Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,005
- 9,872
Amefika katika ofisi za mkuu wa mkoa leo saa 4:50 asubuhi na kupokelewa na wajumbe wa kamati ya amani ya mkoa huo.
Kwa mujibu wa katibu mieka wa mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Matia Levi amesema makabidhiano baina ya wawili hao yanatarajiwa kufanyika wakati wowote leo.
Katika mabadiliko ya wakuu wa mikoa yaliyofanywa na Rais Samia leo, aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ally Hapi amehamishiwa mkoani Mara kuchukua nafasi ya Gabriel huku aliyekuwa katibu tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Dk Batilda Buriani akiteuliwa kuchukua nafasi ya Hapi.