Eng. Burton A. Bukuku;wakati mimi namwona Kikwete bomu, kuna wengine wanamuona mzuri sana, wakati wengine wanamuona Nyerere mzuri wengine wanajuta hata kumjua!
Hizi ni caliber za binadamu na haijaandikwa mahali kuwa ukiwa unasema ubaya wa Nyerere lazima useme na uzuri wake. Na mtego huu ndio kila siku huwa mnauvaa sana, hakuna mahali kuwa ukisema ubaya wa Nyerere basi laizma useme na mazuri yake.
Nilitaka unieleze makosa ya Nyerere ukiwa mtu huru, jaji huru asiye na upendeleo wowote. Lakini upenzi unazidi sana kuliko kuismamia ukweli.
Ukweli ni kuwa JK ni baba wa taifa, ni kweli alikuwa na mapungufu yake mengi tu, nataka uyaseme hayo --orodhesha na ukiyasema hayataondoa ukweli kuwa Nyerere ana mazuri yake!!
Mkuu Bukuku, nakubaliana nawewe kabisa kuwa mwalimu kama binadamu alikuwa na mapungufu yake. Katika moja ya hotuba zake za mwisho alisema, 'mchukue yale mazuri yetu na muache yale mabaya'. Amekiiri hadharani kwa kinywa chake. Mimi mara zote nimekuwa nikiyasema yale ambayo sikuridhika na utendaji au utekelezwaji wake.
Tatizo linakuja pale kunapokuwepo na chuki, ima ya kuzaliwa au ya kujifunza dhidi ya Nyerere. Fikiria mtu anaposema Nyerere alikuwa mkabila, hiyo ni sawa kwa maoni yake, lakini aende mbali nakututhibitishia kuwa alikuwa mkabila kwa ABCD.
Mtu anaposema alikuwa mdini, fair! lakini athibitishe bila shaka udini wa Nyerere. Tena hili la udini hata mwandishi Mohamed Said tumejadiliana naye mwezi mzima hapa JF hakuweza kuthibitisha kisomi udini wa Nyerere zaidi ya hisia na hadithi za kusikia. Sasa limejirudia ndio maana tunauliza na si kutetea historia ya Nyerere; 1) Tuthibitishiwe ukabila wake. Hadi sasa hakuna aliyethibitisha.
2) Tuthibitishiwe udini wake, hakuna aliyejitokeza n.k.
Hii maana yake ni nini! tutaambiwa siku moja Nyerere alikuwa Mchina, tunakubali. Siku nyingine alikuwa mdogo wake Dikteta Ngweso, tunakubali. Mama yake alizaliwa ukoo wa Hitler, tunakubali. Yote haya yatajumuishwa na mwendesha mashitaka ili aorodhesha makosa 100 ya Nyerere na kutaka hakimu atoe hukumu bila ya uthibitisho. Hapa ndipo wengine tunasema hapana, tuna akili zetu, tumeishi nyakati za mwlm tunamjua tupeni uthibitisho. Kabla ya hukumu tuthibitishiwe madai dhidi yake.
Kwa vile mara nyingi huwa hawana uthibitisho ya mabaya yake basi sisi tuna uthibitisho wa mema yake ndio linapokuja suala kutaja mazuri yake.
Bukuku inapotokea mtu akasema Nyerere alikuwa mbaya sana kwasababu alikataa kuleta TV, hivi kuna njia gani rahisi ya kumsaidia mtu huyu kama si kumweleza uzuri wa mambo mengi aliyoyafanya kuliko TV.
Siwezi kusema tu hapana ulikuwa uamuzi mzuri kutokuwa na TV nakaishia hapo, nitakuwa nimetumbukia katika mtego wa kudhani bila ushahidi, nitaeleza kwanini TV haikuwa muhimu kuliko elimu na afya na hapa ndipo nalazimika kutaja mema ya Nyerere.
Tufanye hivi: Maswali ni mengi hebu tuanze na haya mawili kwanza, tuelezwe ukabila na udini wa Nyerere.
Mkuu Bukuku fungua pazia ili wenye hoja wakuunge mkono nasi tuelimike.Hakuna sababu ya kutaja mazuri tuanze na haya mawaili tu. Ukabila na Udini wa Nyerere kwa vithibitisho!