Mwanamke jifunze uvumilivu

Mwanamke jifunze uvumilivu

Sio wanaume wote wako hivyo.
Nadhani ningedeclare interest kwanza...Mimi huwa sivumilii wala kumng'ang'ania mwanaume/mapenzi ambayo naona yameshafika kikomo.

Nadhani hii ni inferiority complex kudhani kwamba ukiachana na mwanaume huyu utakosa mbora zaidi yake au wote ni sawa.

Mapenzi yanapokufa move on,kuendelea kung'ang'ana ni kupoteza fursa ya kumpata mume mwema ambaye Mungu amekupangia ila kikwazo ni wewe na uking'ang'anizi wako.

I wish wanawake wote tungekuwa na ujasiri wa kumove on...
Shosti ujasiri unakuja kama unakazi na hutegemei mume,huyu wifi yangu Baba yake mzazi alisha wafukuza kitambo na mama yake,ameambiwa tafuta biashara nikufungulie kasem hawezi kuamka asubuhi kufanya biashara,akili yakuweka pesa hana yeye mashauzi harusi akatunze mpaka jana kaja kwangu nimemuliza una kiasi gani chakuweza kukusaidia amenambia ana mil2 ambazo aliachiwa za chakula hana akiba ametoka kufanya harusi ya shoga few weeks back,sasa what will she do with 2m maisha haya? namuonea huruma lakini kama ameamua nta mu wish all the best..
 
hizi ndoa mbona hazina jema kila siku ni haya haya na bado wengine tunafikiria kuoa kwelii. hapa nishajiandaa kisaikolojia maana lolote linaweza kutokea
Tena ujiandae kisawasawa maan sio mchezo
 
Wenye ndoa wanazichezea tusiokua nazo tunazililia n kuomba salama tu
Mmmh shoga hamna anaechezea ukiwaona wanandoa kwa nje utasema umechelewa wapi kupat ndoa ukiingia ndugu yaache tu ndugu yangu maan mengine utaweza kuyasimulia mengine hayasimuliki unabaki nayo ndani ya moyo wako yanazidi kukutafuna tu kila uchwao ndoa za karne hii zaidi ya chuo kikuu
 
My dear,hakuna mateso makubwa kama yale ya moyo.
Huyo ni mtu mzima, mama wa watoto watano anajua nini anafanya.
Nafikiri busara ni kukaa pembeni... Waachie ndoa yao.
Kama angetaka suluhu yapo mabaraza ya usuluhishi na sio wewe.
Umeongea murua kabisa
 
Yani shosti kama ulikuwepo nimeuliza samethings kasema no yeye ameona msg kwenye cm ya mumewe na picha
za huyo mtoto ndio akachukua number ya cm na kuanza kumfatilia mpaka wamempata na still mumewe kamwambia sio mwanangu lakini yeye anasema ni mwanao hapo ndio yule bwana akamwambia usinichanganye niko safarini,mke nae akasema ukirudi Talaka yangu utaileta kwetu,ndio akaja kwangu kunielezwa.
Hebu ilinganie Kwanza hiyo ndoa isivunjike kaka ako akirudi jaribuni kuwashirikisha watu wazima ili muafaka upatikane na hiyo ndoa iendelee m shauri wifio hakuna ndoa rahisi ktk hii dunia mwambie akae alee wanawe aache kupekua simu ya mumewe ukitaka ufe haraka na pressure pekua simu ya mumeo kam hutaambiwa simjui utaambiwa wrong number so mwambie atulie na umshauri atafute biashara afanye
 
Mungu annusuru sana kwa hilo niliwahi mara 2 na nikasema sitorudia tena na sio nimechukua cm kwa nia ya kupekura nilikua bedroom juu yeye alikua chini sasa aliagiza kuku wa kienyeji kwa dadake shamba ili asubuhi akija aje nao,akanambia chukua cm yangu upige sasa siunajua Iphone msg ikawa juu nikasoma ndio nikafungua cm nilipoona msg kuku alinishinda lol..
Ndo wanaume walivyo asipokwambia simjui atakwambia wrong number ni bora vitu vingine uvipitie mbali Kama ambavyo hauwezi kuigusa mboni ya jicho lako Mimi mume wangu hata aisahau simu yake looh wala sishuhuliki nayo kabisa atakapoiwacha ndipo atakapoikuta Kisa ukajiharibia Siku hawa viumbe sio watu wa kuwaamini kabisa yaan
 
Na watu wote waseme "hakika"

Hata angekuwa na watoto 10..... aende kama anataka kwenda

Huu uvumilivu wa kuwanao wanawake tuuuuuu mie siuelewagi..... na kuna vya kuvumilia jamani ila sio uzinzi umalaya vipigo na kutoheshimiana
HAKIKA
Sio wanaume wote wako hivyo.
Nadhani ningedeclare interest kwanza...Mimi huwa sivumilii wala kumng'ang'ania mwanaume/mapenzi ambayo naona yameshafika kikomo.

Nadhani hii ni inferiority complex kudhani kwamba ukiachana na mwanaume huyu utakosa mbora zaidi yake au wote ni sawa.

Mapenzi yanapokufa move on,kuendelea kung'ang'ana ni kupoteza fursa ya kumpata mume mwema ambaye Mungu amekupangia ila kikwazo ni wewe na uking'ang'anizi wako.

I wish wanawake wote tungekuwa na ujasiri wa kumove on...
I see me
 
Muache afanye vile anavyoona moyo wake utapata amani...

Maisha yenyewe mafupi sana kuishi under stress za kiumbe Mwenzako.
 
Habari wana MMU,

Kuna jambo linanitatiza,Jana amekuja wifi yangu mke wa Kaka na kilio nikajua amefiwa
kumuliza haya kumezidi nini? anasema anataka kuachwa amesha choka na kuona msg
kwenye cm ya mumewe za mapenzi na hivi karibuni aliona msg na picha za mtoto
kwenye cm ya mumewe akafatilia mpaka akajua kama mumewe ana mtoto mwengine
sasa ame hama nyumba na anataka Talaka yake,hapo alipo yeye ni mkubwa kuliko
bro,ameolewa mwanzo ana watoto wa2 na akazaa wa3 na bro, nilicho mwambia

Astahmili alee watoto wake,hakuna ndoa yenye raha moja kwa moja leo tamu kesho chungu
na istoshe watoto wake anasomeshewa,maisha sio mabaya anayo ishi tatizo la mumewe ajitahidi
kumuomba mwenyezi mungu atatulia,anasema moyo wake hauchukui tena anataka talaka yake
na watoto wake wawili kawachukua lakini mmoja karudi anasema anataka kuishi na ndugu zake
nimemwambia wifi anipe mda bro amesafiri akirejea ntaongea nae lakini ameshikilia Talaka
Bro amesema Talaka sio Tatizo atampa aseme jengine, lakini waungwana mie staki waachane
sababu watoto watapata tabu,mama wa wifi nae nimeongea nae kanichamba utadhani mie ndio
nilomuoa mwanawe sasa hapa nimebakia njia ya panda hata lakumwambia akanielewa sinaaaa.

Naomba mnisaidie mawazo ili hawa watoto waishi na wazazi wao kwa salama na amani..
Akifa na maradhi atalea watoto? Kama MTU amezaa nje ina maana hata kondom hatumii, hili liwe linakumbukwa
 
Sure ktk suala la mahusiano huwa tuna mtazamo sawa.
Hadi najiulizaga huyu mtu ni pacha wangu nini?
Cheers
Haha yani nilichotaka kuandika nimekuta umeandika mulemule. Thank you . Tutakuwa tuna umapacha wa mbali aisee lol

#Teamknowyourworth#
 
Nifah hata sikuungi mkono ataondoka kwa wangapi wanaume wameumbiwa tamaa ..avumilie alee watt asiondoke kama kuondoka aondoke mume
Point of correction..Kila binadamu ameumbiwa tamaa, ila sio kila mtu anaendekeza tamaa. Kumwambia mtu avumilie kisa wanaume wana tamaa, si sawa, mpe tu sababu nyingine ya kuvumilia
 
My dear....

Kwa kuwa ni masikini (ndio pocha nilopata) ndio avumilie yote?

Kumbuka hayo ndio alosema hakuna ajuae amwvumilia ya kiasi gani

Pia simu ni private kuliko sehemu za sirini eeeh...??? Kutopitia simu ya mume haina maana matatizo hakuna bali ni kuficha kichwa mchangani wakati kiwiliwili kipo nje. Inawezekana wifi mtu anajua tabia za mumewe ndio maana alifukunyua simu......au kuna vitu alivihisi

Wakati mwingine alarm inapiga inabidi kumchubguza.

Hata kama kaka yako kakataa mtoto...... inawezekana kakataa sio wake au kakataa kama kawaida ya wanaume kukana watoto ila mwisho wa siku ina maana aligawa utamu wa mkewe nje

Mwisho wa siku wifi yako atajipanga.....wanasema (ga) tembo hashindwi kubeba mkonga wake....

Ila akubaliane na mumewe way foward kuhusu watoto wao..... maana yeye ndie anayejua viatu alivyovyaa vinambanaaje



Badili Tabia Mkuu kila binadamu ana mapungufu yake hata wifi yangu ana mapungufu yake,ila akitaka watu waweke cards on the table wote watakua na makosa,yeye wakikosana kodogo nipe talaka yangu,au huyo mtoto aloona picha kwenye cm kulikua na ulazima gani kwenda kumtafuta mpaka amuone au aseme ndio mwanao japo mume anakata sio mwanae?
simtetei my bro niko upande wa wifi yangu sababu nimwanamke kama mimi na i know how it feels mumeo aki cheat inaumaje lakini anadhani kudai talaka ndio salution? akisha dai talaka what is next nyumba wanaoyo ishi na mamake ni ya bro,babake mzazi na mamake wameachana baba ameoa mke mwengine na hataki ujinga kawatimua zamani na ndio sababu ya yeye kuolewa ili aishi na mama yake kwenye ndoa yake ya mwanzo,bro amejenga nyumba ndio anayo kaa mama yake wifi sasa why a complicate things? sisemi ateseke kisa hatokua na pakuishi lakini hana hata hela ya kuanzia maisha namuonea huruma ila kama that's what she wants i will respect her decision ..
 
My dear....

Kwa kuwa ni masikini (ndio pocha nilopata) ndio avumilie yote?

Kumbuka hayo ndio alosema hakuna ajuae amwvumilia ya kiasi gani

Pia simu ni private kuliko sehemu za sirini eeeh...??? Kutopitia simu ya mume haina maana matatizo hakuna bali ni kuficha kichwa mchangani wakati kiwiliwili kipo nje. Inawezekana wifi mtu anajua tabia za mumewe ndio maana alifukunyua simu......au kuna vitu alivihisi

Wakati mwingine alarm inapiga inabidi kumchubguza.

Hata kama kaka yako kakataa mtoto...... inawezekana kakataa sio wake au kakataa kama kawaida ya wanaume kukana watoto ila mwisho wa siku ina maana aligawa utamu wa mkewe nje

Mwisho wa siku wifi yako atajipanga.....wanasema (ga) tembo hashindwi kubeba mkonga wake....

Ila akubaliane na mumewe way foward kuhusu watoto wao..... maana yeye ndie anayejua viatu alivyovyaa vinambanaaje
I like this again and again. Ukiwa maskini utabebeshwa mizigo ya misumari na hutakiwi kuishusha mwee
 
Nikwambie kitu Nimpendenani. Wewe unayosema ni sahihi na ndio jambo analopaswa kufanya wifi yako. Ila tayari wifiyo kajazwa ujinga. Kinachomsukuma ni mawazo kuwa urithi wa wanae unapungua kwa kaka yako kuwa na watoto wengine. Anasahau kuwa kaka yako anamlelea watoto wa dume jingine bila kinyongo. Wapambe washamjaza ujinga kwamba talaka itampa haki ya kugawana mali nusu kwa nusu. Na kwa uchumi wa kaka lazima hesabu itakuwa inashawishi ndio maana na mama mkwe kakuchamba aking'ang'ania talaka. Shemeji yangu nae anamsumbua bro kwa ujinga wa namna hiyo. Unaanzaje kuchunguza simu ya mumeo. Anachokitafuta amekipata halafu anachachawa!!
 
Kuna msemo..ukiacha kwakua mume si mwaminifu basi atakaefata nae utamwacha kwa sababu hiyohiyo na sababu zingine piaa,akaze moyo..watoto watano baba wawili,akaolewe tena azae watoto;apige goti amwombe mwenyezi mungu ambadilishe mumewe
 
Alishazoea kuachika. Ngoja akampate mume wa tatu. Afikishe ndoa 8 kama the late Elizabeth Tailor.
 
Nikwambie kitu Nimpendenani. Wewe unayosema ni sahihi na ndio jambo analopaswa kufanya wifi yako. Ila tayari wifiyo kajazwa ujinga. Kinachomsukuma ni mawazo kuwa urithi wa wanae unapungua kwa kaka yako kuwa na watoto wengine. Anasahau kuwa kaka yako anamlelea watoto wa dume jingine bila kinyongo. Wapambe washamjaza ujinga kwamba talaka itampa haki ya kugawana mali nusu kwa nusu. Na kwa uchumi wa kaka lazima hesabu itakuwa inashawishi ndio maana na mama mkwe kakuchamba aking'ang'ania talaka. Shemeji yangu nae anamsumbua bro kwa ujinga wa namna hiyo. Unaanzaje kuchunguza simu ya mumeo. Anachokitafuta amekipata halafu anachachawa!!
Kama kuna kaukweli hapo dear, ila wanawake malimbukeni ndio huwa wanafanya hivyo!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom