Mkuu, niseme tu hivi katika kujibu?/kuongeza uzito katika hoja yako: Zaidi ya miaka 60, ya kujipangia sisi wenyewe mambo yetu tunavyotaka kuyafanya sisi wenyewe, kweli tumeshindwa kabisa kumpata "welder G6" tunayeweza kumtegemea kufanikisha kazi zetu sisi wenyewe?Wewe unategemea engineer graduate toka vyuo vyetu aliyejifunza welding kwa week mbili tu amsimamie G6 welder kweli?
Lakini kuna mambo mengi tunapuyanga tu.Mkuu, niseme tu hivi katika kujibu?/kuongeza uzito katika hoja yako: Zaidi ya miaka 60, ya kujipangia sisi wenyewe mambo yetu tunavyotaka kuyafanya sisi wenyewe, kweli tumeshindwa kabisa kumpata "welder G6" tunayeweza kumtegemea kufanikisha kazi zetu sisi wenyewe?
Kwa swali hili, tafadhari ninakuomba urejee tena kwenye hoja yangu hapo juu, iliyokufanya uwaze swali lako hapo juu.
Uamini wangu, kwa dhati yangu yote ya moyo, Tanzania kwa sasa hivi tunao watu wengi walio na uwezo wa kufanya mambo makubwa sana ya kuliendeleza taifa hili katika nyanja mbalimbali.
Tatizo pekee lililopo, hatuna viongozi wenye uwezo wa kutu'organize' tufanya hayo yote tunayoyaweza.
Ngoja kwa leo niachie hapo, lakini huu ni mjadala unaonisikitisha sana kuona jinsi tunavyozungukazunguka tu, na kulialia kwa kila jambo kutafuta tusaidiwe.