Hapa tunazungumzia Mwanza na Arusha... Researchers hawakusanyi data kama wewe utakavyo au unavyotaka iwe... Ila kama unataka hicho unachosema wewe, basi na wewe leta hapa verified data kutoka any verified organization ambayo inaonyesha Jiji la Mwanza lina maisha bora kuliko Jiji la Arusha.. Hatutaki utuwekee picha na maneno ya vijiweni..
unazungumzia maisha bora! maisha bora ni ya kwako binafsi na familia yako, usije ukajidanganya wale ombaomba dar wana maisha bora zaidi ya karim wa karagwe nayemiliki viwanda vya kahawa na vituo vya mafuta. au wale wanaofanya kazi ngumu kwenye migodi ya makaa ya mawe kule china na india na juzi hapa walikuwa wanalalamika hakuna maji eti wana maisha bora kuliko mie wa wa tz ambaye naoga maji ya kutosha kwenye bomba la mvua, nakula sato fresh, nk. ubora wa maisha yako hauko kwenye makaratasi aisee
wakati mkazi wa arusha tiba ikikosekana hospital ya mkoa itambidi asafiri kutafuta tiba mkoa mwingine, mkazi wa mwanza ikishindikana hospital ya mkoa atapewa rufaa ya bugando ndani jiji.
wakati mkazi wa jiji la arusha akitaka kupanda ndege ya abiria atambidi asafiri hadi nje ya jiji na nje ya mkoa, mkazi wa mwanza anapanda ndege ndani ya jiji.
wakati mkazi wa mwanza yule wa chini kabisa ambaye hana bomba la maji ananinua dumu la lita 20 la maji safi kwa tsh. 50 mkazi wa arusha ananunua maji ya chumvi kwa tsh 1000 meno
machafu kama nini.
wakati mkazi wa kawaida wa jiji la mwanza anaoga maji ya presha ya kutosha kwenye bomba la mvua mkazi wa kawaida wa jiji la arusha anaoga maji ya kwenye kindoo tena nusu.
wakati habari za kimataifa kwa lugha ya kiswahili za bbc watanzania wanazitazama kupitia startv live kutoka mwanza city, jiji la arusha hakuna tv station inayotazamwa hata monduli.
wakati wakaz wa mwanza wanavuka barabara juu kwa juu wanaarusha wanavizia kama panya gari iko mbali ndo wanavuka tena kwa mbio kali mno! ebo mtavunjika miguu.