Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
hapo kwenye red , watu kama hawa sijui kama tunao kwenye nchi yetu kwa sasa hivi, na kama wapo ni mmoja kati ya mia moja.Hajasema waislamu watupu bana weee aah! Amewataja wakristo pia tena miongoni mwa hao uliowataja. Kweli hukuona au hukuelewa? ALichokieleza tena kwa kukirudia mara kwa mara kimantiki ni waislamu walikua na influence kubwa sana,tena walishika nafasi nyingi zile muhimu katika vyama hivyo na harakati zake; na nazungumzia nafasi muhimu! (usije tu mathalani ukamtaja mshindo, kwa vile alikua anashika bango la PPT-MAENDELEO basi awemo kwenye historia ya orodha ya waasisi wake).
Mantiki yake pia inaeleza bayana: kuwepo kwao hao waisalamu tena kwa influence kubwa,hakuvifanyi vyama hivyo kuwa vya kiislamu,la hasha! Hawakuvianzisha kwa sababu ya uislamu wao,wala kwa maslahi ya UISLAMU bali ukombozi wa TANGANYIKA,period!
Tukiachana na MKJJ, my take sasa: Hao waislamu waasisi wa TAA,TANU,ASP na CCM,ndio walikua waislamu wa kweli ambao tunapaswa kuwaenzi. Kama Abdulwahid Sykes anaweza kumpisha Julius aongoze harakati na asimwite kafiri,huyo ni mfano wa kuigwa na waislamu wengine. Lakini nina wasiwasi kama wewe ndugu unaweza kufanya hivyo kama ungekua na nafasi hiyo. Hebu nitoe wasiwasi tafadhali!