Kama Kuna wadau au viongozi wanaoupitia huu Uzi nilitamani sana mwanza kuwe na yafuatayo
1. suala la urasmishaji wa maeneo ya milimani ni suala la kisiasa, nilitamani kama mkoa umeamua hivyo, basi raia wapewe namna ya kuyaendeleza maeneo Yao ikizingatiwa kuwa ni taswira na uso wa Jiji hivyo hayapaswi kuonekana rough vile yalivyo sasa hivi. Wanaoshindwa kuendeleza waondolewe na pale wawekezaji wakija kutaka kuwekeza wapewe maeneo wajenge vitu vya kieleweka. Kuweka siasa kwenye maeneo katikati ya miji ni kushindwa kufikiria kwa ipasavyo, mbona suala la machinga liliwezekana
2.kuendeleza fukwe na kuimarisha utalii wa ziwa, kuwe na sport boat za kutosha pamoja na facilities zote za msiingi hii italeta watu wengi wenye uchumi wa kati hivyo mzunguko wa pesa utakuwa poa
3. Kuwe na kumbi kubwa za mikutano level za kimataifa ili kuvutia asasi mbali mbali kuja kufanyia huko mikutano Yao.
4. Kuwepo na maeneo ya recreation ambayo yanakuwa na migahawa Bora ya kisasa, sports facilities, super markets pamoja na swimming pools
5. Kuwe na viwanja vya ndani vya michezo mbalimbali kama netball, volleyball, basketball, boxing na swimming pool
6. Kuwe na museum kubwa ambayo ndani mwake inakuwa na maktaba ya kihistoria.
7. Kuwe na chuo kikuu, rocky city university au mwanza university chenye fani nyingi kama ilivyo UDOM.
8. Kuwe na kiwanja Cha mpira kikubwa na Cha kisasa
9. Kuwe na sehemu Bora na ya kisasa kwa ajili ya maonyesho mbali mbali ya kimataifa . Hata pale nane nane siyo rafiki kufanyia maonyesho ya kilimo kwani hakuna facilities za kujizuia na mvua ikitokea imenyesha, hakuna migahawa wakati maenesho haya huambatana na biashara pia. Tuwe na maeneo mawili ambayo yako-equiped, eneo kwa ajili ya maenesho ya nane nane na eneo kwa ajili ya maenesho ya bidhaa za kimataifa . Mkoa wafungue macho hizi ni fursa wanaziacha tu.
10. Uwanja wa ndege wa level ya kimataifa
11. Bara bara za njia sita au zaidi
12. N.k
Haya yakifanyika yatavutia makampuni, asasi mbali mbali na watu wenye uchumi wa kati kuwekeza au kuishi mwanza. Matunda yake ni kama yafuatayo.
. Kuongezeka kwa mahoteli mazuri kwani kutakuwa na ushindani wa ubora wa hizo hotels ili kuvutia wateja. Hotel nyota Tano zitajengwa mno.
. Uwekezaji kwenye sector zingine kama malls, modern restaurants, clubs, banks, apartments n.k vitaongezeka
. Mji itapemdeza mno
FAIDA KWA MKOA NA WAKAZI
. wepesi wa misha kwani mzunguko wa Hela utakuwa mkubwa
. Ongezeko la makusanyo
. Mji utatanuka na mahitaji