Wana JF,
Maadam JF ni ukumbi wetu, na sisi humu JF, tuko members wengi, na tumefanya mengi, hivyo mimi member mwenzenu Pascal Mayalla, naomba niwe wa kwanza, kuwajulisha wana JF wenzangu, ili kuwapa ile JF advantage ya wewe kama Mwana JF, be the first to know kuwa CCM ndio inakwenda kushinda uchaguzi mkuu huu kwa a landslide victory ya ushindi wa kishindo, kwa pande zote mbili za Muungano!
Ushindi huu ni kufuatia mimi mwana JF mwenzenu, Pasco Mayalla, nimesikia sauti ndani ya moyo wangu, yaani voices from within, kuwa katika uchaguzi huu, mshindi ni CCM!. Hii voices from within, is never wrong, maana ni sauti yake YEYE mwenyewe!
Kwa upande wa Tanzania Bara, CCM itashinda kwa kishindo kwasababu ya track record ya Magufuli, itaibeba CCM na kushinda kwa kishindo.
Kwa upande wa Zanzibar, kwa mujibu wa katiba, rais wa Zanzibar ni mjumbe wa cabinet ya JMT, Muundo wa serikali ya JMT, hatuna serikali ya mseto, ushindi ni by a simple majority, hata akishinda kwa kura moja, ni mshindi, and the winner takes it all. Hivyo mshindi wa Zanzibar lazima iwe ni CCM!.
Nawatakia maandalizi mema ya October 28, sio kwenda kuchagua, bali kwenda tuu kuthibisha kilichochaguliwa tayari kwa ajili tuu ya kukamilisha taratibu za mchakato wa kukamilisha uchaguzi, kama ni kuchagua, watu siku nyingi, wameisha chagua mioyoni mwao, tarehe 28 ni kukamilisha tuu taratibu.
Pasco,
The First