Mohammed Hamad
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 3,988
- 1,305
- Thread starter
- #21
I dare to say, kuna watu hata kama walikwenda shule haijawasaidia sana, makala aliyoitoa MMK, ilijaribu kuainisha, kulinganisha na baadae kuweka bayana yale ambayo watu wataanza kujiuliza, kama CDM inadaiwa kuwa ya wachaga na wakristo kwa hoja tu eti kwasababu waanzilishi ni Christians na watu kutoka kilimanjaro, the same persons wanaweza kujiuliza swali hilo hilo juu ya vyama vingine, kama CCM, CUF NCCR-Mageuzi etc. Hapa kipi ambacho hakieleweki...kwanini watu tunapenda kufikiri ndani ya box na si nje? Unapokuwa na watu wa jinsi au aina ya MALARIA SUGU.....Ambao siku zote ukifuatilia post zao wanaongea upuuzi tu, na hakuna unachoweza kuambulia matokeo yake yatakuwa haya. Kila kinachojadilia au kuhojia kinapokuna na neno " Islam" ni negativity mwanzo-Mwisho.
Angalizo: Funguke viumbe mliopumbazika kwa ujinga wa watala wenu. Mnashindwa kujadili kwanini maisha yamekuwa magumu, nini source ya hayo yote tunaangalia upuuzi wa nanma hii..."damn". Jengeni hoja zitakazo mkomboa mtanzania na si habari ya wewe islam wewe christian, yatatufikisha wapi haya.
Wewe the so called Malaria Sugu, unatibu hospital ile ile ambayo haina madaktari, unapeleka watoto wako shule zile zile ambazo hazina vifaa na miundo mbinu nyingine, wewe huyo huyo unatoka kijiji kile kile kama changu ambako hakuna maji wala umeme achilia mbali huduma za afya, nani anapaswa kuyafanya haya, nani anapaswa kuhoji haya. Tubadirike Watanzania, tufunguke macho yetu, achaneni na viongozi wa dini au siasa wanao hubiri ujinga huu.
Hapo kwenye red mkuu sikubaliani na wewe mwenye kujua na aliesoma kama wewe hawezi kusema eti TAA/TANU mpaka CCM ni chama cha waislamu ikiwa kulikuwa na wakristo kindakindaki kama madaktari watano – Dr. Vedasto Kyaruzi, Dr Joseph Mutahangarwa, Dr Wlibard Mwanjisi, Dr Michael Lugazia na Dr Luciano Tsere, patrick kunambi, gerimano pacha, japhet kirilo na l.m. Makaranga.bila kuwashau joseph kimalando na john rupia.
Kwahiyo kimantiki Mwanakijiji analo alilokusudia na si jingine ila kuipembejea CDM na kuutukanisha Uislam! Kama alikuwa na haja na hoja ya kuisafisha TAA/TANU na CCM na waenyeji wa Dar es Salaam ambao ni Wazaramo ila aliona kuwa kina Sykes hawakuwa Wazaramo ametumia ufundi kuisuka hoja yake ili afanikishe malengo yake! Narudia hakututendea haki Waislam mimi nikiwa mmoja wao kwa kuufananisha Uislam na Uchagga ambao ndani ya huo Uchagga kuna waislam pia!
Shukran sana kwakuwa wewe mwenzetu umeenda sana shule na uimekusaidia sana nadhani utakuwa unaelewa mantiki ya mada yangu.