Mwanamapinduzi adai Uhuru Zanzibar

Mwanamapinduzi adai Uhuru Zanzibar

Mkuu kwanza nikufahamishe kuwa uingereza alipewa Tanganyika kuishikilia hadi tutakapokuwa tayari kujitawala... So aliondoka kama tulivyotaka na wao wanatambua hilo haswa. So hakuna Mtanganyika mwenye wasiwasi na muingereza... Jaribu kuwa unatofautisha mambo kwenye mijadara maana inaleta wingi usiohitajika... Ila Zenji inajulikana ni Mali ya mtu aitwae Sultan na hata utajili unaozungumziwa na Wa huyo mtu ukiachia uliuchumaje japo ni wazi aliuchumia bara.. So tunapozungumzia Zanzibar tujikite huko am sure shule ulijifunza namna ya kutofautisha vitu visivyo endana.. Nikisema kijiko,kisu,una na kandambili am sure utaelewa nini kipo tofauti

= mijadala
= utajiri

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Sure ndio huwa nawaambia sana... Kuna Mzungu aloshamtoa nishai mzenji kwa style hiyo...

Usifikiri wazungu hawajui kuwa hapo hakuna muungano ,wanajua kila kitu . Na ndio baadhi ya nchi za magharibi wamewachukua wazanzibari kama wakimbizi kutoka nchi ya Zanzibar Na si Tanzania .Mambo yote hayako black and white kama tunavyofikiri katikati ziko rangi nyengine .ukitaka uthibitisho uliza magazeti makubwa ya nchi za west kuhusu idadi ya wazanzibari Na watanzania waliochukua uraia wa hizo nchi utaambiwa, Nakupa home work wewe Na pascal
 
Hizo zote ni porojo za hapa na pale ukweli unabaki kuwa Zanzibar ni nchi na hilo la kuwa na passport moja ni maelewano ya muungano tu.

Wazanzibari leo hii wana vitambulisho vyao rasmi vya uraia wao, Uzanzibari. Wewe si Mtanzania? Jaribu kwenda Zanzibar uwaambie wakupe kitambulisho uone watakupa kipi. Usishangae wakikwambia hapa hatutoi vitambulisho vya machogo.

Na hivi karibuni washaamua kuwa mafuta na gas ya Zanzibar ni mali ya Wazanzibari pekee, si hasha soon, pia wakaamua kuwa na hati zao za kusafiria ziwe za Kizanzibari.
Kana place of birth kwenye passport ni porojo napata wazi wasi na akili yako pengine unaukichaa au umeamua Ku try ignorance. Na kama unaona uasili Wa mzenji haupotei kwenye passport yake how about ya ile miarabu na mihindi unataka kwenye passport waandike asili zao za Oman,Yemen,Iran,India and Pakistan?
 
= mijadala
= utajiri

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
Tulifuata mfumo Wa lugha ya kijinga ya kiswahili. Maana ya lugha ni kuelewana so kama umeelewa am right for what I wrote. And wewe acha kupandisha dela lako juu. Nilishakukamata na vichapizi vyako kadhaa humu. Sijui nawe huo ujinga ndio mkuu wake
 
Kwa hivyo hayo yaliyotamkwa Na wanasheria kuhusu Latham island ni porojo tu mafuta yanaweza kuchimbwa wakati wowote Na Tanganyika??
Sio porojo, kuna mambo ya muungano na mambo ambayo sio ya muungano, mipaka yote ya nchi ni jambo la muungano, hivyo kila kilichomo ndani ya mipaka ya JMT ni cha JMT, hadi visiwa vyote ndani ya mipaka yetu ni mali yetu kikiwemo kisiwa cha Unguja na Pemba, ndio maana tunafanya chochote kuhusu mali zetu, ile kwenye matumizi ya ardhi sio ya muungano, hivyo Zanzibar iko huru kutumia ardhi yake kwa namna ile jinsi inafaa kwa manufaa yake, ikiwemo kuchimba mafuta.

Paskali
 
Hivi visiwa huwezi kuviacha vitaleta shida
ISIS watafanya makao yao makuu pale halafu watuletee shida huku bara. Isitoshe kutokana na global warming baada ya miaka 100 kakisiwa kote katakuwa kamezama. Watakimbilia wapi hawa wanaodai "uhuru"?
 
Sio porojo, kuna mambo ya muungano na mambo ambayo sio ya muungano, mipaka yote ya nchi ni jambo la muungano, hivyo kila kilichomo ndani ya mipaka ya JMT ni cha JMT, hadi visiwa vyote ndani ya mipaka yetu ni mali yetu kikiwemo kisiwa cha Unguja na Pemba, ndio maana tunafanya chochote kuhusu mali zetu, ile kwenye matumizi ya ardhi sio ya muungano, hivyo Zanzibar iko huru kutumia ardhi yake kwa namna ile jinsi inafaa kwa manufaa yake, ikiwemo kuchimba mafuta.

Paskali

mipaka yote ya nchi ni jambo la muungano, hivyo kila kilichomo ndani ya mipaka ya JMT ni cha JMT

ile kwenye matumizi ya ardhi sio ya muungano, hivyo Zanzibar iko huru kutumia ardhi yake kwa namna ile jinsi inafaa kwa manufaa yake, ikiwemo kuchimba mafuta.


Hapa kuna kizungu mkuti , unaweza kutuelimisha na kutuwekea wazi huu utapeli???
 
ISIS watafanya makao yao makuu pale halafu watuletee shida huku bara. Isitoshe kutokana na global warming baada ya miaka 100 kakisiwa kote katakuwa kamezama. Watakimbilia wapi hawa wanaodai "uhuru"?

hizo ndizo fikra mnazonyweshwa kanisani ???
 
Kwa ni mipaka ya Zanzibar haitambuliki kimataifa?
Ndio zanzibar inatambulika kimataifa, baadhi ya nchi ambazo zinatoa kwa mfano scholarship, lazima utoe idification ya u zanzibar ndio upate scholarship.

Hata unapo omba visa baadhi ya mataifa wanataka card ya u zanzibar kuonesha proved kuwa ni mzanzibari na unapoishi na zanzibar.
 
Hizo zote ni porojo za hapa na pale ukweli unabaki kuwa Zanzibar ni nchi na hilo la kuwa na passport moja ni maelewano ya muungano tu.

Wazanzibari leo hii wana vitambulisho vyao rasmi vya uraia wao, Uzanzibari. Wewe si Mtanzania? Jaribu kwenda Zanzibar uwaambie wakupe kitambulisho uone watakupa kipi. Usishangae wakikwambia hapa hatutoi vitambulisho vya machogo.

Na hivi karibuni washaamua kuwa mafuta na gas ya Zanzibar ni mali ya Wazanzibari pekee, si hasha soon, pia wakaamua kuwa na hati zao za kusafiria za Kizanzibari.
Ahsante

Tatizo la watanganyika wengi hawajitambui, na siku watakayo jitambua ndio tanganyika itakaporudi ,na ndio siku watakayo weka utawala mpya ili kuwapa ukweli halisi wa mambo, huu utawala tulio nao una wavunga vunga, sijui uhuru wa Tanzania bara, hivi kuwa Tanzania bara ili pata uhuru 9 Dec?

Huku nje tunatambuliwa kama wazanzibari, na tuna diaspora zetu kila nchi tulioko wazanzibari, Ingawa tanganyika ijiitayo Tanzania kuweka diaspora zake kutufunika bado nasi tupo mbele.

Tutaendelea na mapambano yakupigania uhuru wa zanzibar kwa ya le mambo ya muungano.

Hata nyie watanganyika bado mnahitajika kupigania uhuru, hivi sasa hamko huru, ukitaka kujua hilo omba passport yako Tanzania, hivyo vikwazo utakavyo viona, ndio utajiona kwamba kweli Tanzania inahitaji kupiganiwa uhuru, wa kitaifa na kimataifa, maana watawala wanatutawala vizuri .
 
Juu
Ndio zanzibar inatambulika kimataifa, baadhi ya nchi ambazo zinatoa kwa mfano scholarship, lazima utoe idification ya u zanzibar ndio upate scholarship.

Hata unapo omba visa baadhi ya mataifa wanataka card ya u zanzibar kuonesha proved kuwa ni mzanzibari na unapoishi na zanzibar.
Usiseme baada ya nchi sema arabuni tu utaeleweka maana wanaamini Zanzibar ni ya waislam.
 
mipaka yote ya nchi ni jambo la muungano, hivyo kila kilichomo ndani ya mipaka ya JMT ni cha JMT
ile kwenye matumizi ya ardhi sio ya muungano, hivyo Zanzibar iko huru kutumia ardhi yake kwa namna ile jinsi inafaa kwa manufaa yake, ikiwemo kuchimba mafuta.
Hapa kuna kizungu mkuti , unaweza kutuelimisha na kutuwekea wazi huu utapeli???
Hakuna utapeli wowote, muungano ni kama ndoa, nchi ni kama nyumba, mali zote za wanandoa ni mali zenu wewe na mkeo, na nyumba ni nyumba yenu, na chumba ni chumba chenu, lakini huko nyumbani na chumbani, kuna tofauti za utawala, mke ndie mtawala wa jikoni, na chumbani kwako, na kuna vitu vyakwako na vya kwake, mfano kijaluba ni cha mkeo, anaweka vitu vyake, fedha za kwenye kibubu ni za mkeo, anazihifadhi kwa matumizi yake ya vitu vidogo vidogo vya kike.

Vivyo hivyo Tanzania ni nchi moja ya JMT, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake kama ilivyo mke kwa jikoni, ardhi yote ya Tanzania ni mali ya JMT, kama ilivyo nyumba kwenye ndoa, ila matumizi ya ardhi ya Zanzibar ni mambo ya ndani, kama ilivyo utawala wa jikoni.

Paskali
 
Hakuna utapeli wowote, muungano ni kama ndoa, nchi ni kama nyumba, mali zote za wanandoa ni mali zenu wewe na mkeo, na nyumba ni nyumba yenu, na chumba ni chumba chenu, lakini huko nyumbani na chumbani, kuna tofauti za utawala, mke ndie mtawala wa jikoni, na chumbani kwako, na kuna vitu vyakwako na vya kwake, mfano kijaluba ni cha mkeo, anaweka vitu vyake, fedha za kwenye kibubu ni za mkeo, anazihifadhi kwa matumizi yake ya vitu vidogo vidogo vya kike.

Vivyo hivyo Tanzania ni nchi moja ya JMT, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake kama ilivyo mke kwa jikoni, ardhi yote ya Tanzania ni mali ya JMT, kama ilivyo nyumba kwenye ndoa, ila matumizi ya ardhi ya Zanzibar ni mambo ya ndani, kama ilivyo utawala wa jikoni.

Paskali


Ulisoma kitabu gani muungano wa nchi ni kama ndoa , au maneno hayo kasema yesu ???

ndoa hiyo ilifungwa na wakatoliki??

Ndoa hiyo ni ya mashoga ???

Mbona yale maneno yako hayasemi kuwa huu ni mfano wa ndoa ??

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar si halali - Profesa Abdul Sharif + Sauti
 
Honestly speaking nimechoka malalamiko yasiyoisha. Hivi ni kitu gani Wazanzbar wanataka kama siyo kuchinjana wao kwa wao, kubaguana kwa misingi ya asili na dini na hatimaye kutesa wanawake na watoto wasiokuwa na hatia?

Ninaona chokochoko hizi ni tamaa za watu wachache ambao hata ukiwauliza kile wnachokitafuta hawakujui zaidi ya visasi na matamanio yasiyohalisi.

Mliambiwa marekebisho ya katiba mkavurunda. Serikali tatu ilikuwa ni njia sahihi na yenye amani iliyo na madhara kidogo kuliko serikali ya kibaguzi wanayoitafuta. Bila serikali ya Muungano hakuna Zanzibar huru kwa wote. Hili mkae mkilijua.

Kwa heri.
Umechoka malalamiko yasioisha pengine wewe ni mmoja wa watawala. Anaenyukuliwa nakupata maumivu ya mnyukuo kamwe haachi kupiga kelele.Umesoma wapi historia ya Zanzibar kuchinjana wenyewe kwa wenyewe. Au unamaana ya watanganyika kuwachinja wapenda amani nawenyeji wa Zanzibar? Mauaji ninayokumbuka yaliofanywa Zanzibar ni yale ya wakuja dhidi ya wenyeji ni 1961 (vita vya Juni)wakati wa uchaguzi na ASP ikielekea kushindwa vibaya. Mauaji mengine ni 1964 yaliofanywa na genge la wakatoliki na mamluki kutoka bara liliongozwa na John Okello,Mganda, baada tena ASP kushindwa kwenye Uchaguzi.na walioshinda ZPPP/ZNP kupewa uhuru na mkoloni wa kiingereza 1963.

Choko choko za sasa zimeletwa tena na mrithi wa ASP, yaani CCM baada tena kushindwa vibaya kwenye uchaguzi na chama cha wazalendo CUF.

Bila serikali ya Muungano kuna Zanzibar huru na yenye mamlaka kamili kwa wote. Hili mkae mkilijua.

upload_2016-12-12_14-30-16.png


Bwana Salim Said Rashid, Katibu wa Kwanza wa Baraza la Mapinduzi, Januari 1964 Zanzibar:

Mwenyenzi mungu akupe umri mrefu zaidi uje kuwa shahidi wa kwanza kutoa mahakamani kuhusu uharamu wa muungano. Wewe ndio pekee uliobaki anaejua ukweli na undani kwa vile wewe ndio mliongozana na Karume kuja Dar kuonana na Nyerere, na baadae Nyerere alikuondosha kijanja eti uwende ukakate nyewele na ulipo rudi mambo ameshamaliza.
 
Power mongers! Simply walafi wa madaraka wenye madai kama haya!
Achana na walafi wa madaraka hao.....asilimia sabini ya watanzania wanaoishi wamezaliwa ndani ya Tanzania....hawajui kitu kinaitwa Tanganyika ni upuuzi mkubwa kutaka kugawa nchi .....kutokana na fikra duni za hivi vizee vichache..ambavyo majira yanasoma saa 12 jioni
 
Back
Top Bottom