TANZIA Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei afariki Dunia

TANZIA Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei afariki Dunia

Sumu utakuwa wewe unayepinga hata usichokielewa.
Hujui ninachopinga?
Ngoja basi nikueleze tena kwa mara nyingine hapa; na naomba tafadhali usidai tena kuwa sijui ninachopinga.

Ninapinga Samia Suluhu Hassan kulazimisha yeye na genge lake kuwatawala waTanzania bila ya ridhaa yao.

Sikubaliani na njia zote anazotumia kuwakandamiza waTanzania ili aendelee kuwatawala kwa nguvu.

Samia Suluhu Hassan hajachaguliwa kihalali kuongoza taifa hili; kwa hiyo napinga juhudi zote zinazofanyika kuhalalisha utawala HARAMU, na shughuli zote zinazotekelezwa na serikali isiyokuwa HALALI..

Kwa maovu yote aliyofanya Samia na Genge lake, ni lazima pawepo na njia ya kuwawajibisha wote waliohusika katika kutekeleza maovu hayo dhidi ya waTanzania.

Hatuwezi kwa njia yoyote kuwasafisha waovu ili waendelee kukaa madarakani isivyokuwa halali.

Usirudie tena kuandika upuuzi kama huo ulioweka hapo juu.
 
Pamoja na mambo mengi lazima uyu mzee
Wakuu,

Heche kupitia mtandaoni ametangaza kifo cha mwasisi wa chama chao CHADEMA, Mzee Edwin Mtei baada ya familia kuthibitisha huku mipango ya mazishi ikiendelea nyumbani kwake Tengeru, Arusha.

=====

View attachment 3532056

Baadhi ya mambo muhimu kuhusu Ediwin Mtei ambayo pengine ulikuwa hufahamu

Elimu,"Shahada ya Sanaa (Political Science, History, Geography) - Makerere (1957)"
BoT, Gavana wa kwanza (1966–1974)
Uwaziri, Waziri wa Fedha (1977–1979)
Siasa, Muasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA (1992)
Tawasifu, From Goatherd to Governor (2009)

1. Safari ya "Kutoka Chini"
Mtei alizaliwa mwaka 1932 huko Marangu, Moshi. Katika tawasifu yake (autobiography) iitwayo "From Goatherd to Governor", anaelezea jinsi alivyokulia katika mazingira duni, akichunga mbuzi baada ya masomo ya "bush school". Alisoma katika shule za Old Moshi na Tabora Boys kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwaka 1953.

2. Gavana wa Kwanza wa Benki Kuu (BoT)
Wengi wanaijua CHADEMA, lakini hawajui kuwa Mtei ndiye alikuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakati ilipoanzishwa mwaka 1966. Alisimamia mchakato wa kwanza wa kutoa sarafu ya Tanzania (shilingi) baada ya kuvunjika kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki. Alishikilia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minane (1966–1974).

3. Msuguano na Mwalimu Nyerere
Mtei alikuwa Waziri wa Fedha katika serikali ya Mwalimu Julius Nyerere. Hata hivyo, alijiuzulu nafasi hiyo mwaka 1979 kutokana na kutofautiana na Nyerere kuhusu sera za kiuchumi, hasa mapendekezo ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ambayo Nyerere aliyakataa. Kitendo chake cha kujiuzulu kwa hiari kilihesabika kama ujasiri mkubwa wa kimaslahi wakati huo.

4. Nyadhifa za Kimataifa
Kabla ya kuingia kwenye siasa za ushindani, alihudumu kama Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na pia alifanya kazi katika Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kama Mkurugenzi Mtendaji (Executive Director) akiwakilisha kundi la nchi za Kiafrika.

5. Kuasisi CHADEMA
Baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa mwaka 1992, Mtei alikuwa mmoja wa waasisi wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Alihudumu kama Mwenyekiti wa kwanza wa chama hicho na alitumia rasilimali zake na ushawishi wake kukijenga tangu kikiwa kidogo hadi kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.

6. Uhusiano wa Kifamilia na Freeman Mbowe
Jambo ambalo wengi hulitolea macho ni uhusiano wake na aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Edwin Mtei ni mkwe wa Freeman Mbowe (Mbowe amemuoa binti wa Mtei, Lillian). Hii mara nyingi imekuwa ikitumiwa na wapinzani wao wa kisiasa, lakini ndani ya chama inaonekana kama muendelezo wa misingi aliyoiweka.
fika kesho kutwa udhuria mazishi yake , lazima , Mzee kaacha legacy kubwa ndani ya haki.

Mtu wa kwanza nikifika lazima kumpa Mbowe pole maana mkwe wake uyu.
 
Wakuu,

Heche kupitia mtandaoni ametangaza kifo cha mwasisi wa chama chao CHADEMA, Mzee Edwin Mtei baada ya familia kuthibitisha huku mipango ya mazishi ikiendelea nyumbani kwake Tengeru, Arusha.

=====

View attachment 3532056

Baadhi ya mambo muhimu kuhusu Ediwin Mtei ambayo pengine ulikuwa hufahamu

Elimu,"Shahada ya Sanaa (Political Science, History, Geography) - Makerere (1957)"
BoT, Gavana wa kwanza (1966–1974)
Uwaziri, Waziri wa Fedha (1977–1979)
Siasa, Muasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA (1992)
Tawasifu, From Goatherd to Governor (2009)

1. Safari ya "Kutoka Chini"
Mtei alizaliwa mwaka 1932 huko Marangu, Moshi. Katika tawasifu yake (autobiography) iitwayo "From Goatherd to Governor", anaelezea jinsi alivyokulia katika mazingira duni, akichunga mbuzi baada ya masomo ya "bush school". Alisoma katika shule za Old Moshi na Tabora Boys kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwaka 1953.

2. Gavana wa Kwanza wa Benki Kuu (BoT)
Wengi wanaijua CHADEMA, lakini hawajui kuwa Mtei ndiye alikuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakati ilipoanzishwa mwaka 1966. Alisimamia mchakato wa kwanza wa kutoa sarafu ya Tanzania (shilingi) baada ya kuvunjika kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki. Alishikilia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minane (1966–1974).

3. Msuguano na Mwalimu Nyerere
Mtei alikuwa Waziri wa Fedha katika serikali ya Mwalimu Julius Nyerere. Hata hivyo, alijiuzulu nafasi hiyo mwaka 1979 kutokana na kutofautiana na Nyerere kuhusu sera za kiuchumi, hasa mapendekezo ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ambayo Nyerere aliyakataa. Kitendo chake cha kujiuzulu kwa hiari kilihesabika kama ujasiri mkubwa wa kimaslahi wakati huo.

4. Nyadhifa za Kimataifa
Kabla ya kuingia kwenye siasa za ushindani, alihudumu kama Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na pia alifanya kazi katika Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kama Mkurugenzi Mtendaji (Executive Director) akiwakilisha kundi la nchi za Kiafrika.

5. Kuasisi CHADEMA
Baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa mwaka 1992, Mtei alikuwa mmoja wa waasisi wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Alihudumu kama Mwenyekiti wa kwanza wa chama hicho na alitumia rasilimali zake na ushawishi wake kukijenga tangu kikiwa kidogo hadi kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.

6. Uhusiano wa Kifamilia na Freeman Mbowe
Jambo ambalo wengi hulitolea macho ni uhusiano wake na aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Edwin Mtei ni mkwe wa Freeman Mbowe (Mbowe amemuoa binti wa Mtei, Lillian). Hii mara nyingi imekuwa ikitumiwa na wapinzani wao wa kisiasa, lakini ndani ya chama inaonekana kama muendelezo wa misingi aliyoiweka.
Ni mmiliki wa mtei express au???
 
Kuna haja ya kuiangalia misamiati ya kiswahili upya mfano "Mwasisi wa CHADEMA Edwin Mtei afariki dunia" hii heading nadhani haiko sahihi ilitakiwa iwe "Mwasisi wa CHADEMA Edwin Mtei afariki" pasipo kuweka neno dunia ama "Aaga dunia" hawa mods mbona hawafanyii kazi makosa madogo madogo kama haya? All in all APUMZIKE MAHALA PEMA PEPONI SHUJAA.
 
Actually, ninakubaliana nawe; huna siasa kabisa. Wewe ni mmoja wa kundi hatari ndani ya nchi hii. Unaumma huku ukipuliza saana; kama unashughulika na watu wasiokuwa na akili.

Huwezi kushabikia hizo siasa za enzi za akina Mtei; halafu leo hii unageuka na kuwa mshangiliaji mkubwa; hapana, siyo mshangiliaji, bali mhusika wa mauaji ya waTanzania.

You're worse than a devil; if there's such a possibility.
The worst scum that has ever been existent in our beloved nation.
Unayo haki ya maoni yako ndio ukomavu wa demokrasia wenyewe huo.

Najua kipi kinachofanyika huko serikalini kwamba sio kila kitu kipingwe.
 
Unayo haki ya maoni yako ndio ukomavu wa demokrasia wenyewe huo.

Najua kipi kinachofanyika huko serikalini kwamba sio kila kitu kipingwe.
Mkuu 'Steve', sijui ni kipi kilichokufanya urudi kwenye hiyo mada uliyonijibu.
Ni hivi: nimekwishapata uzoefu zaidi juu yako kwamba sina lolote tena ninalosoma toka kwako na kuliamini kuwa linatoka moyoni mwako.
Huo mstari wa kwanza juu ya demokrasia; kwa mfano, ni 'bull shit'; huna lolote unaloamini juu yake.

Ajabu ni kwamba hadi sasa unajifanya hujui kinachopingwa?
Historia yako naifahamu vya kutosha; watu wa aina yako ndilo tatizo kubwa linaloikabili nchi yetu.

Hadi hapo tutakapofanikiwa kuwang'oa, nchi hii haitatulia hata kidogo.
Timu ya akina Thabit Kombo, na akina Hamza Johari na wengineo huko unakokuita wewe "serikalini".
 
Mkuu 'Steve', sijui ni kipi kilichokufanya urudi kwenye hiyo mada uliyonijibu.
Ni hivi: nimekwishapata uzoefu zaidi juu yako kwamba sina lolote tena ninalosoma toka kwako na kuliamini kuwa linatoka moyoni mwako.
Huo mstari wa kwanza juu ya demokrasia; kwa mfano, ni 'bull shit'; huna lolote unaloamini juu yake.

Ajabu ni kwamba hadi sasa unajifanya hujui kinachopingwa?
Historia yako naifahamu vya kutosha; watu wa aina yako ndilo tatizo kubwa linaloikabili nchi yetu.

Hadi hapo tutakapofanikiwa kuwang'oa, nchi hii haitatulia hata kidogo.
Timu ya akina Thabit Kombo, na akina Hamza Johari na wengineo huko unakokuita wewe "serikalini".
Endeleeni kupoteza muda kwenye siasa za kuuma moto mkiwa mmekunja sura.
 
Endeleeni kupoteza muda kwenye siasa za kuuma moto mkiwa mmekunja sura.
Bado unajiona unao wigo wa kujipa matumain kadri hali inavyozidi kuwa tetei?

Timu yenu nzima sasa inaanza kujifunua taratibu; na nyote wahusika mtabainika tu!

Huyo Thabiti Kombo mpelekee taarifa yake.
 
Bado unajiona unao wigo wa kujipa matumain kadri hali inavyozidi kuwa tetei?

Timu yenu nzima sasa inaanza kujifunua taratibu; na nyote wahusika mtabainika tu!

Huyo Thabiti Kombo mpelekee taarifa yake.
Mkuu haya maisha ya taharuki ni nyinyi mnayaishi, wenye kuzielewa hizi siasa za mitandaoni wala hawana wasiwasi.
 
Mkuu haya maisha ya taharuki ni nyinyi mnayaishi, wenye kuzielewa hizi siasa za mitandaoni wala hawana wasiwasi.
Hizi "siasa za mtandaoni" wewe zinakuwashia nini sasa!
Hizo siasa mlizozoea za kuua waTanzania haziwapi shida nyinyi?
Hamna "wasiwasi" kabisa; yaani haziwagusi!

Ninapokueleza kuwa wewe ni mmoja wa watu waovu, kundi moja na Samia sibahatishi hata kidogo.
Ila sasa ni wazi hamna njia ya kuepa tena matokeo ya uovu wenu.
 
Back
Top Bottom