Mwanasheria mkuu wa Serikali, Werema aungana na UKAWA

Mwanasheria mkuu wa Serikali, Werema aungana na UKAWA

ni theluthi mbili au theluthi mbili ya tatu?
 
Werema kaamua kuwaambia indirecrly ccm wasitishe BMK, anaogopa kuwaambia directly. Sikumbuki kama imewahi tokea b4 mwanasheria mkuu kufanya press conference, ni kwamba anaogopa kumwambia mfalme kuwa yuko uchi kwa hakika anaogopa lawama kuwa wananchi watasema pesa imepotea bure, mwanasheria hakuwashauri watoa maamuzi juu ya theluthi 2 za Zanzibar haziwezi kupatikana and so Bunge liahirishwe ili kutafuta maridhiano kwanza. Anapowaomba UKAWA warudi nafikiri anafanya utani, Kikubwa ni kuwa anapeleka meseji kwa watoa uamuzi kwamba bunge liahirishwe na take note that ameamua kusema baada ya kauli ya ikulu kuwa katiba itapatikana hata bila UKAWA.

Unajua AG Werema kaamua kusema ukweli ili baadae asilaumiwe yeye. Katoa press conference ili baadae akiulizwa aseme yeye alishatumia busara kuwa kwa mazingira yalivyo 2/3 haiwez kupatikana katiba mpya na kuna ule usemi yeye hapo keshanawa!
 
mkuu wote waliopo pale dom ni ulafitu umewapeleka laki3 kwa day siomasihara mkuu kuna mtu mpaka anakufa hajawai piga laki3 sasa kwa nini asikamie?
ni kweli, ukingatia ndani ya siku 60 milioni 18, naona mzee Arfi uzalendo umemshinda, kaamua kusaliti watanzania kwa kushabikia pesa!
 
Mpaka anambembeza hivyo kawa mpole. Mpaka anawakumbushia kwamba wanasali wote so what.
mkuu lengo si kwamba wanawapenda ukawa la hasha, ni kutaka kuhalalisha huu ufisadi wa posho huko dodoma, ili mwakani waseme, hata jussa alichukuwa posho, na hata lissu alikuwepo nk.
 
mkuu lengo si kwamba wanawapenda ukawa la hasha, ni kutaka kuhalalisha huu ufisadi wa posho huko dodoma, ili mwakani waseme, hata jussa alichukuwa posho, na hata lissu alikuwepo nk.

Ukiona wababe wamekuwa wapoke ujue dawa ya UKAWA imewaingia sawasawa
 
Rais wa nchi anasema yeye hahusiki kulivunja Bunge la Posho na Mwanasheria Mkuu anathibitisha hivyo na kuwataka wale wanaomshinikiza Rais kulivunja Bunge hilo waende shule wakasome sheria, lakini yeye aliyesomea sheria na ambaye pia ni wajibu wake kutufahamisha Watanzania kuhusu hili yuko kimya!!!

nchi ihi inaenda enda kama gari lililopoteza mwelekeo?
 
ni kweli, ukingatia ndani ya siku 60 milioni 18, naona mzee Arfi uzalendo umemshinda, kaamua kusaliti watanzania kwa kushabikia pesa!

You get them rightly! Hata hivyo walisha sema ukawa wameshiriki kutunga sheria ya katiba na mjadara sura 1 n 6.
 
ccm wana macho lakini hayaoni,wanachoangalia hapo ni posho sio katiba,wananchi wakiikataa au isipopatikana theluthi mbili kwao sio kitu,ndio maana wamebadilisha kanuni ili kura ipigwe siku ya mwisho wakiwa tayari wamekusanya posho zao. watu wenye akili hili waliliona mapema lakini wana ccm wamejitoa fahamu
 
Kweli kabisa manake ata uyu wanayemwita mwanasheria wa serikali kuropoka ivyo pini imebana sana, Lakini cha ajabu akisimama Wassira, Lukuvi na Sitta na huko Ikulu wanasema thuluth 2 haina mjadala,

Hii ni dalili tosha ndani ya CCM kuna makundi, wapo wanaotaka mjadala uwe wa haki lakini pia wapo wengi wanaoforce kufanya manuva alimradi matumbo yaendelee kuvimba.
 
Werema hupaswi kutumia muda mwingi kuwabembeleza Ukawa,unapaswa wewe na serikali yako kujibu hoja za Ukawa.Ukawa hawataki kubembelezwa,wanataka rasimu itokanayo na maoni ya wananchi,na wako nje kwa sababu nyie hamtaki kujadili rasimu hiyo,mnataka kuleta ya kwenu wakubwa wachache wa nchi hii.
 
Nasubiri kauli ya Mwanasheria mkuu wa chama chetu CCM Mh Ndg Nape Nnauye. Mie huwa namfananisha sana na Marehem Tarikh Azizi msemaji mkuu wa ile serikali ya Sadam Hussein
 
Nasubiri kauli ya Mwanasheria mkuu wa chama chetu CCM Mh Ndg Nape Nnauye. Mie huwa namfananisha sana na Marehem Tarikh Azizi msemaji mkuu wa ile serikali ya Sadam Hussein

Tarikh Aziz hakuwa msemaji mkuu wa serikali ya Sadam Hussein bali Makamu wa Rais. ..nitakutafutia jina la huyo aliye kuwa waziri wa habari. ..aliyekuwa msemaji mkuu wakati wa vita ya Iraq na US
 
Na ni kwa sheria ipi iliotumika kumpa mamlaka Rais kuunda kamati ya kurasimu katiba mpya bila ya ridhaa wizara ya katiba hata leo ashindwe kuizuiaa.
wasitidanganye mchana kweupeeee asitudanganye uyo mwanasheria mkuu.
 
Uhakika nilio nao ni mmoja... hata ukiachilia mbali suala la idadi, nina uhakika kwa CCM hawataweza kuiunda upya rasimu hasa baada ya kuibadili kutoka mfumo wa serikali tatu na kuifanya mbili...
 

Comical Ali

Tarikh Aziz hakuwa msemaji mkuu wa serikali ya Sadam Hussein bali Makamu wa Rais. ..nitakutafutia jina la huyo aliye kuwa waziri wa habari. ..aliyekuwa msemaji mkuu wakati wa vita ya Iraq na US
 
Last edited by a moderator:
Jamani hapa muokoz pekee wa hili jahaz la katiba ni Rais wa muungano. coz yeye ndio mwenye mamlaka pekee ya decree of power. tusisubir maafa wao ccm wanachukulia poa but wajue kua huu si uchaguzi wala ushindi ila ni misingi ya nchi imara iweze kusimamishaa Taifa letu.

Nakuomba muheshimiwa wangu Rais wengi tunaijua iliokua zamira yako kwa watanzania ni kutuletea uhuru wakatiba japo wenzio wa juu wa halmashairi wamekutelekeza ukakosa msimamo lakini muheshimiwa kumbuka taifa lipo ndani ya dhamana yako tumevuka salama pongezi ni zako hatopongezwa mwingine na kinyume chake tumejikwaa mzigo ni wako na hao unaowaendekeza leo keshoo watakulizaa.

Jikumbushie tu kwa historia ya mda mfupi znz . Rais mstaafu Mh Amani Abeid karume kafanya anayoyapenda yeye mda mwingi lakin hakuchelea karibia na kumaliza mda wake kajitathmini kwa aliyoyafanya akajua lazima akiondoka jamii itamsuta kw ujanja na umakini na kujisafisha na kwa kuieka jamii sawa ametuletea kile wazanzibar tulichokipoteza mda mrefu . kuondosha mpasuko wa kisiasa znz kw kuweka maridhiano jambo ambalo watendaji wake wa ccm walilipinga na kulitolea hoja nyingi but kw vile anajua mamlaka alonayo (decree of power) japo walimtukana na kumdhalilisha but hakuyumba alisimama kiume kuhakikisha anaweka sawa taifa japo serikal ya muungano iliionyeshs eazi kuibeza znz na kusema ZNZ sio nchi hivyo aliliamuru baraza lakutunga sheria znz kufanyiwa mabadiliko makubwa ya kikatiba ilioipa nguvu nchi ya znz ambapo inekua kikwazo kw ccm waleo kuweza kuichakachua mpk kwa ridhaa ya wazanzibar wenyewe pamoja na kuwaweka p1 wa znz wote kw kuundwa kwa kamati ya maridhiano ambayo zanzibar ilikua kama ndoto. Hivyo tunanpenda na kumheshimu Rais wetu huyu ambapo imepelekea kufanya uchaguzi mkuu 2010 kw njia za aman bila kumwaga damu ambayo ni tofaut kw miaka iliyopitaa.

Nawe baba etu wa taifa Rais wetu mpendw hujacherewa usiogope wananch tupo imara na tunaona jitihada zako so keep it up utafikaa tu salaama tunakuombea.

lakini kuna msemo unasema ukitaka kumla nyani usimiangalie usonii
 
Back
Top Bottom