Mwakyembe unaua bandari yetu

Serikali sasa itupe macho kwa vigogo wa TRA na bodi yote imeoza kuanzia kamishina mkuu hadi makamishina wa chini yake ni uozo mtupu na kama serikali itaendelea kulala nchi inaliwa mbaya,

........
 
Robato tunashukuru kwa kujitambulisha waziwazi kuwa mfanyakazi wa bandari. Unafikiri wizi mliofanya haujatosha? Ofisi yenu kumbe ovyo kabisa hakuna taratibu! Wewe kupokea maelekezo toka kwa wakubwa hutaki. Mmeshazoea kupitisha makontena ya pembe za ndovu, wizi wa mafuta na kutuibia bidhaa zetu zinazoenda na kuja. Kama vipi acha kazi kwani lazima ufanye kazi hapo. Mwakyembe tunakuombea kila siku Mungu akupe afya njema. Tanzania ni tajiri sana ila inaliwa na kina Robato.
 
Malafyale kaza uzi vijana wamezoea kula rushwa hao...cut them into their sizes.
 

Tena waambie wenzako kua ule mchezo wa kuchomoa vifaa kwenye magari yetu tunayoagiza nje utawatokea puani karibuni.
 
Mafisadi walia..., mafisadi waliaa.... wakatiwa mirija.....x2
walipo tangaziwaa ... walipo tangaziwaa... usafishaji bandarini..x2
na huo ndio mwanzo .... na huo ndio mwanzo..... kimbunga chakaribia....x2
mtajuta,.. kuishi..mtajuta kuishi kwa pesa za usisadi.....
 
Moja ya Matatizo aliyoelezwa Kikwete na wafanyabiashara wa Oman ni URASIMU na kila siku unaongezeka. Ukitaka kuwekeza mathalan katika Kilimo cha Mpunga kwanza waone TIC, Kisha BRELA, TRA, RUBADA, Halmashauri, Kijiji etc na kote huko RUSHWA tupu. Na kila kukicha sharia zinazidi kuongeza URASIMU.

Nafikiri Mwalimu huyu wa wife wangu (Admin Law) Dr Harrison Mwakyemba pamoja na nia nzuri aliyonayo lakin aangalie namna ya kupunguza URASIMU kwani wafanyakazi wake Serikalini anawajua mwenyewe na BANDARI ni chombo cha biashara chenye ushindani wasije wafanyabiashara wakakimbilia Mombasa au msumbiji.

Lakin kama ubabaishaji na izi Mwakyembe anajulikana sana hana upendeleo anasimamia Haki tu toka akiwa UDSM.
 

Mmezoea nyinyi..
 
Mwakyembe huyo! Huyu sio kati ya wale walikuwa na tumbo la kuharisha wakati tume ha kukusanya maoni inapita
 
SAFI SANA MHESHIMIWA MWAKYEMBE! Ukiona watu wanapiga kelele basi shikilia hapo hapo! Umebana michezo michafu. Big up!
 
Ukisikia kelele kama hizo, ujue mmebanwa sana. Mwakuyembe usiyumbishwe na wachumia tumbo, Sekta ya Umma inahihitaji watu kama Mwakyembe
 
Historia inanifundisha kwamba, "mageuzi" anayoyafanya Dr. Harrison Mwakyembe kwenye upande wa "Mamlaka ya Bandari" yana "makusudio maovu"...!

Wakati utasema...!
 
Unataka Mwakyembe hawaache mfanye kazi gani iliyowashinda kitambo.Mgekuwa mnafanya kazi bandari yetu ingekimbiwa na wateja kibao toka nchi jirani mapato yote sasa yanaenda Mombasa na Durban kwa taarifa yako hata wa TZ wanatumia bandari ya Mombasa baada ya huduma zenu kudorora na ukithiri kwa wizi hapo kwenu.
It seems Mwakyembe has stepped on your toes but what his doing has been long overdue
.
 

wewe inaonekana una maslahi yako pale bandarini:Huna kazi yoyote unayotaka kufanya zaidi ya ufisadi uliouzoea.Acha mwakyembe afanye kazi na si wewe papa usiyeshiba.
 
Bado nabaki kusema kuwa uamuzi aliouchukua ni sahihi maana kama ofisi za wizara zipo Dar na si mbali na bandari sasa tatizo liko wapi?

Huo ucheleweshaji unaousema mbona hata kabla ya kufanya maamuzi hayo ulikuwepo?

Bahati mbaya mtazamo wako unakuambia kuwa kuna watu wanadandia treni kwa mbele na ipo siku utakuambia wanadandia ndege kwa mbele ila jua kuwa kila kitu kina wakati wake na mambo hubadilika kulingana na wakati na wakati huu ndio bandari mambo yanabadilika hivyo la msingi kama binadamu ambaye una uelewa mpana huwezi shangaa sana ni kwanini kuna mabadiliko hata kama hayakufurahishi.

Tanzania ni yetu na kila mtu ana namna ambayo anaona inafaa katika kuleta ufanisi na maendeleo hivyo kama unaona jambo fulani haliendi kama unavyodhani na kutaka basi unaweza kutoa ushauri kwa njia sahihi na si kushutumu mtu binafsi.
 
mnatakiwa mkomeshwe....nashangaa J.K akishakuja hapoo lakini sijui matokeo yake nini......sasa ameingia muhusika mkuu...huwezi mkafaidi wizi wa kuibia watanzania wema halafu mnanuna mkidhibitiwa kama hela haikutoshi hapo..kaanzishe kibanda cha kuuza maji.....
 
Aahaha a a a a Nyampala Mwakyembe kawashika pabaya, na bado mtalia zaidi ndiyo mtaanza kwenda benki mwisho wa mwezi mlikuwa mmezoea kutuuibia.
 
Leo ndo unajua time is money,mnakalisha makontena ya wa2 miez hapo mlikuwa hamuon muda iyo mos,pil usitak kuudanganya uma siku iz hata porin modem ya tigo inakamata,wizara zote na vitengo vyote vina system ya internet ambayo document za aina yoyote zina2mwa within a second usifikir utatoka na baiskel hapo kwenu kupeleka documents wizaran..,unacholilia ww ni mrija umekatwa.,pole mkuu hata shetan anamwisho ulifikir neema iyo...
 
Naomba unijibu maswali haya
1.Mbumbumbu aliye wizarani ni nani huyo?
2.Kwanini unasema awaache mfanye kazi wakati kazi yenu haikuwa na ubora toka mwanzo?
3.Kwanini unafikiri Mwakyembe ni mtaka sifa na si mtendaji?
4.Unasema tusubiri tutakuja kuona kwani kuna kitu gani mnataka kufanya?
5.Kwanini usitoe ushauri utakaomsaidia mwakyembe ila we unakimbilia kusema akuachie ufanye kazi?
6.Utatuhakikishia vipi kama we si mhanga wa operation za Mwakyembe?
7.Kwa kadiri unavofikiri malengo ya Mwakyembe au nia yake au dhamira yake ni mbaya au nzuri?kwa manaeno mengine unafikiri Mwakyembe anataka kuiua bandari?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…