Mwanamke wa dizaini hii anafaa kuolewa?

Mwanamke wa dizaini hii anafaa kuolewa?

Ndio kuchunguzana kwenyewe anatest uvumilivu wako na reaction unapoombwa hela ili aone kama utamfaa kwa miaka mingi ya ndoa au la.

Je, nikikoswa pesa si ndo atanikimbia?
Na siku nikimnyima atakuwaje maana nitakuwa nimeshamzoesha kihivyo (Umleavyo ndivyo akuavyo)?
 
Salam wadau!

Mimi ni kijana wa miaka 27. Kuna mdada nimemtongoza na katika majadiliano naye akadai tupeane mda wa kuchunguzana ndipo tufikie maamuzi. Lakini cha ajabu ndani ya siku mbili tangu nimemtongoza, ameanza kuniomba pesa kwa wingi. Nami najiuliza, kwa hali hiyo ya kuniombaomba pesa mara kwa mara ananichuna au anahitaji pesa zangu??
Nahitaji msaada Wakuu maana sielewi hata nifanyeje mpaka mda huu.

Ulitaka akuombe baada ya muda gani!?
 
Anafaa kuolewa,pia huwezi kupata ambae haombi pesa,wewe ndio ajira yake

Sijakataa kuombwa pesa, lakini yeye amezidi sana. Hatujamaliza hata wiki.
 
Wanataka wapewe wao.....hivi wanaume wa siku hizi mmekuaje....?.....kwa nini hamtaki kutoa hela......?.........ua bila kumwagiliwa mnadhani litapendezaje......?......

Hatuwezi kataa kutoa, ila ndo kwanza nimemtokea anaanza mapema kiasi hicho!
 
Kwani alitakiwa aanze baada ya muda gani kuomba? Kwa mtizamo wako!
 
Kwakweli inabidi waunde umoja maana wametuchosha kila siku lawama hizi hizi, wanaume na nyie mmezidi ubahiri khaaaah!! Kwani mkitoa mnakufa?

Wanataka wapewe wao.....hivi wanaume wa siku hizi mmekuaje....?.....kwa nini hamtaki kutoa hela......?.........ua bila kumwagiliwa mnadhani litapendezaje......?......

Mie nashindwa hata kuwashangaa kwakweli!! Huu ubahiri gani sasa na kukalamika tuuuu kama gari bovu, mwanamke gharama jamani hebu toeni tu msisubiri hadi tuwaombe, khaaaaaah!!

Ndio unachunguzwa kama hauna mkono wa birika

Dogo hana kitu huyu. Bado ni wale wanaotaka vizuri bila kujua kuwa vinaundwa.

Hawa wajukuu wanahitaji darasa la kutosha. Huna sababu ya kimsindikiza mrembo lunch Serena kwa pesa za kupewa na bro ukaishia kunywa maji ya bomba kwenye glass. Warudi uswazi kwa kuku wa kienyeji hadi kieleweke. Vinginevyo watauza vyombo vya jiko mwa wazazi.
 
Asante babu

Heri umeliona hilo



Dogo hana kitu huyu. Bado ni wale wanaotaka vizuri bila kujua kuwa vinaundwa.

Hawa wajukuu wanahitaji darasa la kutosha. Huna sababu ya kimsindikiza mrembo lunch Serena kwa pesa za kupewa na bro ukaishia kunywa maji ya bomba kwenye glass. Warudi uswazi kwa kuku wa kienyeji hadi kieleweke. Vinginevyo watauza vyombo vya jiko mwa wazazi.
 
Je, nikikoswa pesa si ndo atanikimbia?
Na siku nikimnyima atakuwaje maana nitakuwa nimeshamzoesha kihivyo (Umleavyo ndivyo akuavyo)?

Huyu ni demu wa ngapi katika maisha yako? Kuwa mkweli please!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom