''Mwanangu, babako amekufa''

''Mwanangu, babako amekufa''

wewe kweli Wakuacha kama lilivyo jina lako.
yaani pesa ipite kwa mama yako ndo ifike kwa mzazi mwenzio?
hivi siku ulipokuwa unam-mimba huyu dada mama yako alikuwepo ama alijua?
kwann usitafute njia nyingine nzuri zaid na ili asimlee mwanao kwa jeuri na kiburi kuliko hii?
ukweli nakufungulia uzi aisee
Mkuu ile mimi ndo niliona njia sahihi msumbufu sana yule...
 
njia ya kumtumia mama yako?
hujui wingi wa chuki unaopanda hapo take it from me......
Hiyo ndo njia sahihi mimi sitaki hata namba yake ya cm....kabisa njia ambayo itanifanya hata sura yake tu niione sitaki.
 
Umefanya vema kuepusha msongamano, lea mwano, Mungu wetu ni mwaminifu hatakuacha wala kukupungukia, endelea kumtumainia yeye aliye asili ya vitu vyote
 
Dunia ni zaidi ya uijuavyo. Hapo inaonekana kulikua hamna makubaliano ya ndoa ni kubanjuana tu.
Pia makubaliano ya kuzaa hayakuwepo ila kama ulichukua nafasi ukatumia fursa ulifikiri atakamatika akuonee huruma sasa hataki kusikia kodi, bili za mtoto wala nn. Kwa akili yako badala ukae nae umuweke sawa unataka umiharibu mtoto halafu nn kitafuata baada ya hapo ?
Unapolia inawezekana unajutia ujinga ulioufanya au unafurahia raha unayopata au kuigulia maumivu pia sasa sijui inakuaje hapo?
Pole kwa changamoto unazopitia huku kuna jirani walifunga ndoa wamezaa watoto wawili kaleta kiburi kisa ana kazi jamaa kamwchia watoto kaondoka zake maisha yanaendelea
 
Dada usihofu wala kulalamika. Tunda unalo na ndani mna mbegu zitamea. mti uko kule unaweza ukauke lakini tunda na mbegu unavyo. Furahia mtoto wako kwa kuwa yupo. ni fimbo iliyo mkononi, ni ushindi
 
Wanabodi nashukuru kwa michango yenu,yote ya kunipa moyo,kusema nilizaa ili awe ananipa hela,ya kukashifu and the likes.nimeappreciate.
Hadi muda huu moyo wangu unanambia,ni busara nikaendelea na uamuzi huu nilochukua.

Sina hasira wala kinyongo,nalibeba hili kwa mikono miwili.Mtoto huyu ni zawadi toka kwa Mungu,hata yeye anatambua hilo.ila si neno ya walimwengu ni mengi na binadamu hubadilika,mwanaume huyu nilianza naye mahusiano akiwa hana kazi,sikuzaa mtoto huyu ile anipe pesa kama wengi wadhaniavyo.

Alipokuwa hana kazi tulikuwa watu wafuraha na maelewano sana,Mungu kambariki kapata kazi ndo akaanza onyesha makucha.huyo nilokuta anaishi naye alimkimbia kipindi akiwa hana shughuli hapa mjini.Yote kheri.

Ila kama wengi wasemavyo nashukuru kwa hili,mwanangu ntamlea kwa upendo wote.Hatokaa aone hata call yangu kwa simu yake,nimebadili line yangu ya simu.Nimeongea pia na dalali anitafutie nyumba,nitahama hapa napoishi muda si mrefu.Nayaanza maisha mapya na mwanangu.
 
Muda mwingine muwe mnasoma alama za nyakati. Mtu anakwambia hana future na wewe. Unambebea mimba hata Mzee wangu pale msoga alishasema hivo ni viherehere vyenu.
 
Au nyie ndo wale wa nipe mimba mtoto nitalea, ukishazaa unakuwa na figisufigisu wakati mlikubaliana nikupe mimba pekee.
 
wewe kweli Wakuacha kama lilivyo jina lako.
yaani pesa ipite kwa mama yako ndo ifike kwa mzazi mwenzio?
hivi siku ulipokuwa unam-mimba huyu dada mama yako alikuwepo ama alijua?
kwann usitafute njia nyingine nzuri zaid na ili asimlee mwanao kwa jeuri na kiburi kuliko hii?
ukweli nakufungulia uzi aisee
Katika hali ya kawaida unaweza kushangaa kwa nini Wakuacha amefanya hivyo( kutuma pesa kupitia mtu mwingine, hasa mama) lakini kuna watu ni wakorofi, naamini maamuzi ya kulea mtoto yanahitaji maamuzi ya vyombo vya kisheria. Some mothers are given custody but they're totally unfit to cater for their offspring.
 
Nyie si mnadai haki sawa . Sasa kulea tu kichanga hata hakijaanza kusoma unatoa chozi you will never go against the nature of God's creation. Kama mlitoka ubavuni tena ni ubavu wa kushoto mtaendelea kuwa chini yetu tu mpaka maisha ya duniani yaishe. 50% 50% mtaiongea kwenye majukwaa siku za kuadhimisha hiyo siku yenu ila mkifika majumbani kwenu manrudi kama Mungu alivyoamrisha siku ya uumbaji.
 
Kabla hujafungua miguu yako ilibidi ufungue akili yako kwanza sio unazaa tu kama chura halafu watoto wenu mnaanza kuwajaza chuki za kijinga......ujinga wenu ndio unatuletea product za ajabuajabu mitaani

#Mungu aliposema usizini na usishuhudie uwongo hakuwa mjinga
Heee wewe mbona una kauli nzito hivo
Huoni anaumia mwenzako hapa
Ushazaa wewe???!
 
Kama ni mimi,nina kazi yangu na uwezo wa kumlea mwanangu ninao,nisinge hangaika na huyo mwanaume mana ni pasua kichwa

Yani nisingetaka stress zake kabisa,furaha yangu ningeelekeza kwa mwanangu, ningehakikisha nampatia malezi bora kadri niwezavyo

Ila tu akihitaji kumwona mwanae sitamnyima,lakini kumtegemea kwa chochote nisingetaka. Yani kumruhusu asumbue moyo wangu nisingempa hiyo nafasi kabisa
Sio rahisi, umuhimu wa baba ni vivid protection na emotional, Naamini malezi na maisha kiujumla ni zaidi ya pesa,
I pray nilee watoto na baba yao,I can never underestimate his importance
 
Sio rahisi, umuhimu wa baba ni vivid protection na emotional, Naamini malezi na maisha kiujumla ni zaidi ya pesa,
I pray nilee watoto na baba yao,I can never underestimate his importance
Malezi ya wawili ni muhimu kuliko tunavyodhani. Upo sahihi kabisa, kuna mifano hai nimeiona katika maisha, japo siwezi kuongea wazi lakini ni vizuri kulea pamoja, anachompa mama sicho anachompa baba(katika nyanja zote)
Lakini pia, kuna sababu zinaweza kuwafanya wawili wasiishi pamoja, tunaweza kulaumu hili na lile, mwisho lazima mtoto apate malezi bora, iwe mnaishi pamoja au mmetengana. Kuna watu wametengana ili kufanya watoto waishi kwa amani...
 
Back
Top Bottom