Mkuu Ghibuu, Tanzania tuna ndoa za aina tatu, za kimila, za kiserikali na za kidini. Ili ndoa iwe halali, lazima ifungwe kwa ridhaa ya wanandoa.
Ila kwenye ndoa za kimila, mila zetu za Kiafrika zinaruhusu ridhaa ya mwana ndoa mmoja tuu, ambapo ni mume na mke hutakiwa kuolewa kwa lazima atake asitake.
Mfano Kanda ya Ziwa kabila la Wasukuma ridhaa ya ndoa ni mzazi, kwenye ile ngoma yetu maarufu, ya Chagulaga, kinachofanyika ni ubakaji.
Mwanamke akibakwa, kisha akatulia kwenye ndoa na kutimiza wajibu wake wa ndoa, ikiwemo consumation bila kukataa, atahesabika ameridhia na ndoa hiyo inakuwa ni ndoa halali by performance.
Hivyo ndivyo ulivyo huu Muungano wetu. Ulisainiwa na upande mmoja tuu, na ukaridhiwa (ratification) na upande mmoja tuu, wa Tanzania Bara, lakini muungano huo umehalalishwa kwa performance.
Wengine wengi ni wageni humu ila hili tuliisha lizungumza sana humu
Kwa wanaopenda kuujua ukweli na sii wavivu wa kusoma, karibu kwenye rejea hizi
Paskali
https://www.jamiiforums.com/threads/je-wajua-kuwa-zanzibar-haikuridhia-muungano-ina-maana-gani.
https://www.jamiiforums.com/threads...gano-kilichopo-ni-makubaliano-tuu-ya-muungano.
la la hati halisi za Muungano nimelizungumza
Hapa-
Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?!
Na Hapa-
Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?. Kilichopo ni Makubaliano Tuu?!.
Na Hapa-
Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhiaMuungano? Ina Maana Gani?!.
Na Hapa-
Jee Wajua Kuwa Kuna UwezekanoTanzania Sii Nchi Halali Kisheria?!.