwa mkono au zilizopingwa?..

Mzee Mtei (Rip) na Ujamaa ni maji na mafuta .
Angalau zilitambulika kitaifa na kimataifa kuliko wengi wenye akili nyingi na mawazo mazuri wanaokwenda nayo kaburini.

Alikuwa waziri wa fedha nafasi ambayo aliweza kuchangia maarifa yake kwa ukuaji wa Tanzania ya miaka ile ya 70 mwishoni.
 
Ulielewa tofauti na hii huenda ni kwa sababu mentor wako anaweza kuwa Kihongosi.
Watu wote wanajua kila mtu atakufa ila kuna watu wakifa ni afadhali na wengine wakifa ni majonzi, mfano rahisi kama ulipoolewa wakwe zako inawezekana waliona wameletwa majanga na matatizo kwa roho yako mbaya ya kuchukia ndugu wa mume na wakati Kuna shoga yako alipoolewa imekuwa furaha tupu kwa wakwe zake lakini zote ni ndoa.
Pole kwa maumivu lakini "Wema hawafi" 🤓
 
Back
Top Bottom