Mokaze
JF-Expert Member
- Aug 3, 2018
- 14,376
- 14,870
Wakuu salamu zenu.
Nimekaa na kutafakari hali ya maisha yetu sisi binadamu nimeona yapo mithili ya maisha ya kuku bandani.
Kuku anafunguliwa asubuhi kutoka bandani hapo anapata "uhuru" wa kuvinjari na kujitafutia riziki, katika kipindi hicho kumswaga ili arudi bandani sio kazi ya kitoto, ni hadi jioni atakaporejea mwenyewe pindi ameshiba kupitia riziki ya jasho lake, akiwa bandani hapo unaweza kumfanya kitu chochote utakacho kwani wahenga walisema; kuku mali yako manati ya nini ?!, wakati huo unaweza hata kulitia moto banda lote na kuku akateketea au ukaamua kumkamata na kumchinja kwa kitoweo kwani huyo si mali yako bwana!!!.
Kipindi huyo kuku anapokuwa vichakani akijitafutia riziki huko anaweza kugongwa na nyoka, akaliwa na mbwa, akaibwa nk na ukamkosa kabisa, si mnajua lakini??!!.
Sisi binadamu hapa duniani tupo mithili ya kuku bandani, banda letu ndio hii dunia, kila kukicha tuna amka kwenda kutafuta riziki na mihangaiko mingine na jioni kurejea majumbani mwetu, tofauti kubwa kati yetu na kuku bandani ni kwamba angalau kuku anao uhuru na nafasi kubwa ya kutoweka moja kwa moja na mwenye kuku asimpate milele kinyume chake sisi binadamu haiwezekani kumuepuka mmiliki wetu kwani maisha na shughuli zetu zote tunazifanyia BANDANI (Duniani), siku mwenye banda akikasirika na kuamua kulitikisa banda japo kidogo tu, looo!! mara tetemeko la ardhi, Tsunami, mara mafuriko, ukame, vimbunga, magonjwa nk hayo ni baadhi ya majanga ambayo mwenye banda akiamua kuyaleta basi hatuna pa kukimbilia wala pa kwenda kushitaki, si mwenye banda kaamua!!😏
Mfano angalia Turkey na Syria hali inatisha sana kuhusu tetemeko la ardhi.
Basi ndugu zangu, tunapoishi duniani (bandani) katika hali ya faraja na mafanikio tuchukue nafasi hizo kumuabudu na kumshukuru mwenye banda ambaye ndiye ametuweka humu bandani, tumshukuru na tumuabudu asije tujaribu kwa mitihani hiyo migumu wanayopitia binadamu wenzetu lau kama.ni adhabu badi atusamehe makosa yetu na atuepushe na adhabu.
Watu watauliza je; huyo.mwenye banda ni nani??, Mwenye banda (dunia) ni MUNGU mtukufu, sisi ni viumbe wake aliyetuweka humu duniani bila ya sisi kutaka tuwepo humu duniani hivyo sisi ni mali yake tutake tusitake, imepita hiyo.
Nawaambia Atheists; Hatuna ujanja aliyetuweka bandani ni MUNGU kama hampendi ondokeni bandani.
Nimekaa na kutafakari hali ya maisha yetu sisi binadamu nimeona yapo mithili ya maisha ya kuku bandani.
Kuku anafunguliwa asubuhi kutoka bandani hapo anapata "uhuru" wa kuvinjari na kujitafutia riziki, katika kipindi hicho kumswaga ili arudi bandani sio kazi ya kitoto, ni hadi jioni atakaporejea mwenyewe pindi ameshiba kupitia riziki ya jasho lake, akiwa bandani hapo unaweza kumfanya kitu chochote utakacho kwani wahenga walisema; kuku mali yako manati ya nini ?!, wakati huo unaweza hata kulitia moto banda lote na kuku akateketea au ukaamua kumkamata na kumchinja kwa kitoweo kwani huyo si mali yako bwana!!!.
Kipindi huyo kuku anapokuwa vichakani akijitafutia riziki huko anaweza kugongwa na nyoka, akaliwa na mbwa, akaibwa nk na ukamkosa kabisa, si mnajua lakini??!!.
Sisi binadamu hapa duniani tupo mithili ya kuku bandani, banda letu ndio hii dunia, kila kukicha tuna amka kwenda kutafuta riziki na mihangaiko mingine na jioni kurejea majumbani mwetu, tofauti kubwa kati yetu na kuku bandani ni kwamba angalau kuku anao uhuru na nafasi kubwa ya kutoweka moja kwa moja na mwenye kuku asimpate milele kinyume chake sisi binadamu haiwezekani kumuepuka mmiliki wetu kwani maisha na shughuli zetu zote tunazifanyia BANDANI (Duniani), siku mwenye banda akikasirika na kuamua kulitikisa banda japo kidogo tu, looo!! mara tetemeko la ardhi, Tsunami, mara mafuriko, ukame, vimbunga, magonjwa nk hayo ni baadhi ya majanga ambayo mwenye banda akiamua kuyaleta basi hatuna pa kukimbilia wala pa kwenda kushitaki, si mwenye banda kaamua!!😏
Mfano angalia Turkey na Syria hali inatisha sana kuhusu tetemeko la ardhi.
Basi ndugu zangu, tunapoishi duniani (bandani) katika hali ya faraja na mafanikio tuchukue nafasi hizo kumuabudu na kumshukuru mwenye banda ambaye ndiye ametuweka humu bandani, tumshukuru na tumuabudu asije tujaribu kwa mitihani hiyo migumu wanayopitia binadamu wenzetu lau kama.ni adhabu badi atusamehe makosa yetu na atuepushe na adhabu.
Watu watauliza je; huyo.mwenye banda ni nani??, Mwenye banda (dunia) ni MUNGU mtukufu, sisi ni viumbe wake aliyetuweka humu duniani bila ya sisi kutaka tuwepo humu duniani hivyo sisi ni mali yake tutake tusitake, imepita hiyo.
Nawaambia Atheists; Hatuna ujanja aliyetuweka bandani ni MUNGU kama hampendi ondokeni bandani.