Mwanaume wa ndoto yangu

Mwanaume wa ndoto yangu

jaqfantasy212

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2012
Posts
542
Reaction score
258
Habari wakuu!!

Leo nimeamua kuandika kilichopo katika ndoto yangu katika swala zima la mahusiano..

Kila mtu amekuwa na ndoto au aina fulani hiv ya mtu ambaye angependa kuwa nawe katika mahusiano, kwangu mm namuota mwanaume wa aina hii..

1:Mwanaume ambaye ningependa kuwa naye kwanza awe mwenye umri kati ya miaka 27-35
Hii ni kwasababu mm mwenyewe nina miaka 27 kwahiyo nisingependa mwanaume nitakayekuwa nae nimzid umri..

2: Ningependa kuwa na mwanaume ambaye ameshapitia na kufanya mambo mengi sana, kiasi kwamba haoni jipya..
Mfano: mwanaume ambaye alikuwa malaya ameshatembea na aina zote za wanawake amemaliza na ss ameamua kutulia na kutengeneza life.

3: mwanaume ambaye ataniongoza katika maisha yangu, hasa katika ushaur au kunikosoa ninapokosea

4: mwanaume ambaye atakuwa rafiki yangu..

5: mwanaume ambaye anavumilika, nikisema anavumilika namaanisha hata kama hana kaz au ela lakini ni mwanaume ambaye ana akili na ukimsikiliza na kumuangalia ana future..

6:mwanaume ambaye anamsimamo na mwenye kujitambua anataka nn..

Dhaa!! Naota mengi ila kwasasa ngoja niishie hapa..
 
mimi nimebakiwa na nafasi moja....njoo ndoto yako itatimia
 
Vipi na wewe umeshapitia mambo mengi-kukutana na wanaume wengi kiasi huoni jipya kutoka kwao hivyo kutulia ktk ndoa.Coz nisije kukuoa halafu kesho na keshokutwa unapoziangalia tamthilia za bongo muvi zinazofundisha usaliti na wewe unaanza michepuko.Tuambie kabisa je umeshakutana na midushelele tofauti tofauti?
 
Sawa!!
Je wewe umeshaona mengi kiasi kwamba huoni jipya!?, au utaanza kukimbilia masharobalo waliovaa mlegezo na macheni kibao shingoni?
Wewe mwenyewe unajitambua unataka nini!?, do you have a destiny au unaishi tu ili mradi kunakucha?

Ni muhimu kujua kuwa huyo mwanaume nae atahitaji sifa flani kutoka kwako pia..
 
Sawa!!
Je wewe umeshaona mengi kiasi kwamba huoni jipya!?, au utaanza kukimbilia masharobalo waliovaa mlegezo na macheni kibao shingoni?
Wewe mwenyewe unajitambua unataka nini!?, do you have a destiny au unaishi tu ili mradi kunakucha?

Ni muhimu kujua kuwa huyo mwanaume nae atahitaji sifa flani kutoka kwako pia..

Mpk nimefikia hapa nimeona na kupitia mengi, na katika pitapita zangu si yote amabayo nimejifunza nimefanya mengine nimejifunza kutoka katika jamii yangu..

Mwanamke anaweza akawa amefanya mengi sana katika usichana wake inawezekana kabisa yakawa si matakwa yake ila alilazimika kutokana na kukosa mtu sahihi

Mwanaume sharobalo hana nafasi kwangu..
 
Vipi na wewe umeshapitia mambo mengi-kukutana na wanaume wengi kiasi huoni jipya kutoka kwao hivyo kutulia ktk ndoa.Coz nisije kukuoa halafu kesho na keshokutwa unapoziangalia tamthilia za bongo muvi zinazofundisha usaliti na wewe unaanza michepuko.Tuambie kabisa je umeshakutana na midushelele tofauti tofauti?

Hahaaa!! Sina haraka na ndoa, wala siiwazii naamin ndoa ni matokeo tu..
 
Mimi sitaki mwanamke aliyepitia kila aina ya mwanaume kama wewe...
 
Fanya haraka njoo kwangu kabla wenzio hawajaniwahi

Hujakosea hata kimoja vigezo vyako ndivyo hivyo nilivyonavyo.
 
Mimi sitaki mwanamke aliyepitia kila aina ya mwanaume kama wewe...
Mkuu ukiwa unareply just relax, elewa nilichosema sijasema nimepitia kila aina ya mwanaume ila nilichojaribu kusema ni kwamba katika mahusiano mtu unaweza ukawa umepita katika mahusiano labda mara tatu, nne mpk 5 si kwakupenda ila mara zote hizo umefikia katika mikono isiyo sahihi, je utaendelea kuwepo kwenye mahusiano hayo?
 
Back
Top Bottom