uttoh2002
JF-Expert Member
- Feb 3, 2012
- 14,871
- 26,966
Kuna Mdada ni mteja wangu mkubwa katika biashara Yangu,Yupo vizuri kimaisha,Kama mwanaume nilijikuta nikimtamani mana ni mtu na nusu Ila kabla ya kumtongoza nilikuwa Namuuliza kama Ana mume Cuz Mimi sipendi kabisa mambo za mke wa mtu,Kheri Awe demu wa mtu Ila Akiwa ni mke wa mtu hata kama simfahamu mumewe basi Simuhitaji katika maisha yangu,Basi buana akanijibu hana mume Ila Alikuwa na mpenzi tu Ila wameachana basi Nikarusha nyavu bahati nzuri Samaki nikampata..!!
Tumekaa katika Mahusiano kama mwezi ivi Full Romance Huku tukitoka Chakula cha usiku Ila hatukuwahi kufanya mapenzi Sababu ya kutofanya mapenzi Siijui kwanini Nashangaa nilikuwa mzito tu kuomba mechi licha ya kuwa mdada mzuri sana Yani nilikuwa sijui kwanini nakuwa mzito sana..
Maendeleo kwenye biashara yangu ni mazuri sana Ameendelea kuja kwenye biashara yangu na kuniungisha mzigo mkubwa na kuniletea Connection Za watu mbali mbali Hakika biashara yangu Imepamba moto kuhusu wateja Alhamdulilh…!!
Sasa wiki kadhaa nyuma alivoona kimya simgusii swala La Kwenye Kunyanduana akaniambia ananihitaji tukapige show Nikakubali na nikampa Matakwa yangu kuwa lazima tupime afya na tukaenda kupima tukajikuta wote tupo salama,Kilichobaki ni kwenda Kunyanduana..!!
Jumatatu iliopita Tukiwa Kwenye gari yake(Mimi ndio nilikuwa dereva )Tunaelekea hotel kukiwasha Tukafika sehemu Akaniambia nimsubiri nusu Saa Akashuka then mimi nikawa nimetulia kwenye gari,Dakika kadhaa Dirisha la upande wangu likagongwa Nikashuka kioo nikamuona jamaa mmoja ivi simfahamu Ila akawa Ananishangaa Akaanza kuniambia kuwa amenifananisha Mana hii gari ya mtu furani na plate number ndio ivo ivo so anashangaa kuniona mie,Nikamjibu mimi dereva tu Akaanza kuniambia dah Huyu mumewe alikuwa hataki kabisa mke wake aendeshwe imekuwaje ameruhusu..!!Duh mimi nikastuka nikamuuliza kwani ameolewa jamaa akaniambia yeah,Huyu jamaa ni wale kama machawa akanifungikia mengi sana na akaniambia kama Huyu demu ndio kaniajiri bila mumewe kujua basi niache hio kazi chap dah ilinipiga usoni hii kitu,Tukaongea mambo kadhaa akaniomba 10k nikampa akasepa..
Demu alivorudi kwakuwa nilikuwa wa mto nikamuuliza kuhusu Ndoa na kwanini amenidanganya na demu akafunguka kuwa ananipenda ndio mana amenidanganya full kunionesha picha za harusi Aisee ilinipiga Usoni,Nikamwambia hii safari tutaenda siku ingine now sipo sawa..!!
Zikapita siku kama 3 ivi mawasiliano ya kawaida tu Ila nilianza kumpotezea ila sitaki kumchana kuwa sikutaki kabisaa kwasababu ni mteja mkubwa na amenipa connection so nawaza nikimtema makavu live nitapoteza mteja na wateja..
Katika biashara yangu hana hata 10 yake wala hajawahi nipa hela niongezee katika biashara Labda baadhi ya vitu vya geto Amenisaidia kiufupi alivokuja kwenye maisha yangu Amebadilisha Kidogo maisha yangu hasa kwa hawa wateja alioniletea..!!
mimi na mke wa mtu Ni vitu viwili tofautii Nishaambiwa na baba angu Kheri Nikate uume wangu kuliko kulala na mke wa mtu…wazee wa busara ile kauli ya MKE WA MTU SUMU huwa naishi nayo sana moyoni…
Huyu demu age yake 31 ivi Now ananisumbua sana Nawaza nimchane nione itakuwaje au niendelee kumpotezea Tu ili nisipoteze mteja na wale watu alionionganishia au niaje niaje..!!
'Jumatatu iliopita Tukiwa Kwenye gari yake(Mimi ndio nilikuwa dereva '
Angalia hii Tabia sio ya kiume, hatugusi kitu ya mwanamke neither kaolewa no singles.